Ni ukweli mtupu Mshahara wa kima cha chini TUCTA wanaoutaka hautekelezeki

Mkandara
Pia cheki mstari wa pili na mwisho kuto mwisho kabisa
 
Mkuu ama kweli nawe mbayuwayu...Hakuna ukweli wowote kisayansi kama hotuba ya JK - Karagabaho!

Mbayuwayu mjanja wewe teh teh teh.
Lakini ubaki ukijua tangia leo walioshiriki kuweka viwango vya mishahara ni hao tucta tangu mwaka jana, miaka ya nyuma kiwango cha chini kilikuwa kimoja.
 
Ni mwaka gani kiwango cha kima cha chini kilikuwa kimoja?..
Nipe mfano ambao ulimtazama housegirl, tingo au mlinzi kuwa sawa na mwajiriwa wa serikali au shirika la Umma..
 
Ni mwaka gani kiwango cha kima cha chini kilikuwa kimoja?..
Nipe mfano ambao ulimtazama housegirl, tingo au mlinzi kuwa sawa na mwajiriwa wa serikali au shirika la Umma..

Miaka ya nyuma hizo sekta zilikuwa si rasmi kama ilivyo kwa wauza vioski ama mashamba boy. Na ilijulikana kama kazi za dayi- worka. Lakini kwa wakati wa miaka ya nyuma mfano ma operator viwandani na wakata mapaki pale ilemela, igoma kiwango ilikuwa kima ya chini. Sema wahindi ni wajanja wajanja fulani walikuwa hawaajiri mtu wanakuita kibarua na kila siku unaingia na ki kuponi fulani. Kwa hiyo ktk hali kama hiyo wanakuripa kulingana na wanavyotaka maana wewe sio mwajiriwa.

Mkandara ,
Walibadirisha mshahara mwaka jana ama juzi baada ya tucta kubeba bango.
 
MkamaP,
Hii ni taarifa iliyotolea mwaka 2007 sijui kama utakuwa na jingine la kusema..Maanake matatizo ni yale yale na hadithi ni ileile..

2007-10-19 10:44:01
Na Mwandishi Wetu

Hivi karibuni serikali ilitangaza kuongeza mishahara sekta binafsi. Tangazo hilo limeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wananchi wengi wao wakisema kuwa hiyo inaweza kuwa danganya toto.
Akitangaza mishahara hiyo Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana , Kepteni (mstaafu) John Chiligati alisema wafanyakazi wa ndani watalipwa Sh. 65,000 kwa mwezi, wahudumu wa baa na nyumba za wageni Sh. 80,000, wakati sekta ya madini, usafiri na mawasiliano itakuwa Sh. 350,000. Makampuni makubwa ya ulinzi na yale ya kigeni yatalipa kima cha chini cha sh. 105,000 wakati makampuni mengine yatalipa Sh. 80,000.

Watalaam na wananchi wamehoji kuwa kuongezeka kwa mishahara hiyo kumezingatia vigezo vipi wakati hali ya uchumi wetu bado haijawa ya kuridhisha?. Takwimu kutoka Wizara ya Mipango Uchumi na uwezeshaji zinaonyesha kuwa katika kipindi cha mwaka 2006, pato halisi la Taifa lilikua kwa asilimia 6.2, ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 6.7 mwaka 2005.

Kushuka kwa kiwango cha ukuaji wa Pato la Taifa kulisababishwa na ukame uliotokea katika maeneo mengi nchini katika msimu wa mvua wa mwaka 2005/06, ukosefu wa umeme na kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia. Kuongeza mishahara sekta binafsi ambayo ndiyo inachangia kwa kiasi kikubwa kwenye pato la taifa kutazidi kuiathiri sekta hiyo kwani bado inakabiliwa na matatizo mengi.

Sekta zilizoathirika zaidi na kushuka huko ni kilimo; bidhaa za viwandani; umeme na maji. Viwango vya ukuaji viliongezeka kwa sekta za uuzaji wa jumla, rejareja, na mahoteli na utalii; uchukuzi na mawasiliano; madini; na fedha, bima na huduma za kibiashara. Sasa kutokana na takwimu hizo, kweli kuna dalili ya mishahara hiyo kuongezeka au kuna kitu kingine kinachofichwa?,anahoji Dk S. Kessy kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Pamoja na kuongeza mishahara sekta binafsi lakini bado inaonekana kasi ya upandaji wa bei inazidi kuongezeka kila kukicha, hii inaashiria kuwa hata kama kweli mishahara hiyo itaongezeka kiasi gani hali itazidi kuwa siyo nzuri. Mtalaam huyo anasema badala ya kuongeza mishahara serikali ilitakiwa kuangalia namna ya kudhibiti kasi ya upandaji wa bei za bidhaa.

