Ni waongo wanaodai kuwa Katiba ilipitishwa kiujanja, hii ni katiba bora East Africa- Prof Mahalu

Aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya kupitia kanuni za kuendesha bunge maalum, anasema hayo??? Sina comment.
 
Ingekuwa vizuri kwa wale wanaosema katiba ni mbovu wa-identify kifungi kipi ni kibovu kuliko kutoa blanket denial.
Nitakwambia kile ninachokifahamu kwa maarifa yangu madogo tu niliyo nayo.
Kifungu cha UWAZI kimefutwa,Kwanini?CCM wanasema siyo muhimu sana kiwemo Kwenye katiba.Ukweli ni kwamba,kifungu cha UWAZI kikiwemo Kwenye katiba kitahesabika kama one of the fundamental laws that will be guiding our daily social, economic and political activities in our country. Sheria nyingine nyingi ndogo zitasimamiwa na hiki kifungu.Hiki kifungu kingekuwa ndiyo sheria mama of course. Ubaya wa hiki kifungu,kingekuwa kama ngao kwa wahandishi wa habari za uchunguzi wajapo na habari za ndani juu ya matendo yasiyo ya kimaadili yafanywayo na viongozi wa serikali na hata baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola nchini.Ukiwapeleka mahakamani waandishi wa habari waandikao habari za kiuchunguzi kwa hoja kwamba wanaandika habari za uchochezi,mahama itakuambia kwamba wahandishi hawajafanya kosa lolote isipokuwa wametimiza haki yao ya kikatiba,kuisaidia serikali katika kufanya mamba yake kwa uwazi.
 
Nimekuelewa Prof. Mahalu. Ubora wa katiba anauweka katika uhalali wa "process" badala ya "content". Nimesikia watetezi wa katiba iliyopendekezwa wakijikita zaidi kuwa imejumuisha makundi ya kijamii kama wakulima, wavuvi, wafugaji nk. Kwa neutrals tungependa kujua mambo makubwa zaidi kama madaraka ya rais, mifumo ya kiongozi, mfumo wa kiuchumi, elimu nk. Je tukipimwa kwa mizani hiyo bado tutaaambiwa katiba hii ni bora kuliko ya nchi kama Kenya na Rwanda? Au ni bora kuliko iliyopo? Je lengo ni kuwa na katiba iliyo bora kuliko iliyopo? Strategic thinking inatutaka angalau tulenge miaka 50 ijayo!
 
Hii mbona ipo wazi sana hii ni katiba bora kabisa sote tunajua hivyo

mkuu inawea kuwa ni katiba bora lakini bila ushilikiswaji wa watanzania wote inakuwa si bora tena, katiba iliyotengenezwa na chama kimoja tu ccm inapoteza ubora wake.
 
Eti ni KATIBA BORA AFRIKA, bila kutaja kwanini ni katiba bora kuliko katiba kama za Kenya, S. Africa, Ghana, Zimbabwe etc. Kusema tu ni KATIBA BORA, hakuifanyi kuwa bora.

Anasema kwamba katiba haikupitishwa kijanja janja bila kuelezea ni kwanini
  1. Kura ya Zakhia Meghji mjumbe kutoka Tanganyika ilihesabiwa Zanzibar?
  2. Kura ya Ambar Hamis mjumbe kutoka CUF/UKAWA ambaye hakupiga kabisa kura kwanini kura yake ilihesabiwa Zanzibar?
  3. Anna Komu Mjumbe kutoka Zanzibar kura yake ilihesabiwa Tanganyika?
  4. Shida Salum (marehemu) kwanini alionekana kupiga kura kutokea kaburini?
  5. Idadi wa wajumbe wa BMK kutoka ZNZ kwenye sheria ya mabadiliko ya katiba ni 210. Idadi wa wajumbe wa BMK wa ZNZ iliyotangazwa na Sitta ni 219?
  6. Mwakilishi wa Balozi wa Saudia alisema kwamba kutokana na mazingira ya Hijja ni vigumu wajumbe wa BMK walioko Macca kupiga kura, Je wajumbe hao wa BMK ambao inasemekana walipiga kura walisimamiwa wa nani kama kanuni inavyoelekeza?
  7. Mjumbe wa BMK Max aliyeoko Appolo india ICU ambaye hawezi kuzungumza wala kula chakula mwenyewe, aliwezaje kupiga kura katika u-mahututi wake?

Huo ndio UJANJA-UJANJA tunaoongelea Watanzania, Huyu Prof (SIC) Mahalu asizike kichwa mchangani ilihali kiwiliwili chote na masa.buri yake yakiwa nje. Ni bora anyamaze tu kuliko kijidhalilisha.

