Tausi Rehani
Member
- Aug 29, 2020
- 20
- 40
Wasaalam,
Hivi karibuni humu kumekuwa na ongezeko kubwa la nyuzi(threads) zenye mlengo wa kuwadhalilisha wahitimu wa vyuo vikuu (graduates) na wanafunzi waliopo vyuoni kwamba ni useless na hawana uwezo wa kujitegemea kabisa.
Kwa utafiti nilioufanya, hii kampeni inaendeshwa kwa asilimia kubwa na watu ambao hawakubahatika kabisa kufika ngazi ya chuo kikuu ( Yaan Form Four Failures) na baadhi yao Ni walifika ngazi ya chuo kikuu lakini walitoka patupu. Maana siku zote asiyesoma ndo anayemsema aliyesoma. Huwezi mkuta aliyesoma anamsema asiyesoma.
Nadhani wahusika wa hii kampeni iwe kwa makusudi au bahati mbaya wanasahau kuwa lengo kubwa la elimu ni kutoa ujinga na kujaza maarifa ambayo yatamsaidia mlengwa kuendesha maisha ya kila siku.
Level ya chuo kikuu Ni tofauti na level za chini ambako unajiendea kama garii bovu. Ukishafika chuo kuna specialisation mfano mtu anaspecialize kwenye Mining Engineering, Pharmaceutical sciences au IT.
Na Lengo la Elimu hiyo Ni kumpa mtu maarifa ya kama Ni pharmacy akigraduate ajue jinsi ya kutumia hiyo pharmaceutical science aliyosomea kujikwamua kimaisha iwe kwa kuajiriwa au kujiajiri na Si vinginevyo.
Unaposema unataka kuona wahitimu wanaendesha bodaboda au wanakaanga chipsi unaondoa lile lengo la specialisation aliyoipata chuoni. Hapa unalazimisha tuwe na taifa la ovyo lisilo na wataalamu miaka kadhaa ijayo.
Kutangatanga kama kuku wa kienyeji ni Kwa aliyekosa hiyo specialization mostly wenye ajenda hii ovu , kama hukusoma mpaka kuspecialize kwenye kitu kimoja basi endelea kutanga usilazimishe kila mtu atange mtaani. It does not make sense kumlazimisha mtu awe muuza matunda au boda Kwa kigezo cha kujiajiri.
Ukiona kobe ameinama ujue anatunga sheria.Graduates hawataki kufanya hizo Kazi zenu za rat race maana zinaingilika kirahisi kwasababu Hakuna kigezo chochote kinachohitajika kufanya hizo Kazi mnazolazimisha watu wajiajiri.
Mfano, leo hii nikiamka asubuhi Nataka niwe Boda ntakutana na kizuizi kipi? It's just a wake up and do job , na mmejazana kama fungu za nyanya.
Kila mtu asimame na taaluma yake. Kama hauna taaluma endelea kuranda kama ng'ombe aliyepotea mnadani.
Nawasilisha.
Hivi karibuni humu kumekuwa na ongezeko kubwa la nyuzi(threads) zenye mlengo wa kuwadhalilisha wahitimu wa vyuo vikuu (graduates) na wanafunzi waliopo vyuoni kwamba ni useless na hawana uwezo wa kujitegemea kabisa.
Kwa utafiti nilioufanya, hii kampeni inaendeshwa kwa asilimia kubwa na watu ambao hawakubahatika kabisa kufika ngazi ya chuo kikuu ( Yaan Form Four Failures) na baadhi yao Ni walifika ngazi ya chuo kikuu lakini walitoka patupu. Maana siku zote asiyesoma ndo anayemsema aliyesoma. Huwezi mkuta aliyesoma anamsema asiyesoma.
Nadhani wahusika wa hii kampeni iwe kwa makusudi au bahati mbaya wanasahau kuwa lengo kubwa la elimu ni kutoa ujinga na kujaza maarifa ambayo yatamsaidia mlengwa kuendesha maisha ya kila siku.
Level ya chuo kikuu Ni tofauti na level za chini ambako unajiendea kama garii bovu. Ukishafika chuo kuna specialisation mfano mtu anaspecialize kwenye Mining Engineering, Pharmaceutical sciences au IT.
Na Lengo la Elimu hiyo Ni kumpa mtu maarifa ya kama Ni pharmacy akigraduate ajue jinsi ya kutumia hiyo pharmaceutical science aliyosomea kujikwamua kimaisha iwe kwa kuajiriwa au kujiajiri na Si vinginevyo.
Unaposema unataka kuona wahitimu wanaendesha bodaboda au wanakaanga chipsi unaondoa lile lengo la specialisation aliyoipata chuoni. Hapa unalazimisha tuwe na taifa la ovyo lisilo na wataalamu miaka kadhaa ijayo.
Kutangatanga kama kuku wa kienyeji ni Kwa aliyekosa hiyo specialization mostly wenye ajenda hii ovu , kama hukusoma mpaka kuspecialize kwenye kitu kimoja basi endelea kutanga usilazimishe kila mtu atange mtaani. It does not make sense kumlazimisha mtu awe muuza matunda au boda Kwa kigezo cha kujiajiri.
Ukiona kobe ameinama ujue anatunga sheria.Graduates hawataki kufanya hizo Kazi zenu za rat race maana zinaingilika kirahisi kwasababu Hakuna kigezo chochote kinachohitajika kufanya hizo Kazi mnazolazimisha watu wajiajiri.
Mfano, leo hii nikiamka asubuhi Nataka niwe Boda ntakutana na kizuizi kipi? It's just a wake up and do job , na mmejazana kama fungu za nyanya.
Kila mtu asimame na taaluma yake. Kama hauna taaluma endelea kuranda kama ng'ombe aliyepotea mnadani.
Nawasilisha.