``Kuna tabia ambayo si nzuri iliyojengeka miongoni mwa wananchi hasa wafanyabishara ambapo pindi serikali ikitangaza ongezeko la mishahara nao huongeza bei za bidhaa, `` anasema.

Hata hivyo wananchi kadhaa waliohojiwa kuhusiana na ongezeko la mishahara hiyo hawakufurahishwa na kudai kuwa imelenga kuzima makelele ya wapinzania ambao kwa siku za karibuni wamekuwa wakiisakama serikali. Aidha wamedai baadhi ya nyongeza hizo hazikuzingatia mambo kadhaa na kwamba nyingine ni vigumu kufuatiliwa ili kuhakikisha kwamba waajiri wanalipa kama serikali ilivyotangaza.

Hata hivyo wengine wameipongeza serikali kwa hatua hiyo na kuitaka ifuatilie kuona kwamba waajiri binafsi wanawalipa watumishi wao mishahara iliyoanishwa.
Akizungumza, mmoja wa wananchi hao, Bw. Dominic Lyasa amekaririwa akisema kama serikali ilikuwa na lengo zuri la kuwasaidia wananchi ingezuia mawaziri kuzunguka mikoani ambapo inakadiriwa kuwa watatumia Sh. milioni 100 na kwamba ingehakikisha kuwa wanawake wajawazito hawalali chini kwa kukosa vitanda kwenye hospitali mbalimbali. Hata hivyo alisema, sio rahisi serikali kufuatilia waajiri wa wahudumu wa ndani kwa lengo la kubaini kama wanawalipa mshahara Sh. 65,000 kwa mwezi.

Bw. Zaa Twalengeti kutoka Muungano wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini (TANGO), anasema suala la kuwalipa `mahausigeli` linaweza kuangaliwa upya kwa sababu kiwango hicho ni kikubwa kwa familia nyingi.
`Ningependa nimlipe hausigeli wangu hata sh. Lakini moja lakini nitaweza wapi? Isitoshe serikali inasahau kwamba mahausigeli wengi wanakula bure, kuoga na kulala bure pamoja na huduma nyingine wanazopata wanafamilia. Kwa wale wanaofanya kazi na kuondoka pengine mshahara huo ni sahihi,` alisema.
Bw. Twalengeti anasema kwamba serikali inamtaka mtu amlipe hausigeli sh. 65,000 wakati mwajiri wake anamlipa mshahara unaolingana na huo.
`Sasa mtumishi kama huyu atamlipa nini hausigeli wakati ndiye anamlelea wanawe ili naye akalitumikie taifa?` aanahoji.

Alidai hata kama gharama nyingine zitapunguzwa lakini bado hausi geli atabaki na fedha nyingi ambazo wananchi wengi hawatamudu kulipa.
Naye James Kicheere mkazi wa Mwananyamala anasema , ni kawaida ya serikali kuzima hasira za wananchi kiujanja kila zinapojitokeza tuhuma za ufisadi dhidi ya viongozi.
Alitoa mfano wakati fulani kulikuwa na mjadala mkali sana juu ya tuhuma za rushwa zilizojitokeza bungeni lakini kwa kutaka kuzizima serikali iliikaribisha timu ya mpira ya Taifa bungeni.

Alisema lengo la kuipeleka timu ya taifa lilikuwa ni kuwafanya wananchi waachane na mjadala uliokuwepo wakati huo na kuanza kuzungumzia masuala ya michezo. Mmiliki mmoja wa bar maeneo ya Mbagala jijini, alisema hilo likitekelezeka watu wengi watakosa kazi kwa kuwa waajiri watashindwa kumudu kulipa mishahara kwa viwango hivyo. Kwani anasema waajiri wengi wataamua kupunguza idadi ya wafanyakazi na kubaki na wachache watakaomudu kuwalipa viwango hivyo vipya.

`Mtu ana kabaa kake mtaani kanauza kreti moja na nusu za bia na soda kwa siku kwa hiyo ni dhahiri kuwa hatoweza kuwalipa wafanyakazi kiasi hicho na anaweza kufunga baa kabisa,` alisema.

