Nidhamu ya Chama: Kiini cha Kudorora Viongozi wa CCM!

Mkuu MKJJ,

Hii mikwara ya akina Ndejembi na Kimaro ni ya kitoto, ya kijinga na imepitwa na wakati. Inawezekana wametumwa au wamekurupuka. Either way wanatia aibu.

MwanaCCM yeyote anayekidhi vigezo vya kugombea urais atakayeogopa kuchukua fomu kwasababu ya hii mikwara nae ni ****.

Sasa nasubiri kuona reaction ya Mheshimiwa Kikwete. Mi ningekua yeye, at the earliest opportunity ningesema something to the effect, "Ndugu wanaCCM wenzangu, nashukuru kwa support yenu, ila kwa wale wanaopiga mkwara wanachama wengine wasijitokeze kugombea urais ningewaomba wasitishe hizo kauli. Kazi niliyoifanya inaonekana na ndo itakua msingi wangu wa kuwaomba Watanzania kura zao niendelee kuwaongoza".

Hii ni fursa kwa Mheshimiwa kuonesha political maturity. Wale wanaotoa kauli za mkwara hawamsaidii bali wanamkwaza. Wamem-preempt aoneshe kwamba hahitaji kupigwa chepuo. Akikaa kimya atadhihirisha kwamba kweli yeye ni kiongozi dhaifu aliyeshindwa kazi aliyowaahidi wananchi na anahitaji kupigwa jeki.

The ball is in JK's court.

Wazo zuri sana hili, Lakini itakuwa vigumu sana kwa Kikwete kufanya haya. Miaka minne iliyopita imeonyesha kwa kiwango kikubwa utendaji kazi wa JK.
 
Recta,
Mkuu Mkandara, heshima kwako. Mkuu, kinachosumbua sio chaguo la kimaoni linalotolewa na "VIONGOZI" wanaojitokeza na kupendekeza kwa kusema hadharani kuwa Kikwete atagombea kuwa Rais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa 2010. SIo hilo hata kidogo. Tatizo ni pale wanapokwenda mbele zaidi na kutishia kuwa asijitokeze mwingine wa kumpinga JK katika uchaguzi huo. Mkuu hilo ndilo tatizo.

Kauli ya kupendekeza ni maoni halali kabisa. Kauli za kuhitimisha hoja ambayo mtu hana mamlaka ya kuhitimisha ni kosa. VIONGOZI hao waliojitokeza kusema hadharani kuwa hakuna anaetakiwa kumpinga JK 2010 kwa kuzingatia utamaduni uliopo ndani ya chama wanakosea wanapofanya hivyo. Wanakosea kwasababu tu, wanataka wengine wasio na nguvu kama walizonazo wao waogope kupingana na maamuzi yao (si maoni yao). Maamuzi ya kuwa JK ndie atakaegombea peke yake.
Mkuu wangu hapo nilipoweka bold kwa rangi nyekundu ndipo napozungumzia mimi..Nasema hakuna kosa kabisa..sino kosa kwa sababu watu hawa - HAWANA MAMLAKA YA KUHITIMISHA..hivyo kilichosemwa bado ni Mapendekezo nitahofia tu mtu mwenye mamlaka..

Siku zote sisi wananchi tutaogopa mtu mwenye Mamlaka ya kuhitimisha anapotunga sheria ama kupitisha Utaratibu kwa wananchi wote lakini kusema tu wanasema wengi na ndizo siasa zetu..
CCM imejengwa ndani ya Ujamaa wa Kiafrika na chama hicho kina mambo mengi sana yanayoendeshwa kwa Udikteta kutokana na urithi wa nyayo za mwalimu zinazosisitiza heshima ni pamoja na kuogopa wakubwa zako..hivyo mabadiliko yoyote ndani ya chama yanatakiwa kwenda kwa hatua..Binafsi sioni kosa kabisa ktk kumpendekeza Kikwete na hata mikwara inayotolewa ikiwa kuna usiri fulani pembeni kumwangusha Kikwete ktk uchaguzi wa ndani CCM..Ni mbinu za kisiasa ktk mfumo wa Kijamaa kuwekeana mikwara..
Kwa nini wanaompinga Kikwete wasijitokeze hadharani? kwa nini wamejichimbia wakiendesha kampeni zao kichini chini wakati sisi wananchi tunataka sana kuona Upinzani kwa Kikwete ukiwa wazi nhasa ktk maswala ambayo sisi tunapenda kuona mabadiliko!.

