lwambof07
JF-Expert Member
- Jul 12, 2016
- 4,593
- 5,203
Hellow JF
Nianze kwa kusema kuwa kuna msemo usemao kuzaa huwa sio kazi bali kazi hasa huwa ni kumlea huyo aliyezaliwa kukua katika misingi iliyo bora na awe na tabia njema/nzuri zinazomfurahisha kila mtu anayekutana naye na wahenga husema samaki mkunje angali mbichi.
Mara kadhaa pale mtoto anapokuwa na tabia mbaya lawama hutupiwa mwanamke kuwa ameshindwa kumlea mtoto na je kwa nini wababa huwatupia lawama wamama zaidi?
Kwa upande mwengine unaweza kusema kuwa wazazi wa kiume wako sawa kwa sababu tu ni ule ukweli usiopingika asilimia kubwa ya wababa hutumia muda mchache sana kuwa na watoto wao tofauti na mama nianze kwa kutoa mifano miwili ambayo mimi mwenyewe nimeshuhudia kwa macho yangu.
1.)Nilipata bahati ya kumtembelea ndugu yangu na kukaa pale kwake siku kadhaa pale kuna dada wa kazi lakin pia kuna binti ndugu yake mwanamke ambaye mtoto wake anamuita shangazi sasa nyumba ile mama mwenye nyumba hafanyi kazi kabisa yeye ni kutuma tena humtumia mwanaye mwenye umri wa miaka 9 yupo darasa la nne.
Yule mtoto akirud kutoka shule anafanya homework zake chap kwenye T.V hapo ni mwendo wa katuni hadi saa sita usiku ndipo analala na remote anaficha wale wadada wakibadilisha tu kuweka michezo yao dogo mbio kwa mama wamebadilisha wameweka michezo yao utasikia nyie muwekeeni mtoto katuni basi wale wadada wana sepa zao nje wakiondoka dogo mbio kwa mama utasikia mama wakina dada wamekasirika wameniacha peke yangu utasikia mama mtu nyie msimuache mtoto peke yake sebuleni.
Yule dogo akimaliza kula sahani anaacha hapo hapo watatoa wadada kuna siku walikuja wageni wadada wakaandaa msosi mezani vizuri wadada wanataka kuwakaribisha wageni dogo kawahi mezani funua funua kachukua paja sasa shangazi yake akawa anamkonyeza si usubir kwanza wageni waanze kupakua dogo akalipuka sasa shangazi mimi si nina njaa jamani shangazi mtu ikabidi awe mpole.
Shangazi alinambia yaani huyu mtoto we acha tu usiku tumelala si akaniamsha anataka maji nikaenda mchukulia akanywa yale yaliyobaki akamwagia kitandani ule upande ninaolala sasa mm sikusema kitu nikashuka zangu chini nikalala dogo choropo kwa mama yake mama shangazi amelala chini ameniacha peke yangu kitandani mama mtu huyo lala kitandani na mtoto hakuna cha kuuliza sababu wala nn basi nikalala kibishi hvyo hvyo.
Siku nyingine ametoka zake shule wadada wapo nje wanapika akasalimia zake halafu akasema naona dada wa kazi mdogo na mkubwa wanapika akesepa zake ndani.Yule dogo chochote anachotaka anapewa na mama yake sasa maagizo anampa mwanaye then mtoto anakuja kuwapa wadada mama kasema leo mpike hivi na hivi,mama kasema pale mlangoni kuna nguo zangu na zake mfue na amesema zitakate,mama amesema muamke kumeshakucha mkafanye kazi na mfagie mavi ya mbwa yote.
Akirudi shule kama hamna anachokipenda mezani na mama yake hayupo huyo kwenye simu ya mezani mama leo wapika nisivyopenda anamwambia haya muite dada aje dada akienda haya dada mpikie mtoto vitu anavyotaka.
Ikiwa siku ya kufanya fumigation nyumba nzima anatoa tu maelekezo basi wadada watatoa vitu vyote nje nyumba inakuwa tupu wanapiga dawa wanarudishia vitu mama na mtoto wanarudi usikuu utamsikia mama mtu mimi nina allergy na hizi dawa mtoto sasa leo nyumba imependeza.
Baba mtu hanaga hayo mambo sema shida anatoka asubuhi kurud usiku hana muda wa kutosha pale nyumbani na akiwepo nyumbani yule dogo huwa anakosa amani flan hivi kwa sababu baba yake hataki ujinga na hata akiwepo hamwambii kitu chochote baba yake kwa mama .
2.)Jirani mtaa tunaoishi kuna mdada mmoja amepewa na jamaa mmoja hivi sema alimkuta na mtoto tayari alikuwa na umri wa miaka 3 wakati anamuoa ila sasa mama mtu ametengeneza mazingira dogo amuone jamaa kama baba yake na sasa hivi dogo ana miaka 7 lakini anamuita baba yule jamaa baada ya kuliona hili nikasema kumbe mwanamke ana mchango mkubwa sana kwenye malezi na tabia kwa ujumla maana mama amefanikiwa mtoto wake kumuona jamaa kama baba yake na dogo anamjua baba yake mzazi na anampenda vibaya sema siku hizi hawaonani maana alimtelekeza mtoto so mama mtu amechukia.
Kwa mantiki hiyo mtoto ni mama mama akiwa hayupo vizuri kwenye malezi mtoto ni rahisi sana kupotea.