Kwa baadhi ya baa waajiriwa wamekuwa walipwa kulingana na idadi ya vinywaji anavyouza kwa siku jambo ambalo kuna siku mfanyakazi huo anaweza akaoka na fedha nyingi au kidogo sana kutegemeana na hali halisi ya wateja. Hata hivyo, alipongeza uamuzi wa serikali kuwa ni mzuri ila alionya kuwa ufuatiliaji wa karibu usipofanywa hakuna mwajiri atakayelipa viwango hivyo vipya. Wananchi wengi na vyama vya wafanyakazi pia wameitaka serikali kutangaza mishahara ya sekta ya umma ili kulinganisha.

Hata hivyo serikali imesema kuwa haitalazimika kutangaza mishahara ya wafanyakazi wake kwa shinikizo linalowekwa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini kwa sababu viongozi hao si wafanyakazi. Msimamo huo wa serikali umetolewa hivi karibuni mjini Babati na Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa, wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa Wilaya ya Babati mkoani Manyara, alipokuwa akielezea bajeti ya mwaka 2007/08.

Dk. Ngasongwa amekaririwa akisema: ``Tumekubaliana na wafanyakazi wenyewe kutotangaza mishahara yao kwa sababu tukiitangaza tunawasababishia matatizo. Aliongeza: ``Mshahara tumeongeza lakini hatuwezi kufikia laki tatu. Kwa uchumi huu tukifikia hapo uchumi utaanguka.``

Waziri aliamua kueleza msimamo huo wa serikali baada ya mfanyakazi mmoja kulalamikia kiasi kidogo cha mshahara kinachotolewa na serikali, alichodai kuwa hakiwezi kumkomboa mfanyakazi na kuwa na maisha bora wakati bei za vitu zinaendelea kupanda. Watalaam wa masuala ya uchumi wameishauri serikali badala ya kupandisha mishahara iangalie uwezekano wa kupunguza mfumko wa bei ambao kwa sasa umefikia asilimia kumi.

Akizungumza katika mahojiano hivi karibuni, afisa kutoka kitengo cha uchumi wa shirika la fedha la kimataifa IMF Bw Roger Nord, amesema hatua zaidi zinatakiwa kuchukuliwa kudhibiti mfumuko wa bei pamoja na serikali kupunguza matumizi ya ndani ili kuimarisha mwelekeo mzuri wa uchumi uliopo hivi sasa. Anasema kuna umuhimu kwa benki kuu kuhakikisha kuwa inadhibiti mfumko wa bei ili kuufanya uchumi uendelee kuongezeka.

Hata hivyo kupanda kwa mishahara kunaweza kutoleta maana yeyote wala kuongeza uzalishaji katika sekta binafsi kutokana na kutokuwapo kwa mazingira ya kuvutia. Kwa ujumla sekta binafsi bado inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinahitaji kuondolewa ili kuifanya ikue.
Moja ya changamoto ni miundo mbinu hafifu, kushuka kwa thamani ya shilingi, kupanda kwa bei ya mafuta na baadhi ya kodi. Endapo serikali inataka kuifanya sekta binafsi ikuwe na kuongeza mchango wake katika pato la taifa inatakiwa kuangalia changamoto hizo.

Tanzania inayokadiriwa kuwa na watu zaidi ya milioni 37 , pato la mwaka la mwananchi wa chini limeongezeka kutoka shilingi 360,865mwaka 2005 hadi shilingi 399, 873 mwaka 2006. Kuongezeka kwa pato la mwananchi hakumanishi kuwa hata hali ya maisha yake imebadilika, bado juhudi zaidi zinatakiwa ili kuhakikisha kuwa kasi yaongezeko la bei inapungua kwa kujaribu kuondoa au kupunguza kodi ya mafuta ya mitambo ambayo imekuwa chanzo kikuu cha ongezeko hilo.
 
Mheshimiwa raisi kaongea tu kwa jaziba au alishauriwa vibaya,kwani sisi wote pamoja na yeye mwenyewe tunajua wazi kuwa hicho kima cha chini wanachotaka TUCTA kinalipika bila matatizo yoyote kma serikali itasimamia vizuri vyanzo vya income yake.
 