I rest my case
 
Wewe unautajili gani wakati hata chai mpaka kwa mama yako halafu unajifanya unapesa,Nimesema mtu anayepinga katiba hii ni chizi.

Chizi Ni Wewe Na Magamba wenzio mliochakachua maoni ya watz! Tulieni dawa iwangie taratibu,acheni kupiga mayowe!
 
Wewe unautajili gani wakati hata chai mpaka kwa mama yako halafu unajifanya unapesa,Nimesema mtu anayepinga katiba hii ni chizi.
Bahati nzuri kila mtu hapa jamvini anafahamu kuwa wewe ni mwendawazimu na kila ukisemacho hakiaminiki!
 


Ni Katiba bora Afrika Mashariki

Profesa Mahalu anawanyooshea vidole wale wanaodai kuwa Katiba ilipitishwa kiujanja ujanja na kuwa hata uandishi wake haukuwa bora, akisema kuwa huo ni wongo.

“Ni waongo wanaodai kuwa Katiba ilipitishwa kiujanja, nilikuwa pale, tulikuwa na wasomi waliobobea katika uandishi na sheria, hakuna mahali ambapo palipindishwa au kipengele kilichobadilishwa kiujanja. Hatukubadili chochote,” anasema.


Anasema Katiba hiyo iliyopitishwa ni bora na yenye viwango ambavyo hata
majirani zetu Kenya, Uganda na Rwanda, wanaitamani.

“Tumeitengeneza katika viwago ili kila kitu kiende sawa, bila hivyo tusingeweza kufanya lolote. Tumefanya kazi kubwa kuunda Katiba pendekezwa na watanzania hawana budi kujivunia hilo,” anasema.

Chanzo: Mwananchi


Asante Prof. Kwa hali hii si ajabu hata MAJI MAREFU kujiita Prof.
 
Wewe unautajili gani wakati hata chai mpaka kwa mama yako halafu unajifanya unapesa,Nimesema mtu anayepinga katiba hii ni chizi.
wewe ndio chizi kabisa unayeshabikia katiba iliyopigiwa kura na marehemu..hv nyie mnaojiita wasomi usomi wenu unalisaidia nini taifa hili? Ikiwa mnashabikia katiba haramu kama hii? ukiendekeza njaa unaweza kuuza utu wako..hv mnafikiri kwa kichwa au M-A K-A..L.£-¤?
 
Mabaradhuli wa sheria hawa.ivi wazanzibari maoni yao na usalama wa utaifa wao Umezingatiwa humu? Mumesahau kuwa hii ilitakiwa iwe katiba ya muungano,yenye kuzingatia maslahi ya pande Zote za muungano
. Katiba ilitakiwa iwe na maridhiano ya kitaifa,siyo magamba pekeyao.Hizi fani za uprofesa sikuhizi mekumvwa na ebola .Prf. anadai katiba nzuri ila siasa ndiyo imeingilia kati. Sasa atuambie ikiwa ukawa wametoka ili kuepusha hilo ,wale waliobaki si ndio wametunga katiba kisiasa? Akiwemo na yeye Prf.Mahalu?
Katiba ya ccm utaiitaje nzuri? Wakati inalaaniwa na kupingwa kila kona?
 
Hii mbona ipo wazi sana hii ni katiba bora kabisa sote tunajua hivyo

Je, mikataba mikubwa ya uwekezaji katika rasilimali za nchi itapelekwa Bungeni kujadiliwa?
Je Katiba inasemaje kuhusu uhuru wa kutoa maoni na kukusanyika?
Je inakataza kiongozi wa serikali asiwe na akaunti nje ya nchi?

Mafisadi wanaposema KATIBA HII NI NZURI, wana maanisha "NI NZURI KWA WAO MAFISADI" siyo kwa walalahoi wananchi. Sasa hivi watapata uhuru mzuri wa kujitanua na kuiba watakacho na kwenda kuweka nje bila kubughudhiwa. Wenye akili tumeliona hili.
 
Jamani mumsamehe huyu kawa blackmailed huyu . Kwani mmesahau issue yake ya ufisadi wa kuuza nyumba ya ubalozi ilivyotawala vichwa vya habari miaka na michezi michache iliyopita na serikali ilivyokuwa imemshikia bodi? Baadae ilibidi akalambe miguu ya mkapa akaja kutestify kumtetea maana alikuwa anakwenda na maji. wakati muafaka ulipofika ikawa rahisi sana kumtumia huyu fallen hero kuhalalisha uchafu wa katiba maana they had him 'by the balls' hana jinsi la sivyo 'ushahidi mpya' wa kesi yake ungejitokeza na angefungwa tu! Hawa ni watu japo wanatia kichefuchefu mimi huwa nawahurumia maana hawajui watendalo na madhara yake kwa nchi. Wanawazia kuokoa nafsi zao tu no matter what. hawa ndio maprofessor wetu...Mahalu....Shivji....Benson Bana......ni majanga tu!
 
mfumo wa upigaji kura tu , unaonyesha jinsi hiyo katiba ilivyo bora kuliko zooote ulimwenguni, sawa profesa.
Wakati baadhi ya watu wakiendelea kuamini kuwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Samuel Sitta alichakachua kanuni ili apitishe Katiba, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kupitia Kanuni hizo za kuendeshea Bunge hilo, Profesa Costa Ricky Mahalu amemtetea akisema ‘Bunge halikukosea kurekebisha kanuni hizo.’

