Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,985
- 2,770
NIDA pamoja na NIA yenu nzuri ya kuwapatia WaTZ vitambulisho naona hili zoezi la uandikishaji linawakera watu kwa kuwa wanapanga foleni ndefu tena juani kila siku wakikimbizana na deadline. zile fomu hazina ugumu wa Kivile wa kutoweza kujazwa na ofisa anayejua kuandika vizuri na siyo mwandiko wa kuku hata kama hakupata semina yenu. Ili kuondoa foleni na malalamiko wapeni Watendaji wa mtaa ruhusa ya kurecruit watu wenye uwezo wa kuandika vizuri kwa hizi siku zilizobaki. Ni bora hata mkatafuta shule ya Msingi au sekondari penye nafasi na meza ili muweze kumaliza zoezi hili kwa ufanisi.Mkijidai kazi mnaweza ninyi tu mtawafanya watu wengi wasijisajili. Kila ofisi ya serikali za mitaa ni foleni ndefu na malalamiko kibao. Mkija mara mnakuja na ofisa mmoja au wawili ambao hawakidhi haja. Toeni nafasi kama N B S walivyofanya kama mna nia kweli ya kuwapa WaTz Vitambulisho.