Kunradhi wana JF na TUCTA kama nitawakwaza kwa kuuliza kuwa hivi mbona sijasikia suala la productivity likizungumziwa ? Jee hili siyo suala la msingi kabla ya yote? Jee haiwezekani wazee hawa wakabulliana kuwa a certain percentage of the budget ya serikali iwe ni mishahara hivyo productivity na efficiency vikiongezeka na wastage ikipungua ni endelevu zaidi [kwani kila serikali itakapokusanya zaidi automatically mishahara itapanda. JUST THINKING OUT ALOUD
Wananchi na wana jamii wenzagu

Kiu -halisia mshahara wa kima cha chini cha zaidi ya US dola 300 kwa wafanyakazi wa Tanzania hautekelezeki.
Haiwezekani na haiwezekani, mfanyakazi anayedai huo mshahara itambidi adai zaidi ya hapo mara mbili ili atekeleze. Mfano wewe ni mwalimu wa kike una mtoto na umeajiri dada wa kumlea nyumbani itakubidi umlipe dada huyo zaidi ya us dola 300. Na utaishi je? itabidi udai tena zaidi us dola 300 kutoka serikalini ili upate kuishi.

Ugiriki lwo wamefirisika kwa sababu nao wafanya kazi wali dai ongezeko kama hilo. Ugiriki wanahaha kutafuta sehemu ya kukopa, EURO imeanguka sababu ya ugiriki.

Naungana na JK mshahara huo hautekelezeki.
 
Kunradhi wana JF na TUCTA kama nitawakwaza kwa kuuliza kuwa hivi mbona sijasikia suala la productivity likizungumziwa ? Jee hili siyo suala la msingi kabla ya yote? Jee haiwezekani wazee hawa wakabulliana kuwa a certain percentage of the budget ya serikali iwe ni mishahara hivyo productivity na efficiency vikiongezeka na wastage ikipungua ni endelevu zaidi [kwani kila serikali itakapokusanya zaidi automatically mishahara itapanda. JUST THINKING OUT ALOUD

Mhhh
Kodi ikikusanywa na kudhibiti mafisadi mashahara unalipika. Mimi chichemi kitu
 
Abunuasi,
Mkuu Productivity ktk sekta ya serikali huanza na huduma zenyewe kuwa bora hapa hakuna uzalishaji isipokuwa huduma. Kinachogomba hapa ni mishshara duni kwa wafanayakzi waserikalikiasi kwamba kila mfanyakazi wa serikali ana kijiofisi chake pembeni. Ukitaka Passport unazunguka, Ukitaka huduma ya Hospital au elimu ni lazima upitie ktk ofisi zao kupata huduma safi na bora kuliko ile ya serikali.

Na ukitazama undani wa hali hii umetokana na mishahara midogo sana na jambo moja lililonikera zaidi nilipokuwa tanzania ni kwamba hata wale watoto wanaosoma Private schools ni lazima wapate tuition jioni kwa malipo ya ziada. Kuna rafiki yangu ana mwanaye anasoma Internatioonal school akilipa ada ya dollar 14,000 kwa mwaka, lakini watoto wake bado wanaenda tuition jioni kulingana na mapendekezo ya walimu...Hii kweli ni - HAKI?

Kama nilivyosema mdogowangu alifanyiwa operation ya Apendix, ujumla wa gharama ilifikia Tsh 800 tena Muhimbili. Na wala sii yeye pekee kuna gharama kubwa ktk Elimu na Afya kiasi kwamba unashindwa kuelewa fedha zinapelekwa wapi hasa ikiwa pato la serikali linatokana na kodi zetu.

Mimi naamini kabisa maelezo ya Tucta kwamba ipo kila sababu ya kuongeza mishahara ya chini kulingana na maisha yetu laa sivyo Bank kuu ithaminishe Tsh kulingana na mfumko wa bei ili wananchi wapate uhalali wa mishahara wanayopokea..Kweli haiwezekani kuwapa wananchi mshahara mmoja kima cha chini sekta zote kama MkamaP alivyokuwa akifikiria toka mwanzo - Haiwezekani, haiwezekani kwa sababu ya Mazingira yetu na hali halisi ya kima hicho kwa watu wote nchini ambao asilimia kubwa wapo ktk kima hicho..

Pia, Watanzania ni watu wavivu sana, wavivu wa kufikiri na wavivu kufanya kazi, wavivu wa kujali muda na uzalishaji hivyo hatujui thamani ya nguvu na kazi zetu. Utamaduni wetu umebeba sana na mila za Kikoloni na utumwa ambazo ndio rolemodel ya mafanikio..Ulaya huwezi kukuta mtu akiwa na mtumishi (housegirl) mfungua gate mkata majani, sijui mlinzi na kadhalika kwa kipato cha kati (middle class) lakini Afrika na hasa Tanzania kila familia ina Kijakazi..