Mkuu wangu Lisemwalo Lipo na kama halipo linakuja.. hawa wazee sio tu wameibuka toka usingizini wakaanza kusema hayo bila kuwepo dalili za vurugu ndani ya chama..
Nina hakika wazee hawa wasingefikia maneno haya kama Mwandosya, Lowassa au Asha Rose Migiro wangesimama na kusema wanatarajia kugombea kiti cha urais dhidi ya Kikwete.. hapo tungeona fair game, lakini yamepita majungu tu nyuma nyuma kiasi kwamba hata mimi hapa Mkandara naaza kuzipata data za Mapinduzi haya baridi..

Kumbukeni Mwanakijiji, FMES na wengine wengi tu wamekuwa wakitutaarifu kuhusu vikao na mikutano ya siri kumwondoa Kikwete au kuchukua majimbo fulani ya utawala kama vile utawala wa nchi hii umekuwa mnadani..Hii mikutano ilianza lini kama mnakumbuka na leo tunaanza kuona dalili zake bado tunashindwa kuamini kinachoendelea... hali ambayo sii mbaya tu kwa Kikwete isipokuwa inahatarisha Usalama wa nchi yetu..
Upinzani wa Kikwete na vyama vya Upinzani unaeleweka na ni wazi lakini Upinzani ulipo ndani ya CCM unatisha, ni kinyume cha katiba na wala na sitaomba hata siku moja mgombea wa CCM atokane na ushirika wa Mafisadi..

My biggest lesson ni uchaguzi wa Kikwete mwenyewe mwaka 2005. Nimeona jinsi Mafisadi wanavyoweza kuibomoa nchi..Mkapa alikuwa fundisho la jinsi kiongozi mmoja arrogant anavyoweza kuifilisi nchi, mafunzo yote haya mawili yananisukuma mimi kuepukana na matukio yenye harufu ya Ufisadi au Arrogant!..na sintapenda wananchi warudie makosa yale..

I still believe Kikwete kisha jikata na Mafisadi..na kweli kuna mbinu kubwa zinafanyika kumwondoa madarakani kwa sababu ambazo ni nje kabisa ya uwezo wake kutawala. Sababu ambazo hazifanani na malalamishi ya wananchi, hivyo upinzani wa aina hiyo nipo radhi kabisa ukiwekewa mikwara unless wajitokeze na kupiga kampeni wazi bila kutumia fedha na umaarufu wao kuwahadaa wananchi ambao asilimia 80 ni maskini..Firaun ni lazima atakamata wengi!
 
a. Kuna watu ambao kwa Kikwete kuendelea kutawala wananufaika aidha personally or professionaly au kisiasa. Hivyo, endapo Kikwete hatamaliza sasa kipindi hicho kingine akaja mtu mwingine na kuunda utawala mpya kuna watu wengi ambao sitoshangaa watabwaga nje ya utawala. Hili wanaliogopa.

b. Kuna watu ambao wanaamini asipopata nafasi ya kuendelea na miaka mitano mingine zile ahadi alizotoa 2005 hazitatimilika. Msingi wa Kikwete kugombea kama mtakavyosikia muda si mrefu ni ili akamilishe ahadi zile nyingine zote kwani miaka "mitano ya kwanza ni kutengeneza mazingira na ile mitano ya mwisho ni kufanya kazi". Hivyo, watatuambia haitakuwa fair kutarajia mtu atimize mambo yale yote ndani ya miaka 5 hivyo tumpe nafasi ya kuyamaliza kwa miaka mingine 5. Tatizo hawatatukumbusha kuwa walipoomba kura 2005 waliomba kwa miaka mitano tu! Hawajatimiza yale basi mtu yeyote ndani ya CCM na nje anaweza kuja na kusema mmeshindwa. Hili wanaliogopa.

