Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Katika siku za hivi karibuni Msajiri wa vyama vya siasa alitangaza mgaho wa ruzuku wa kwa vyama vya siasa. Takwimu hizo zinaonyesha mgaho wa ccm ni mara nne ya ule wa chadema. Tofauti hii bila shaka inatokana kwa kiasi kikubwa na uwiano wa kura za urais walizopata wagombea kupitia tiketi za vyama hivyo. Kwakuwa kwa mujibu wa taarifa ambazo zimekuwa zinatolewa na chadema, tume ya uchaguzi ilimpa ushindi mgombea wa ccm hasio ustahili; na kwakuwa katika kufanya hivyo amekiwezesha chama hicho kupata ruzuku kubwa kuliko stahili yake; ni sababu zipi zinaifanya chadema ishindwe kuifungulia kesi ya jinai tume hiyo kwa kula njama na ccm kupunguza kura zake kwa lengo la kukiibia fedha zake za ruzuku. maoni