Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,883
- 2,763
Zaidi ya marehemu Regia kuwa mwanachama wa jf, pia alikuwa mwanasiasa. Wa chama gani, hapa ndio penye uzito wa mada hii. Ni ukweli usiofichika kuwa Regia alipendwa na kukubalika ndani na nje ya jf. Na alikubalika zaidi baada ya kujianika kuwa yeye ni nani na ana nia gani. Sote tukajua kumbe yule (nani tena?) ndio Regia?! Harakati zikaanza na mwisho akawa mbunge, japo si ule ubunge aliotarajia.
Akawa anatoa michango yake humu kwa mujibu wa ilani ya chama chake cha cdm na kina sie tukawa tunamsapoti kwa hali na mali. Japo walikuja wadau wa ccm na kusema yale ya chama chao lakini bado waliishia kupondwa na makopo. Nnape mmojawapo. Jf ikawa na mapenzi na Regia na chama chake.
Tuliposikia taarifa za msiba wake jf yote (ukiacha kundi la wachache wanaojulikana) ikazizima kwa kutoamini kilichotokea. Mengi yakaandikwa kumhusu Regia lakini mengi zaidi kuhusu maisha yake ya kisiasa maana ndio tumemjua zaidi hapo. Jf ikapanga mikakati na namna ya kumuenzi huyu dada kwa yele yote aliyoyaanzisha akiwa na nia ya kuyatekeleza, mojawapo likiwa ni kukusanya maoni ya nini cdm iwafanyie wananchi.
Moja ya azimio la mkutano wa marafiki wa Regia ni kuendeleza aliyoyaacha na wanajf wengi wanakubali hili. Kwa lugha nyingine kuendeleza yale mawazo ya kutekeleza ilani ya cdm, na hii imekuwa na impact kubwa sana kwenye nafsi za watu. Ndipo katika kuwaza na kutafakari nikagundua kuwa jamii inataka mabadiliko ya kimfumo. Regia hakupendwa kama yeye tu bali alipendwa zaidi kama mwana chadema. Tafakari...
Akawa anatoa michango yake humu kwa mujibu wa ilani ya chama chake cha cdm na kina sie tukawa tunamsapoti kwa hali na mali. Japo walikuja wadau wa ccm na kusema yale ya chama chao lakini bado waliishia kupondwa na makopo. Nnape mmojawapo. Jf ikawa na mapenzi na Regia na chama chake.
Tuliposikia taarifa za msiba wake jf yote (ukiacha kundi la wachache wanaojulikana) ikazizima kwa kutoamini kilichotokea. Mengi yakaandikwa kumhusu Regia lakini mengi zaidi kuhusu maisha yake ya kisiasa maana ndio tumemjua zaidi hapo. Jf ikapanga mikakati na namna ya kumuenzi huyu dada kwa yele yote aliyoyaanzisha akiwa na nia ya kuyatekeleza, mojawapo likiwa ni kukusanya maoni ya nini cdm iwafanyie wananchi.
Moja ya azimio la mkutano wa marafiki wa Regia ni kuendeleza aliyoyaacha na wanajf wengi wanakubali hili. Kwa lugha nyingine kuendeleza yale mawazo ya kutekeleza ilani ya cdm, na hii imekuwa na impact kubwa sana kwenye nafsi za watu. Ndipo katika kuwaza na kutafakari nikagundua kuwa jamii inataka mabadiliko ya kimfumo. Regia hakupendwa kama yeye tu bali alipendwa zaidi kama mwana chadema. Tafakari...