MKURABITA
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 317
- 126
Ndugu wana JF, mtakumbuka kuwa hivi karibuni Chuo kikuu cha Dodoma UDOM wametangaza nafasi nyingi za ajira, ambazo mwisho wa kutuma maombi itakuwa tar. 10 Sept.
Leo nimepeleka barua ya maombi ya rafiki yangu. Nilichokiona pale masijala ya UDOM mpaka nimeogopa. Nimekuta wahudumu wakichambua barua kulingana na nafasi za kazi. Kwa ufupi ni kwamba maombi ni mengi kupita maelezo. Na kwa dokezo nililopewa na mmoja wa wahudumu, kuna uwezekano mkubwa ili kukata mzizi wa fitina, kuwaita wote walioomba na kuwapa written paper kabla ya kushortlist watakaofaulu na kuwaita kwenye oral interview.
Ushauri wangu wote waliotuma application UDOM: Kama utaitwa kwenye intervie, ni vizuri ujiandae kifedha kwani kuna uwezekano kipindi hicho watu wakawa wengi sana hivyo kukawa na scarcity ya malazi na gharama kupanda kwani Dodoma bado Hotel na Guest Houses si nyingi.
Nimegundua leo kuwa huu mfumo wa Serikali kutaka kila mtu aende University utaighalimu nchi. Ni vema wangejenga vyuo vingi vya ufundi ili kupunguza msongamano wa kila mtu kutaka kuajiliwa. Ikumbukwe kuwa vyuo vikuu vyetu vingi vina programmes na mitaala ambayo haimjengi mtu kujiajili.
Nawatakia kila la kheri wote mlioomba ajira.
Leo nimepeleka barua ya maombi ya rafiki yangu. Nilichokiona pale masijala ya UDOM mpaka nimeogopa. Nimekuta wahudumu wakichambua barua kulingana na nafasi za kazi. Kwa ufupi ni kwamba maombi ni mengi kupita maelezo. Na kwa dokezo nililopewa na mmoja wa wahudumu, kuna uwezekano mkubwa ili kukata mzizi wa fitina, kuwaita wote walioomba na kuwapa written paper kabla ya kushortlist watakaofaulu na kuwaita kwenye oral interview.
Ushauri wangu wote waliotuma application UDOM: Kama utaitwa kwenye intervie, ni vizuri ujiandae kifedha kwani kuna uwezekano kipindi hicho watu wakawa wengi sana hivyo kukawa na scarcity ya malazi na gharama kupanda kwani Dodoma bado Hotel na Guest Houses si nyingi.
Nimegundua leo kuwa huu mfumo wa Serikali kutaka kila mtu aende University utaighalimu nchi. Ni vema wangejenga vyuo vingi vya ufundi ili kupunguza msongamano wa kila mtu kutaka kuajiliwa. Ikumbukwe kuwa vyuo vikuu vyetu vingi vina programmes na mitaala ambayo haimjengi mtu kujiajili.
Nawatakia kila la kheri wote mlioomba ajira.