Billie
JF-Expert Member
- Aug 13, 2011
- 12,791
- 20,014
Nakumbuka nilipokuwa mdogo levo za primary hadi form one.Nilikuwa mtundu sana hadi kupelekea kuwa nachapwa mara kwa mara na mama ili nibadilike.Namshukuru MUNGU nilibadilika baada ya kuchapwa mfururizo ndani wiki nzima hapo ndipo nikawa mtoto mzuri kwa kweli nazishukuru bakora kwa vile zilinibadilisha tabia.Tukirudi maisha ya leo fimbo zimekuwa zikizuiliwa kuanzia mashuleni hadi nyumbani na ustaarabu mbadala ni kujadiliana na mtoto kueleza anayotakiwa kufanya na sio kumchapa pia nikicheck movie nyingi za ulaya na marekan nimegundua fimbo haitumiki kabisa.Nina ka son kangu kana mwaka mmoja nashindwa kuamua nitumie mtaala wa bakora au majadiliano kwenye ukuaji wake ili baadaye nipate mtoto mwenye maadili mazuri? WAZAZI TUSAIDIANE KULIJADILI HILI hapa MMU.