c. Endapo Kikwete hatopewa ngwe ya pili ya utawala na hivyo kulazimisha kuwa nje baada ya muhula huu mmoja yale yanayomtokea Mkapa ndiyo yatakayomtokea yeye. Kikwete anahusika na mikataba mibovu kabisa katika nchi hii, udumazaji wa utawala wa sheria na uchaguzi mbovu wa viongozi watendaji. Kibano anachopewa Mkapa leo hii ndicho kitakachotumiwa kwa Kikwete. Hili hawawezi kuliruhusu. Na hili wanaliogopa.
 
a. Kuna watu ambao kwa Kikwete kuendelea kutawala wananufaika aidha personally or professionaly au kisiasa. Hivyo, endapo Kikwete hatamaliza sasa kipindi hicho kingine akaja mtu mwingine na kuunda utawala mpya kuna watu wengi ambao sitoshangaa watabwaga nje ya utawala. Hili wanaliogopa.

b. Kuna watu ambao wanaamini asipopata nafasi ya kuendelea na miaka mitano mingine zile ahadi alizotoa 2005 hazitatimilika. Msingi wa Kikwete kugombea kama mtakavyosikia muda si mrefu ni ili akamilishe ahadi zile nyingine zote kwani miaka "mitano ya kwanza ni kutengeneza mazingira na ile mitano ya mwisho ni kufanya kazi". Hivyo, watatuambia haitakuwa fair kutarajia mtu atimize mambo yale yote ndani ya miaka 5 hivyo tumpe nafasi ya kuyamaliza kwa miaka mingine 5. Tatizo hawatatukumbusha kuwa walipoomba kura 2005 waliomba kwa miaka mitano tu! Hawajatimiza yale basi mtu yeyote ndani ya CCM na nje anaweza kuja na kusema mmeshindwa. Hili wanaliogopa.

c. Endapo Kikwete hatopewa ngwe ya pili ya utawala na hivyo kulazimisha kuwa nje baada ya muhula huu mmoja yale yanayomtokea Mkapa ndiyo yatakayomtokea yeye. Kikwete anahusika na mikataba mibovu kabisa katika nchi hii, udumazaji wa utawala wa sheria na uchaguzi mbovu wa viongozi watendaji. Kibano anachopewa Mkapa leo hii ndicho kitakachotumiwa kwa Kikwete. Hili hawawezi kuliruhusu. Na hili wanaliogopa.

Kwahiyo kwa maslahi ya chama, watu binafsi na nafsi yake, kikwete anakila sababu ya kugombea. Na kwasababu ulizozitoa inaonekana ni lazima agombea, na atapitishwa na chama chake. kama ndivyo, lazima upinzania wafikirie mgombea wa ukweli.
 
Mtu yeyeto atakayejitokeza kukabiliana na Kikwete anajitafutia asilolijua, wakubwa wanaonekana kumnyeta Kikwete, CCM wana aina ya udikteta wanaouita "demokrasia ya kuwa muungwana" hii alifanyiwa Bilali, alipolazimishwa aliondowe jina lake na kumwachia A.Karume eti "amalize" n'ngwe ya pili utafikiri urais ni mali ya CCM.
 
Mimi nawaambia, mkitaka kujua mvurugano uliopo CCM leo hii, Kikwete atangaze kuwa hatogombea kutokana na sababu mbalimbali kuwa karibu na familia yake na kuwa nia yake ya kuwa Rais imeshatimia. Kitakachofuata hapo kinaweza kuitwa "kizaazaa"...
 
Inawezekana kabisa kikwete atagombea pia kutokana na ukweli kwamba anaamini hakuna mgombea kutoka upinzania ambaye anaweza kumsumbua! Hivi ni kweli wapinzani hawawezi kupata mgombea ambaye atakamata roho za wananchi!
 
Inawezekana kabisa kikwete atagombea pia kutokana na ukweli kwamba anaamini hakuna mgombea kutoka upinzania ambaye anaweza kumsumbua! Hivi ni kweli wapinzani hawawezi kupata mgombea ambaye atakamata roho za wananchi!

