Habarini wapendwa.
Kuna suala moja limekuwa likinitatiza sana na nimekuwa najiuliza mara kwa mara bila kupata majibu yanayoridhisha.
Jambo hili linahusiana na mgawanyo wa pato la taifa.
Binafsi nimekuwa nikihisi kwamba wanaofaidi mali ya nchi ni wanasiasa huku wataalamu wa fani mbalimbali wakitelekezwa.
Najua naweza kupata msaada wa mawazo hapa. Sioni sababu ya wabunge kulipwa zaidi ya wataalamu wetu kama madaktari, walimu nk.
Sina hakika kama hili limekaa sawa na sina hakika kama nchi za wenzetu wanawalipa wanasiasa zaidi ya wataalamu.
Kutokana na mgawanyo mbovu bunge limejaa wataalamu lukuki ambao wamekimbia fani zao zenye maslahi duni na kwenda bungeni kupiga longolongo na kujipatia maslahi maradufu. Tunakwenda wapi?
Naomba msaada katika hili.
Nawakilisha.
Kuna suala moja limekuwa likinitatiza sana na nimekuwa najiuliza mara kwa mara bila kupata majibu yanayoridhisha.
Jambo hili linahusiana na mgawanyo wa pato la taifa.
Binafsi nimekuwa nikihisi kwamba wanaofaidi mali ya nchi ni wanasiasa huku wataalamu wa fani mbalimbali wakitelekezwa.
Najua naweza kupata msaada wa mawazo hapa. Sioni sababu ya wabunge kulipwa zaidi ya wataalamu wetu kama madaktari, walimu nk.
Sina hakika kama hili limekaa sawa na sina hakika kama nchi za wenzetu wanawalipa wanasiasa zaidi ya wataalamu.
Kutokana na mgawanyo mbovu bunge limejaa wataalamu lukuki ambao wamekimbia fani zao zenye maslahi duni na kwenda bungeni kupiga longolongo na kujipatia maslahi maradufu. Tunakwenda wapi?
Naomba msaada katika hili.
Nawakilisha.