Nilichokigundua kuhusu watanzania, mara baada ya kuwatoa watoto wangu English Medium na kuwaleta Kayumba

Bongotunacheza

JF-Expert Member
Dec 7, 2018
733
1,677
Ni kwamba hawa watu wa mtaani kwetu wananiiga au na wao uchumi umewapiga kama Mimi.

Ni hivi niliwahi kuandika Uzi hapa nikisema nimeamua kuwatoa watoto wangu English Medium na kuwaleta Kayumba baada ya uchumi wangu kuzorota. Then nikaja nikaanzisha Uzi kuhusu FAIDA binafsi nilizo zipata baada ya kuwahimishia watoto wangu Kayumba.

Leo nimeenda shuleni kulikuwa na kikao cha wazazi. I was surprised KUKUTANA na watu zaidi ya kumi ambao na wao watoto wao walikuwa wanasoma English Medium na sasa wamewahamishia Kayumba.. Nilishindwa kupata jibu je ni kwamba hawa jamaa wana niiga Mimi au na wao uchumi umewapiga kama Mimi?

Kati yao kumi ni mmoja ndio Nina uhakika kwa asilimia mia kwamba amewahamishia watoto wake Kayumba kwa sababu ya kunigeza Mimi au at least kuwa inspired na Mimi.

Niliambiwa na mtu kwamba huyu jamaa aliwahi kusikika bar akiwaambia watu anawarudisha watoto wake Kayumba kwa sababu uchumi umekuwa mgumu. Akasema " Kama ( jina langu) nimewarudisha watoto wangu Kayumba yeye ni nani asiwarudishe?

Ni hivi hapo mtaani kwetu ( uswahilini) Mimi ninachukuliwa kama kijana mwenye uwezo kifedha.

Ila ukweli ninaujua Mimi mwenyewe ninapitia kipindi kigumu kiuchumi.. Ndio maana niliamua kuwarudisha watoto wangu shule ya Kayumba.

Mimi kuwarudisha watoto wangu Kayumba ilikuwa ni habari iliyo enea mtaa mzima..

Najua baadhi ya watu watakuwa wamefurahi kwa sababu kwao hilo linamaanisha anguko langu..

Hata hivyo leo nimekuja kugundua kwamba, Kumbe ni watu wengi tu hapo mtaani ambao walikuwa wanasomesha watoto wao English Medium walikuwa wanaumia kimya kimya ila walikuwa hawajui cha kufanya kwa sababu walikuwa wana ogopa macho na maneno ya watu ndio maana wengi wao walikuwa wanaishi kwa stress ilimradi ionekane watoto wao wanasoma English Mediums.

Nilipo watoa watoto wangu English Medium.na kuwaleta Kayumba, wazazi wengi wamefuata njia, now wanawatoa watoto wao English Mediums na kuwaleta Kayumba..

Nilicho kigundua kuhusu watanzania wengi ni kwamba wengi wanafanya mambo kwa ajili ya kujionyesha kwa watu. Kwa ajili ya approval and validation from other people.

Kwako ewe Mtanzania. Fanya kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wako. Ishi maisha yako halisi usiishi kuwa impress watu.
 
Umecopy na kupaste uzi wa LIKUD
Hapana hajacopy wala kupaste Uzi wangu ila maudhui yake yanafanana na maudhui ya Uzi nilio wahi kuutoa. Mimi nipo against na shule za English Medium za waswahili na ambazo hazipo chini ya taasisi. To me ili niweze kuiita English Medium, at least ada yake iwe milioni kumi kwa mwaka. Chini ya hapo najua ni ubabaishaji tu. Hiyo milioni 1 na nusu au mbili au 3 au 4 kwa mwaka bora nikalewe bar kuliko kumpeleke Mr. MUGETTA akalewe...

English Mediums za m.1 point tano , 2,3ms kwa mwaka ni Kayumba ambazo zinafundisha kwa KIINGEREZA period
 
Hapana hajacopy wala kupaste Uzi wangu ila maudhui yake yanafanana na maudhui ya Uzi nilio wahi kuutoa. Mimi nipo against na shule za English Medium za waswahili na ambazo hazipo chini ya taasisi. To me ili niweze kuiita English Medium, at least ada yake iwe milioni kumi kwa mwaka. Chini ya hapo najua ni ubabaishaji tu. Hiyo milioni 1 na nusu au mbili au 3 au 4 kwa mwaka bora nikalewe bar kuliko kumpeleke Mr. MUGETTA akalewe...

English Mediums za m.1 point tano , 2,3ms kwa mwaka ni Kayumba ambazo zinafundisha kwa KIINGEREZA period
Daaah wewe ni kichaa unayejitambua

Over
 
Ajira zenyewe zipo wapi mkuu? Usiseme watajiajiri kwa sababu in Tz both Kayumba na English Mediums wanamuandaa mtoto kuajiriwa..
Maandalizi ya mtoto yanaanzia nyumbani ili aje kua nani.
Shuleni mtoto anaenda kupewa maarifa ili yamsaidie huko duniani akija kuanza kuishi.
Kwahivyo........
Swala la mtoto atakua nani ni jukumu la mzazi pamoja na mtoto mwenyewe.
Kumbuka shuleni sio jukumu lao kumuandaa mtoto ajekua nani...😊
Lakini pia ajira iwepo ama isiwepo, nature inatutaka kwamba maisha lazima yaendelee...🤗
 
Halafu wakimaliza shule na kupata kazi waanze kuimba " Nani kama mama"
Nyie ndo mnakufaga kwa presha uzeeni
Baba bora niyule anae wajibika kwa mtoto/watoto wake, hii haijalishi kwamba mtoto anampenda mama zaidi ya baba.
Watoto wako ni matokeo ya starehe zako, na mwisho wa siku hakuna mtoto alie kuomba umzae.
By the way..........
Baba kama wewe ndio wababa wajinga na wapumbavu wenye fikra za kusomesha watoto wao ili wakifanikiwa waje wawe msaada kwao.
Wewe kama baba unapaswa kujiandalia maisha yako ya uzeeni ili uzeeke vizuri.
 
Baba bora niyule anae wajibika kwa mtoto/watoto wake, hii haijalishi kwamba mtoto anampenda mama zaidi ya baba.
Watoto wako ni matokeo ya starehe zako, na mwisho wa siku hakuna mtoto alie kuomba umzae.
By the way..........
Baba kama wewe ndio wababa wajinga na wapumbavu wenye fikra za kusomesha watoto wao ili wakifanikiwa waje wawe msaada kwao.
Wewe kama baba unapaswa kujiandalia maisha yako ya uzeeni ili uzeeke vizuri.

Ur still a learner mkuu.

Nani alie kudanganya kwambia kulipa mamilioni English Mediums ndio kuwajibika kwa watoto wako? Nani huyo tumtafute tukamchape?

Elewa neno " kumchapa"
 
Maandalizi ya mtoto yanaanzia nyumbani ili aje kua nani.
Shuleni mtoto anaenda kupewa maarifa ili yamsaidie huko duniani akija kuanza kuishi.
Kwahivyo........
Swala la mtoto atakua nani ni jukumu la mzazi pamoja na mtoto mwenyewe.
Kumbuka shuleni sio jukumu lao kumuandaa mtoto ajekua nani...😊
Lakini pia ajira iwepo ama isiwepo, nature inatutaka kwamba maisha lazima yaendelee...🤗
Hizo shule za English Medium wanampa mtoto maarifa gani ya kumsaidia huko duniani akija kuanza kuishi?
 
Back
Top Bottom