Unajua nini... wapinzani hawauhitaji Urais. Wala wasipoteze nguvu zao huko. Kikwete kama unavyosema hatishwi na wapinzani bali na CCM.
 
Unajua nini... wapinzani hawauhitaji Urais. Wala wasipoteze nguvu zao huko. Kikwete kama unavyosema hatishwi na wapinzani bali na CCM.

Kaka swala hapa sio kwamba wapinzani hawauhitaji urahisi, uhalisi ni kwamba hawakotayari kupata uraisi sasa. Kwa manufaa ya kukuza demokrasia upinzani ijitayarishe kupata wabunge wa kutosha uchaguzi huu.

Lakini kusimamisha mgombea wa uraisi atayefaa ni jambo la msingi sana katika upinzani kukuza uwepo wao katika siasa. Pili, wanakuza taratibu za kumpat mgombea, na la msingi ni vyema CCM itambua kwamba kunawatu nje ya CCM wanaoweza kuongoza hii nchi.
 
pia wapinzani wakipata the right candidate and strategist believe me ' they can take this country'. The question is are they ready to rule! I can see it coming brother very soon more that we can predict
 
Mimi nawaambia, mkitaka kujua mvurugano uliopo CCM leo hii, Kikwete atangaze kuwa hatogombea kutokana na sababu mbalimbali kuwa karibu na familia yake na kuwa nia yake ya kuwa Rais imeshatimia. Kitakachofuata hapo kinaweza kuitwa "kizaazaa"...

Mkuu Mwanakijiji,

Ukweli ni kuwa Kikwete atagombea tu na atajitahidi kumng'oa meno yeyote atakayekisogelea hicho kiti chake na inaelekea kuna tishio analoliona ndani ya CCM.

JK ni mpenda makuu na mpenda kujirusha-rusha, vitu ambavyo havipo nje ya u-mungu-mtu wa uraisi, unless akiondoka kwenye hicho kiti awe ameshajikusanyia mamilioni ya $$$ kuliko akina EL na RA kitu ambacho sidhani kama ameshakamilisha.

Kibaya zaidi ni kuwa, sidhani kama anatambua kuwa;
  1. Hana vision ya kuiendeleza nchi
  2. Hana uwezo wa kuongoza. Kuongoza sio kunena tu na kutegemea kuwa yatatokea, kama anavyofanya JK. Uongozi ni kuweka mikakati, kufuatilia utendaji na matokeo yake. Kwa mfano suala la bandari ya Dar ambayo inaendelea kudorora na yeye JK anaendelea kutoa matamko.
  3. Kuombaomba kwa wahisani ni aibu kwake na kwa taifa na sio mtaji wa maendeleo.Kwa mfano sijui kwa nini uwanja mpya wa taifa uitwe wa taifa ingawa umejengwa kwa jasho la waChina ingawa pesa ya kuujenga mara 5 zaidi tulikuwa nao na tukazitupa kwenye twin towers za BOT.
  4. Kikwete haongozi kwenye vita ya rushwa na ufisadi, au utawala wa sheria na haki bali ni kizuizi.

Kazi ni kwa waTZ wote, CCM na Upinzani, kuamua kujikomboa au kujinyonga. Muhimu ni kutambua kuwa JK ni kikwazo kwa maendeleo na kichocheo cha rushwa.
 
Kinachonishangaza ni kuwa hawa ndugu zetu wanaonekana wanatambua kitu ambacho wengine hatukitambui; yaani, ndani ya CCM kuna mtu zaidi ya Kikwete ambaye anatamani kugombea Urais mwakani. Mtu huyo nina uhakika si Shibuda kwani Shibuda alifanya hivyo hata mwaka 2005 na sidhani kama anawatisha hivyo. Kitendo cha mtu aliyekuwa Waziri Mkuu, kitendo cha mtu aliyewahi kuwa Spika na jumuiya mbalimbali za CCM mikoani kuanza kujitokeza na kusema Kikwete ndiye atakuwa mgombea wao kunatudokeza jambo moja kuwa kuna mtu mwingine ndani ya CCM anataka kuwania nafasi hiyo ya Urais.