Na kama umesoma hapo juu kuna kiongozi wa vyama hivi vya ushirika amediriki hata kudai kwamba mishahara ya housegirl ni mikubwa pasipo kufikiria kwamba utaratibu wote wa kuwa na Kijakazi ni fikra za Kikoloni na Utumwa. Amediriki hata kutaja salio la kijakazi kuwa ni malipo bora zaidi ya mwajiri ambaye halazimiki kuwa na Kijakazi, ila analazimika kuomba haki yake kwa kusema mshahara anaopata ni mdogo hauwezi kukidhi mahitaji yake. Ni akili ya kitumwa kuangalia mwenzako anapata ngapi ili upime uhalali wa malipo yako hali ni mchakato mzima wa maisha, elimu, uzalishaji na true value ya fedha unayopokea ndiyo thamani halisi ya kazi yako.

Hata hivyo mkuu wangu kinachogomba hapa ni uwezekano wa serikali kulipa mshahara huo. Serikali inaweza kuwalipa wafanyakazi kiwango hicho kama serikali yenyewe itakuwa na uwazi ktk jambo hili. Serikali itakuwa tayari kukubali kutazama njia na mbinu ambazo wachumi na wahadhiri wamependekeza. Inawezekana tu ikiwa kuna transfer na makato ya matumizi ktk sekta nyinginezo kwa sababu kama iitokea vita kesho basi utaona serikali ikikusanya fedha na kuwa na uwezo wa ajabu kijeshi kupambana na uvamizi. Ikitokea njaa na ukame tutasubiri misaada ya ILO na Red cross kutusaidia kwa sababu waathirika sii viongozi wa Ikulu..
 
Abunuasi,
Mkuu Productivity ktk sekta ya serikali huanza na huduma zenyewe kuwa bora hapa hakuna uzalishaji isipokuwa huduma. Kinachogomba hapa ni mishshara duni kwa wafanayakzi waserikalikiasi kwamba kila mfanyakazi wa serikali ana kijiofisi chake pembeni. Ukitaka Passport unazunguka, Ukitaka huduma ya Hospital au elimu ni lazima upitie ktk ofisi zao kupata huduma safi na bora kuliko ile ya serikali.

Na ukitazama undani wa hali hii umetokana na mishahara midogo sana na jambo moja lililonikera zaidi nilipokuwa tanzania ni kwamba hata wale watoto wanaosoma Private schools ni lazima wapate tuition jioni kwa malipo ya ziada. Kuna rafiki yangu ana mwanaye anasoma Internatioonal school akilipa ada ya dollar 14,000 kwa mwaka, lakini watoto wake bado wanaenda tuition jioni kulingana na mapendekezo ya walimu...Hii kweli ni - HAKI?

Kama nilivyosema mdogowangu alifanyiwa operation ya Apendix, ujumla wa gharama ilifikia Tsh 800 tena Muhimbili. Na wala sii yeye pekee kuna gharama kubwa ktk Elimu na Afya kiasi kwamba unashindwa kuelewa fedha zinapelekwa wapi hasa ikiwa pato la serikali linatokana na kodi zetu.

Mimi naamini kabisa maelezo ya Tucta kwamba ipo kila sababu ya kuongeza mishahara ya chini kulingana na maisha yetu laa sivyo Bank kuu ithaminishe Tsh kulingana na mfumko wa bei ili wananchi wapate uhalali wa mishahara wanayopokea..Kweli haiwezekani kuwapa wananchi mshahara mmoja kima cha chini sekta zote. Haiwezekani kwa sababu ya Mazingira yetu..Watanzania ni watu wavivu sana, wavivu kufikiri na wavivu kufanya kazi. Utamaduni wetu umebeba sana na mila za Kikoloni na utumwa ambazo ndio rolemodel ya mafanikio..Ulaya huwezi kukuta mtu akiwa na mtumishi (housegirl) mfungua gate mkata majani, sijui mlinzi na kadhalika kwa kipato cha kati (middle class) lakini Afrika na hasa Tanzania kila familia ina Kijakazi..

