Nilihoji utambulisho wa Mohammed Dewji Michuano ya AFL lakini niliishia kushambuliwa na wana Simba!

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
10,260
12,758
Nimeshangazwa kuona kelele za mashabiki zikishinikiza kuwa Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Mangungu ajiuzulu baada ya Simba SC kupokea kichapo cha goli 5 kwa 1.

Mashabiki wapiga kelele bila kutafakari kuwa Mwenyekiti Mangungu ni Mwenyekiti kivuli tu hana nguvu kiutendaji wa kazi kama ilivyo kwa Eng. Hersi, bali Mtendaji Mkuu ni Mo Dewji, ndiye aliyejificha kwenye kivuli cha Murtaza Mangungu.

Mo Dewji ndiye aliyesimamia uchaguzi wa wenyeviti taifa mpaka kupatikana kwa Mangungu.

Mo Dewj ndiye aliyesimamia zoezi la kumleta Manzoki kuja kuwadanganya wana Simba SC ili wamchague Mangungu amtumie vizuri katika mambo yake.

Ujio wa Mh. Rais katika Simba Day ulifuata protocol za kiusalama na ndiyo maana Murtaza Mangungu na Try again walionekana WAKIWA karibu na Mh. Rais, lakini Mo Dewji kikatiba ya Simba SC hatambuliki lakini alifanya kazi ya MC na kusoma makala ya mchongo mbele ya Mh. Rais ukifuata kanuni hiyo ni kazi ya Ahmedy Ally.

Rais wa Heshima hana mamlaka yoyote na kutambulishwa kwenye ufunguzi wa African Super League.

Murtaza Mangungu alipaswa kutambulishwa pale ila Mo Dewj alifunika na kukandamiza Katiba ya Simba SC.

Kwa hayo machache mashabiki hawapaswi kupaza sauti kuwa Mangugu ajiuzulu wakati na yeye anakandamizwa na Mo Dewji, kwa hiyo mzizi mkubwa ni Mo Dewji na huyo ndiyo anapaswa kujiuzulu/kujitoa Simba SC.
 
Nimeshangazwa kuona Kelele za mashabiki zikishinikiza kuwa Mwenyekiti wa Simba sc Murtaza Mangungu ajiuzulu baada ya Simba sc kupokea kichapo Cha goli 5 kwa 1.

Mashabiki wapiga Kelele Bila kutafakari kuwa Mwenyekiti Mangungu ni Mwenyekiti kivuli tu Hana Nguvu kiutendaji wa kazi Kama ilivyo kwa Eng hers Bali mtendaji mkuu ni Mo dewji ndiye aliyejificha kwenye kivuli Cha Murtaza Mangungu.

Mo dewji ndiye aliyesimamia uchaguzi wa wenyeviti taifa mpaka kupatikana kwa Mangungu.

Mo dewj ndiye aliyesimamia zoezi la kumleta Manzoki kuja kuwa danganya wanasimba Sc ili wamchague Mangungu amtumie vizuri katika Mambo yake.

Ujio wa Mh RAIS katika Simba day ulifuata protocol za kiusalama na ndiyo maana Murtaza Mangungu na Try again walionekana WAKIWA karibu na MH RAIS lakini Mo dewj kikatiba ya Simba Sc hatambuliki lakini alifanya kazi ya MC na kusoma makala ya mchongo mbele ya Mh RAIS ukifuata kanuni hiyo ni kazi ya Ahmedy Ally.

Raisi Wa Heshima Hana mamlaka yoyote na kutambulishwa kwenye ufunguzi wa African Super league.

Murtaza Mangungu alipaswa kutambulishwa pale Ila Mo dewj alifunika na kukandamiza katiba ya Simba Sc.

Kwa hayo machache Mashabiki hawapaswi kupaza sauti kuwa Mangugu ajiuzulu wakati na Yeye ana kandamizwa na Mo dewji kwa hiyo mzizi mkubwa ni Mo dewji na huyo ndiyo anapaswa kujiuzulu/kujitoa Simba sc.
nashindwa kuelewa kwamba Mo ni Mfadhili?Mmilik? Rais wa Club au Mkt wa club?
 
Bado hujasema.

Utatoa kila sauti
IMG-20231105-WA0073.jpg
 
Back
Top Bottom