Nianze kwa kusema kuwa kuna msemo usemao kuzaa huwa sio kazi bali kazi hasa huwa ni kumlea huyo aliyezaliwa kukua katika misingi iliyo bora na awe na tabia njema/nzuri zinazomfurahisha kila mtu anayekutana naye na wahenga husema samaki mkunje angali mbichi.
Mara kadhaa pale mtoto anapokuwa na tabia mbaya lawama hutupiwa mwanamke kuwa ameshindwa kumlea mtoto na je kwa nini wababa huwatupia lawama wamama zaidi?
Kwa upande mwengine unaweza kusema kuwa wazazi wa kiume wako sawa kwa sababu tu ni ule ukweli usiopingika asilimia kubwa ya wababa hutumia muda mchache sana kuwa na watoto wao tofauti na mama nianze kwa kutoa mifano miwili ambayo mimi mwenyewe nimeshuhudia kwa macho yangu.
1.)Nilipata bahati ya kumtembelea ndugu yangu na kukaa pale kwake siku kadhaa pale kuna dada wa kazi lakin pia kuna binti ndugu yake mwanamke ambaye mtoto wake anamuita shangazi sasa nyumba ile mama mwenye nyumba hafanyi kazi kabisa yeye ni kutuma tena humtumia mwanaye mwenye umri wa miaka 9 yupo darasa la nne.
Yule mtoto akirud kutoka shule anafanya homework zake chap kwenye T.V hapo ni mwendo wa katuni hadi saa sita usiku ndipo analala na remote anaficha wale wadada wakibadilisha tu kuweka michezo yao dogo mbio kwa mama wamebadilisha wameweka michezo yao utasikia nyie muwekeeni mtoto katuni basi wale wadada wana sepa zao nje wakiondoka dogo mbio kwa mama utasikia mama wakina dada wamekasirika wameniacha peke yangu utasikia mama mtu nyie msimuache mtoto peke yake sebuleni.
Yule dogo akimaliza kula sahani anaacha hapo hapo watatoa wadada kuna siku walikuja wageni wadada wakaandaa msosi mezani vizuri wadada wanataka kuwakaribisha wageni dogo kawahi mezani funua funua kachukua paja sasa shangazi yake akawa anamkonyeza si usubir kwanza wageni waanze kupakua dogo akalipuka sasa shangazi mimi si nina njaa jamani shangazi mtu ikabidi awe mpole.
Shangazi alinambia yaani huyu mtoto we acha tu usiku tumelala si akaniamsha anataka maji nikaenda mchukulia akanywa yale yaliyobaki akamwagia kitandani ule upande ninaolala sasa mm sikusema kitu nikashuka zangu chini nikalala dogo choropo kwa mama yake mama shangazi amelala chini ameniacha peke yangu kitandani mama mtu huyo lala kitandani na mtoto hakuna cha kuuliza sababu wala nn basi nikalala kibishi hvyo hvyo.
Siku nyingine ametoka zake shule wadada wapo nje wanapika akasalimia zake halafu akasema naona dada wa kazi mdogo na mkubwa wanapika akesepa zake ndani.Yule dogo chochote anachotaka anapewa na mama yake sasa maagizo anampa mwanaye then mtoto anakuja kuwapa wadada mama kasema leo mpike hivi na hivi,mama kasema pale mlangoni kuna nguo zangu na zake mfue na amesema zitakate,mama amesema muamke kumeshakucha mkafanye kazi na mfagie mavi ya mbwa yote.
Akirudi shule kama hamna anachokipenda mezani na mama yake hayupo huyo kwenye simu ya mezani mama leo wapika nisivyopenda anamwambia haya muite dada aje dada akienda haya dada mpikie mtoto vitu anavyotaka.
Ikiwa siku ya kufanya fumigation nyumba nzima anatoa tu maelekezo basi wadada watatoa vitu vyote nje nyumba inakuwa tupu wanapiga dawa wanarudishia vitu mama na mtoto wanarudi usikuu utamsikia mama mtu mimi nina allergy na hizi dawa mtoto sasa leo nyumba imependeza.
Baba mtu hanaga hayo mambo sema shida anatoka asubuhi kurud usiku hana muda wa kutosha pale nyumbani na akiwepo nyumbani yule dogo huwa anakosa amani flan hivi kwa sababu baba yake hataki ujinga na hata akiwepo hamwambii kitu chochote baba yake kwa mama .
2.)Jirani mtaa tunaoishi kuna mdada mmoja amepewa na jamaa mmoja hivi sema alimkuta na mtoto tayari alikuwa na umri wa miaka 3 wakati anamuoa ila sasa mama mtu ametengeneza mazingira dogo amuone jamaa kama baba yake na sasa hivi dogo ana miaka 7 lakini anamuita baba yule jamaa baada ya kuliona hili nikasema kumbe mwanamke ana mchango mkubwa sana kwenye malezi na tabia kwa ujumla maana mama amefanikiwa mtoto wake kumuona jamaa kama baba yake na dogo anamjua baba yake mzazi na anampenda vibaya sema siku hizi hawaonani maana alimtelekeza mtoto so mama mtu amechukia.
Kwa mantiki hiyo mtoto ni mama mama akiwa hayupo vizuri kwenye malezi mtoto ni rahisi sana kupotea.