Na kama umesoma hapo juu kuna kiongozi wa vyama hivi vya ushirika amediriki hata kudai kwamba mishahara ya housegirl ni mikubwa pasipo kufikiria kwamba utaratibu wote wa kuwa na Kijakazi ni fikra za Kikoloni na Utumwa. Amediriki hata kutaja salio la kijakazi kuwa ni malipo bora zaidi ya mwajiri ambaye halazimiki kuwa na Kijakazi, ila analazimika kuomba haki yake kwa kusema mshahara anaopata ni mdogo hauwezi kukidhi mahitaji yake. Ni akili ya kitumwa kuangalia mwenzako anapata ngapi ili upime uhalali wa malipo yako hali ni mchakato mzima wa maisha, elimu, uzalishaji na true value ya fedha unayopokea ndiyo thamani halisi ya kazi yako.

Hata hivyo mkuu wangu kinachogomba hapa ni uwezekano wa serikali kulipa mshahara huo. Serikali inaweza kuwalipa wafanyakazi kiwango hicho kama serikali yenyewe itakuwa na uwazi ktk jambo hili. Serikali itakuwa tayari kukubali kutazama njia na mbinu ambazo wachumi na wahadhiri wamependekeza. Inawezekana tu ikiwa kuna transfer na makato ya matumizi ktk sekta nyinginezo kwa sababu kama iitokea vita kesho basi utaona serikali ikikusanya fedha na kuwa na uwezo wa ajabu kijeshi kupambana na uvamizi. Ikitokea njaa na ukame tutasubiri misaada ya ILO na Red cross kutusaidia kwa sababu waathirika sii viongozi wa Ikulu..

Hao wote ni bakora tu ndo zinawafaa.
Hizo ndo roho za kifisadi tunazoziongea, kwamba watanzania karibu wote ni mafisadi . Ndio wakipata chansi kama ya RA nao hao watafisadi kwa kasi ile ile.
Lowasa ama RA hawakutengeneza richmondi kwa sababu ya mshahara mdogo, bali ni huruka iliyo damuni tu kama walivyo watanzania wengine kwa nafasi zao.
 
Hao wote ni bakora tu ndo zinawafaa.
Hizo ndo roho za kifisadi tunazoziongea, kwamba watanzania karibu wote ni mafisadi . Ndio wakipata chansi kama ya RA nao hao watafisadi kwa kasi ile ile.
Lowasa ama RA hawakutengeneza richmondi kwa sababu ya mshahara mdogo, bali ni huruka iliyo damuni tu kama walivyo watanzania wengine kwa nafasi zao.
Well, a Corrupt Government ndiyo chanzo cha wananchi wake kufuata matendo yao..Ndio maana wahenga husema - Practice what U preach! Hao watumishi wote wala rushwa ni matokeo ya uongozi mbaya na ndio maana wenzetu huziondoa madarakani serikali zilizo corrupt.
 
Na ukitazama undani wa hali hii umetokana na mishahara midogo sana na jambo moja lililonikera zaidi nilipokuwa tanzania ni kwamba hata wale watoto wanaosoma Private schools ni lazima wapate tuition jioni kwa malipo ya ziada. Kuna rafiki yangu ana mwanaye anasoma Internatioonal school akilipa ada ya dollar 14,000 kwa mwaka, lakini watoto wake bado wanaenda tuition jioni kulingana na mapendekezo ya walimu...Hii kweli ni - HAKI?

i hope the quality of education reflects the fee,but according to this statemnt,i doubt

Kama nilivyosema mdogowangu alifanyiwa operation ya Apendix, ujumla wa gharama ilifikia Tsh 800 tena Muhimbili.

u meant tsh80,000?tsh800,000,?tsh8,000,000?
 
Matumizi hayo walikopa sana kuziba nakisi iliyotokana na matumizi makubwa yanatokana na nyanja mbili kuu yaani Wage bill pamoja na matumizi ya ununuzi wa silaha kwani wanamgogoro na uturuki wa eneo la mpakani lenye mafuta.
 
Kweli mnawalipa hivi watawala wenu? Kwa wanaojua hesabu

Zote hizi ni kwa mwezi:

[24 x 2,422,000 =
21 x 2,046,000 =
27 x 2,080,000 =
1 x 4,850,000 =
1 x 4,850,000 =
323 x 1,921,000 =
127 x 1,921,000 =
] [12]

The process is also known as "the order of operation"...



Ukipata jibu.. utakuwa na weekend mbaya kweli!


MkamaP kwanini hawa waweze kulipwa hivi na sio wale wanaoomba tsh 315,000??
Uliwahi kuzungumzia uzalishaji,hawa wanaolipwa hivi hapo juu wanauzalishaji gani unao-justify mishahara yao??

 
Back
Top Bottom