A very good observation.
 
Kikwete sasa anarekodi!
Mwaka 2005 Kikwete hakuwa na rekodi ya kuonesha uongozi wake na kama ingekuwa katika nchi nyingine kuna mambo ambayo angetakiwa kutolea maelezo ndio maana walimkwepesha kufanya midahalo na wagombea wengine ili watu wampime. Kulikuwa na masuala ya IPTL na tuhuma za kupokea fedha toka Iran na Oman. Bahati mbaya waandishi na wana CCM wengi walikuwa wamepigwa ganzi ya mapenzi kiasi kwamba hakuna aliyethubutu kumhoji maswali magumu na hivyo tukampitisha kwa kufaraha kwa kuangalia vile ambavyo si vya msingi.

Mkuu hapa nitatofautiana na wewe kidogo. Kikwete wa 2005 alikuwa na rekodi tena mbaya sana lakini ilinyamazishwa na Mkapa, tumesahau IPTL?.

Mkapa alikuwa radhi kuvua watu uraia ili tu wafunge midomo yao na ndio maana JK akishirikiana na wanamtandao waliweza kuiteka nyara nchi na kuficha madudu yao. Imagine hata Lowassa alikubalika kuwa PM.

Rekodi ya utendaji wa Kikwete haijawahi kuwa nzuri hata siku moja na alipokuwa Foreign Affairs, mabalozi wengi walikuwa wanalalamika wazi kuwa JK ni mzembe. Hii ilimfanya katibu mkuu wa zamani wa utumishi, Rugumyamheto, ambaye ni mmoja kati ya watu JK aliowaondoa mara tu alipoingia madarakani, kumshauri raisi Mkapa kumuondoa FA, kitu ambacho JK aligoma na Mkapa kufyata.
 
mimi mgeni ivi CCM hawana midahalo wakati wa kumchagua mgombea wao urais
Nashangaa mkulu ameshindwa kusimama kwenye mdahalo na LIPUMBA, FREEMAN, MREMA , MVUNGI, SENKORO na wengineyo

Nina uhakika kama angekuwa amefanya midahalo yasingemkuta yale yaliyo mkuta BOT towers

kama wapinzani wanajiamini kushinda yeye ni wakati wa waTZ kuangalia upinzani
mtu ambae hajiamini hata kazi yake pia haiaminiki
 
mimi mgeni ivi CCM hawana midahalo wakati wa kumchagua mgombea wao urais
Nashangaa mkulu ameshindwa kusimama kwenye mdahalo na LIPUMBA, FREEMAN, MREMA , MVUNGI, SENKORO na wengineyo

Nina uhakika kama angekuwa amefanya midahalo yasingemkuta yale yaliyo mkuta BOT towers

kama wapinzani wanajiamini kushinda yeye ni wakati wa waTZ kuangalia upinzani
mtu ambae hajiamini hata kazi yake pia haiaminiki

...Unamaanisha pale alipo ongea kwa kutojiamini baada ya maswali ya Aisha wa CNN, au?
 
Wanaotaka kugombea wasitishwe

Hata hivyo ndani ya CCM kama kuna watu wanaamini wanaweza kuliongoza Taifa letu vizuri zaidi, kwa kuthubutu zaidi na kuliamsha kuelekea mafanikio na maendeleo ya kweli (ya watu siyo vitu) basi watu hawa wako huru kujitokeza bila kuona haya kama alivyofanya Shibuda. Watetezi wake (Kikwete) hawana uhodhi wa CCM na wasitumie jina la CCM kuwatisha watu wengine ambao wako ndani ya Chama hicho.

Mtanzania yoyote ndani ya CCM anayetaka kugombea nafasi ya Urais ni lazima apewe nafasi sawa.


Good call Mwanakijiji. Kama kuna tunaowaona wanafaa tuweke namba zao za simu hapa JF ili tuwapigie kuwapa moyo na kuwahimiza wagombee.

Let a grassroot movement against Kikwete-2010 begin from JF and spread. We are the people the country has been waiting for (Obama).
 
