Ni Uwezo wako wa kutambua Fursa

mojax

Member
Aug 18, 2015
13
23
ELIMU BIASHARA

NI UWEZO WAKO

Kufanya maamuzi mara nyingi huwa inategemea na nini kipo kichwani kwako na nini unafahamu kuhusu hicho kitu cha kufanyia maamuzi. Uwezo wa kutambua jambo na uwezo wa kutafakari na kulifanyia maamuzi hutofautiana baina ya mtu na mtu na ndio maana tunatofautiana hata level za maendeleo. Kwa kawaida uwezo huwa unapimwa na mafanikio, ukiwa unapanda cheo ofisini watu watajua una uwezo mkubwa wa kufanya kazi hivyo unastahili nafasi ya juu ofisini.

Swala huwa sio Fursa, swala huwa ni Uwezo wako wa kuona na kuitambua fursa, na kujua ni namna gani ya kuitumia ili kufikia mafanikio. Kwa mfano, Mtwara kinafunguliwa kiwanda cha Dangote, kila mtu anasema kutakua na fursa nyingi, na mimi nakubali, swala ni fursa ipi unaiona? Unaiona fursa ya ajira? Unaiona fursa ya kupata Tender ya kuwa agent wa kusupply cement zao? Unaiona fursa ya kufungua restaurant karibu na kiwanda uuzie wafanyakazi chakula? Unaiona fursa ya kujenga apartment wafanyakazi waje wapange? Unaiona fursa ya kununua kiwanja now ili baadae kikipanda bei ukiuze? Unaiona fursa ya kuandaa kozi ya environment and safety management kwa wafanyakazi wa viwandani? Unaiona Fursa gani?

Fursa zipo nyingi sana, swala ni una uwezo wa kuzifanya? Una uwezo wa Kuthubutu kuikamatia fursa moja ukaitimiza. Una uwezo wa kumshawishi mtu mkaingia joint venture mkafanya au utasema huna mtaji? Una uwezo wa kumshawishi mtu akakupa Mtaji uende ukaifanye? Je, una uwezo wa Kuifanya? Tusilalamike hakuna fursa bali tujifungue uelewa wetu na upana katika kuzifanya na kuzikamilisha Fursa zilizopo.
JIKUNG'UTE, JIPANGE, ANZA.

By Man Dea
#ElimuBiashara #ManDeaIdeas
 
Maelezo mafupi lakini yana maana kubwa na pana sana kwa wajasiriamali.

Ahsante sana
 
mkuu elezea kila kipengele ili uendelee kutukung'uta vumbi. nimeipenda sana
 
mleta mada umenifuraisha sana. Bg up sana. Ni vyema kuwashirikisha wandugu mambo aya ya kufanyia kazi na kuondokana na umaskini.

Mimi labda ni jazie nyama. kwa ujuzi nilio nao katika eneo la ujasiria mali. Eneo lingine ambalo laweza kuku saidia sana kugundua fursa. Ni kupendelea kusafiri.

Kuna fursa nyingi sana mikoani. Katika tafiti zangu nimegundua. Watu hawaoni fursa kwa sababu. Wameshazoea mazingira waliyopo.

Tofauti na mgeni anapokuja labda mtaani kwenu. Au mkoani kwenu uyu inakua raisi sana kuona fursa kuliko mwenyeji.

Maana wenyeji wameshayazoea mazingira ya maali husika.

Ndio maana wachina wanakuja Africa au Tanzania na kutajirika kwa haraka. Kwaiyo ili jambo yatakiwa watanzania tujifunze kutembelea mikoani tusipende kukaa maali pamoja. Fursa zipo nyingi sana uzioni kwa sababu ya kukaa eneo moja kwa muda mrefu.
 
mleta mada umenifuraisha sana. Bg up sana. Ni vyema kuwashirikisha wandugu mambo aya ya kufanyia kazi na kuondokana na umaskini.

Mimi labda ni jazie nyama. kwa ujuzi nilio nao katika eneo la ujasiria mali. Eneo lingine ambalo laweza kuku saidia sana kugundua fursa. Ni kupendelea kusafiri.

Kuna fursa nyingi sana mikoani. Katika tafiti zangu nimegundua. Watu hawaoni fursa kwa sababu. Wameshazoea mazingira waliyopo.

Tofauti na mgeni anapokuja labda mtaani kwenu. Au mkoani kwenu uyu inakua raisi sana kuona fursa kuliko mwenyeji.

MAANA WENYEJI WAMEISHAYAZOEA MAZINGIRA HUSIKA.

Ndio maana wachina wanakuja Africa au Tanzania na kutajirika kwa haraka. Kwaiyo ili jambo yatakiwa watanzania tujifunze kutembelea mikoani tusipende kukaa maali pamoja. Fursa zipo nyingi sana uzioni kwa sababu ya kukaa eneo moja kwa muda mrefu.
Kabisa!
 
Back
Top Bottom