Profesa Mahalu ambaye ni Mhadhiri wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine, Bunge la Katiba liliendelea kubadili baadhi ya kanuni zilitungwa ili kufikia malengo ya kupata Katiba nzuri

Profesa Mahalu anawasihi watanzania na wanasiasa kutomhukumu Sitta kwa madai kuwa alikuwa akichakachua kanuni hizo kwa maslahi binafsi. Alisema kamati yake kuidhinisha kanuni zilizofaa kuendesha Bunge la Katiba, bado kulikuwa na fursa ya kuendelea kuzifanyia mabadiliko kanuni hizo kadiri ya mahitaji.

“Sitta hana uwezo wa kufanya marekebisho kwa maslahi binafsi au ya chama, tatizo ni kuwa hili jambo limeingiliwa na siasa kidogo, mchakato mzima ulifanya kazi kama timu,” anasema

Anasema marekebisho yeyote ya kanuni yanapoibuliwa na mjumbe, hupelekwa kwenye kamati ya uongozi, kisha kwenye Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge na Spika Sitta huwauliza wajumbe iwapo wanaafiki au la.

“Sitta huuliza tu iwapo marekebisho yanaafikiwa au la. Lakini masuala ya kisiasa yanamhukumu jambo ambalo si kweli, mimi nilikuwa mwenyekiti najua hakuna chochote.” anasema

Profesa Mahalu anaendelea kueleza “Marekebisho ni muhimu kwa kuwa sheria mbaya inakwamisha vitu, iwapo mambo hayaendi inavyotakiwa kutokana na baadhi ya kanuni, hatuna budi kuzifanyia marekebisho kwa sababu nia yetu ni kupata katiba bora,” anasema Profesa Mahalu.

Anasema kuwa katika kipindi chote cha uendeshaji wa bunge hilo hakuna kanuni iliyoharibiwa na kama jambo hilo lingetokea basi angelipinga kwa nguvu zote.

Pamoja na hayo Profesa Mahalu anasema kuwa, Bunge hilo lilifanya kazi katika mfumo uliokubaliwa wa kanuni kuanzia uteuzi wa wajumbe hadi pale Rais alipokabidhiwa Katiba pendekezwa.

“Uteuzi wa viongozi ulikuwa mzuri, sheria namba 83 ilitumika ipasavyo na kila kitu kilienda sawa,” anasema

Mwanasheria huyo ambaye pia alikuwa katika kamati ya uandishi anasema, watanzania hawana budi kufurahia katiba hiyo pendekezwa kwa sababu imefanyiwa kazi na jopo la wasomi na wazalendo wa nchi hii.

“Tulifanya kazi sana, hatuwezi kusema kuwa tutafanya vitu vyote kila mwananchi anavyovitaka lakini misingi muhimu tumeiweka katika katiba hiyo, kwa mfano, misingi ya uchumi, utamaduni na haki,” anasema


Anasema katiba hiyo imemlenga Mtanzania wa kawaida ambaye hapo zamani alikosa haki zake za msingi na hakujua wapi pa kupeleka kilio hicho, lakini sasa Katiba inamtambua.

Anatolea mfano wa makundi ambayo yalisahaulika kaw muda mrefu kuwa ni pamoja na wakulima, wafugaji na wavuvi ambao hivi sasa Katiba inawatambua.

“Asilimia kubwa ya Watanzania ni wakulima na wafugaji, katika Katiba hii haki zao zimeainishwa. Kila mmoja amepata haki ya kufuga, kuwinda, kumiliki ardhi na kulima. Hili halikuwepo hapo zamani kwani sasa hivi hata wachimbaji wadogo nao wamepewa umuhimu,” anasema.

Profesa Mahalu anayataja mambo matatu makubwa ambayo yameainishwa na kuchambuliwa katika Katiba mpya kuwa ni ushirikishwaji wa Tanzania bara na Zanzibar. Anasema masuala ya Muungano katika Katiba hii yatasaidia kuondoa kero zilizopo na kuleta suluhu.