...Unamaanisha pale alipo ongea kwa kutojiamini baada ya maswali ya Aisha wa CNN, au?

ndio na yeye ni mchumi
sio hapo tu mara nyingi akiulizwa swali anababaisha..
au kama kuna matatizo anakaaa kimya, hawezi ku lead, mpaka matatizo ya poe yeye ndio ana ibuka..
 
Mkuu unajua wengi wetu woga we unafikili kuna watu hawataki kuchukua fomu?Wanapenda sana lakini wanaogopa sana kusutwa au kutengwa....[/QUOTE]

- Sasa kilichobaki ni kuanzisha chama chetu cha siasa, cha JF na kusimama wenyewe ili 2015 tufanye kweli, unaiudhi na inasikitisha sana!

FMES!
[/SIZE]
Interesting!!
Mkuu,there has been over the last few years a telling growth in the level of people with ideas, international exposure, business experience and entrepreneurial instinct, you can clearly tell that by the value of their writting here in JF and i think this was a missing ingredient if you look back about 20-30 years in history in Tanzania.
People on the ground have now developed that ambition to question,ile nidhamu ya woga(ujinga) kwa baadhi ya watu sasa haipo tena! a typical example is the Mzee Mwanakijiji(cheche) .Hivyo basi naelekea kufikiri JF ibakiye tu kuwa Chachu/ gurudumu la mabadiliko,mahala pa kuchota na kutuama hekima/mawazo.Cha ajabu Ukayachukua mawazo hayoX2 na kupanda nayo jukwaani yataitwa 'mabomu' ila hapa JF yanatambulikana na kusomwa kama 'data'.
**Just my humble opinion mkuu.
 
Interesting!!
Mkuu,there has been over the last few years a telling growth in the level of people with ideas, international exposure, business experience and entrepreneurial instinct, you can clearly tell that by the value of their writting here in JF and i think this was a missing ingredient if you look back about 20-30 years in history in Tanzania.
People on the ground have now developed that ambition to question,ile nidhamu ya woga(ujinga) kwa baadhi ya watu sasa haipo tena! a typical example is the Mzee Mwanakijiji(cheche) .Hivyo basi naelekea kufikiri JF ibakiye tu kuwa Chachu/ gurudumu la mabadiliko,mahala pa kuchota na kutuama hekima/mawazo.Cha ajabu Ukayachukua mawazo hayoX2 na kupanda nayo jukwaani yataitwa 'mabomu' ila hapa JF yanatambulikana na kusomwa kama 'data'.
**Just my humble opinion mkuu.

Yawezekana watu wamefunguka macho kwa kiasi kikubwa kabisa, lakini siasa zinauwanja wake. Ushiriki wa moja kwa moja ndio njia moja wapo ya kuleta mabadiliko, hapo wengi ndipo tunashidwa. Lakini kunaulazima watu wawesosholized ndani ya vyama vya siasa maana hadithi ya wagombea binafsi iko mbali.
 
Unajua nini... wapinzani hawauhitaji Urais. Wala wasipoteze nguvu zao huko. Kikwete kama unavyosema hatishwi na wapinzani bali na CCM.
.
Hapana mkuu wangu Wapinzani wanauhitaji sana Urais kwa sababu Urais ndio kila kitu. Kwa nini tunamlaumu Kikwete na sio chama wala watu wengine!..
Kikwete asema hatishwi na mtu isipokuwa CCM, hayo ni maneno ya kawaida kabisa kwani usipopita CCM hawezi kuwa rais..period. Ni hofu ambayo kila mgombea anayo kutokana na mfumo wa uchaguzi..
pia wapinzani wakipata the right candidate and strategist believe me ' they can take this country'. The question is are they ready to rule! I can see it coming brother very soon more that we can predict
Hapa Petu, Hata mimi naanza kujenga matumaini haya kwa sababu kuna kila sababu za Upinzani kuibuka washindi mwaka 2010. Mazingara ya uchaguzi ujao ni mazuri kuliko yale ya Mrema mwaka 1995.
Leo hii hakuna mtu kama Nyerere ambaye anaweza kumnadi mgombea na akauzika. Inawezekana kabisa!
 
Back
Top Bottom