Jambo jingine kubwa ambalo Profesa Mahalu amesema Katiba imeyafanyia kazi ni ushirikishwaji wa vijana katika siasa kwa kiasi kikubwa hadi kutambuliwa kwa Baraza la Vijana la Taifa.

“Unajua vijana ndiyo taifa la kesho, na ni asilimia kubwa ya Watanzania...hivyo katika Katiba tumeweka haki nyingi za vijana na ndiyo maana likaundwa Baraza la Vijana wenye umri wa kuanzia miaka 18 hadi 35 ambao watatakiwa kushiriki kikamilifu katika siasa,” anasema.

Kingine ni ushirikishwaji wa wanawake kwa asilimia 50 jambo ambalo anasema kuwa litawanyanyua wanawake hao katika kushika nafasi za uongozi. Profesa Mahalu anasema kuwa wanawake sasa hawatanyanyasika katika masuala ya ardhi na watatambulika kisheria katika masuala ya mirathi.

“Kilichobaki ni wanawake wenyewe kutambua haki zao na kuzidai kwa sababu tayari Katiba imeshaweka masuala hayo ndani yake.” anasema

Sambamba na hilo masuala ya haki za makundi ya wafugaji, walemavu, wakulima na wachimbaji wadogo kuwekwa katika Katiba ni jambo ambalo anasema limeifanya Katiba hiyo imguse mwananchi katika kiwango cha chini kinachowakilisha jamii kubwa ya Watanzania.

Ni Katiba bora Afrika Mashariki

Profesa Mahalu anawanyooshea vidole wale wanaodai kuwa Katiba ilipitishwa kiujanja ujanja na kuwa hata uandishi wake haukuwa bora, akisema kuwa huo ni wongo.

“Ni waongo wanaodai kuwa Katiba ilipitishwa kiujanja, nilikuwa pale, tulikuwa na wasomi waliobobea katika uandishi na sheria, hakuna mahali ambapo palipindishwa au kipengele kilichobadilishwa kiujanja. Hatukubadili chochote,” anasema.


Anasema Katiba hiyo iliyopitishwa ni bora na yenye viwango ambavyo hata majirani zetu Kenya, Uganda na Rwanda, wanaitamani.

“Tumeitengeneza katika viwago ili kila kitu kiende sawa, bila hivyo tusingeweza kufanya lolote. Tumefanya kazi kubwa kuunda Katiba pendekezwa na watanzania hawana budi kujivunia hilo,” anasema.

Ukawa na Bunge la Katiba

Profesa Mahalu anaeleza kuwa kitendo cha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia Bunge la Katiba ni kutumia uhuru wao kama wanasiasa.

“Siwezi kuwahukumu au kuwalaumu Ukawa kwa chochote kwa sababu wana uhuru wa kushiriki kikamilifu katika Bunge hilo na pia wana uhuru wa kuliacha iwapo wanaona hawaridhishwi nalo,” anasema.

Anasema kama Ukawa waliona mchakato wa Katiba haukuwaridhisha, wana uhuru wa kulisusia na hakuna atakayeweza kuwahukumu.


Chanzo: Mwananchi

 
Ingekuwa vizuri kwa wale wanaosema katiba ni mbovu wa-identify kifungi kipi ni kibovu kuliko kutoa blanket denial.
nadhani utakuwa unapenda kukaa kwenye vijiwe vya kahawa au vingine vyote vinavyofanana na hivyo ambavyo vina sifa kuu ya watu kuzungumza pasi na kupeana nafasi hasa inapozuka hoja yenye mkinzano mkubwa ama wa kisiasa. Na huna muda wa kujishughulisha kujisomea vitabu na sitashangaa sana nikisikia kuwa umeambiwa kuwa rasimu ya Sita nad Chenge ni bora ila hujaisoma.

kwa uchache maoni yetu sisi wananchi ambayo yamepuuzwa ni pamoja na:
1. Wananchi kupokwa madaraka ya kuwawajibisha wabunge ambao hawafanyi kazi walizotumwa na waajiri wao ambao ni sisi wananchi.
2. Wananchi tunataka serikali iwe ndogo ili fedha nyingi ziende kwenye maendeleo, BMK imeona sisi hatuna maono, hapa watawala wamelinda maslahi yao, SASA MAWAZIRI 40 WA NINI, madaraka yangepelekwa kwa Wakurugenzi.
3. Wananchi tulisema watu wasilundikiwe vyeo, kuna Watz wengi tena wenye uwezo, BMK limetupuuza.
4. Wabunge wasiwe mawaziri, pia tumepuuzwa
orodha inaendeleo, Rasimu iliyotangazwa ni katiba maslahi badala ya kuwa katiba ya wananchi, kuwa na fikra huru usishikiwe akili yako
 
Back
Top Bottom