Ni kweli tunahitaji mahakama ya Kadhi na kujiunga na OIC?

Mimi Muislam na nimeoa ndoa ya kiislamu kutapo tokea Muungu aipushe mbali mgogoro kati yetu
Ni lazima tuyamalize lishera kama uislam unavo sema sasa jee
Sheria ya ndia ya 1971 inatambua ndoa za kiislam kuhukumiwa kwa taratibu hizo ? Jawabu hapana upo ushahidi wa kesi nyingi kuamuliwa kufata mazingira ya ushahi na kuamuliwa kinyume chake
Sasa jee ni lazima kuwe na mahakama ya kadhi ? Mawazo yangu sio lazima ila tunaweza kubadilisha sheria ya ndoa na kuweka kipemgele cha kutambua ndoa za kiislam na kuweka sheria ya kuwa ndoa hizo zitahukumiwa na taratibu za kiislam
Na sheria hizo ndo ziwe juu ya sheria nyengine
Ni kama vile Customary law zinavotambuliwa kwa baadhi ya makabila
Hivo tunaweza kubadilisha tu sheria ya ndoa kukidhi haja hii ya waislam bla ya kuingiza gharama nyengine
Ama kuhusu kujiunga na OIC sio lazima hasa kwa Tanzania kuna upinzani kutoka upande wa pili
Hoja yao ni kuwa huu ni umoja nchi za kiislam na tanganyika sio nchi ya kiislam so sio lazima
Lakini hili linaweza likubaliwe katika katiba mpya kwamba ushirikiano wa nje usiwe ni jambo la muungano hivo Zanzibar ni nchi ya kiisllam
Kwa wingi wao wanaweza kujiunga


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

kwanza tuwekane sawa hapa...sheria za ndoa ziko wazi kabisa zinatambua ndoa za kiislamu,..pia hata inapofikia talaka kwenda mahakani ni tayari BAKWATA wameshafanya maamuzi ambayo yanatambulika kisheria hivyo mahakama inakamilisha tu mchakato,ukija ishu ya mirathi iko wazi pia kwamba mahakama lazima ifuate sheria za kiislamu kuhusu mgawo ambao upo kwenye Quaran takatifu,kwa maana hiyo hadi sasa hakuna mapungufu yanayofanya mwislamu akose haki zake
 
Ndg. 7Son.
Binafsi sijakuelewa vizuri, naomba unifahamishe haya mambo mawili tu:--
1- Mirathi, Talaka.....bado sheria za kiislam ndizo zinazo tumika. Are they in compliance with Holy QUR'AN? are the Judges, Magistrates ,Para-legals,competent enough within the doctrine?? Plz.articulate yr.mind don't rush.
2-Anae mlipa mpiga zumari ndie anae chagua wimbo,wanao Dai mahakama ya kadhi nao ni walipa kodi kama wengine, baadhiya Nchi nyingi zikiwemo majirani zetu wana mfumo huo.
WATANZANIA mbona tuna-deviate attention kwenye vitu vyepesi Social Issues badala ya kufikiria hali bora ya uchumi kwa wananchi wetu, let us focus on Ufisadi Magamba's etc...,

Kaka am very much sure kwamba zinacomply na Quaran takatifu,mirathi mgawanyo wake umechukuliwa huko kama alivyoelekeza Muhamed SW hivyo ishu inayobaki ni kwa judge au hakimu kuzifuata kama inavyotakiwa,labda niweke mambo sawa hapa kuna baadhi ya waislamu hawataki kuzitumia sheria hizo kwa sababu ni za kibaguzi lakini hiyo haiondoi uwepo wa sheria husika,Hii ishu kwa sasa ndo muhimu kuliko hao mafisadi maana at end itaanza kupandikiza chuki baana ya pande mbili,hivyo sisi kama watz kwa.ujumla wetu tuungane kuilinda amani yetu
 
Hili haliwezekani katika nchi ambayo serikali yake haina dini. Mahakama zetu zinajitosheleza.

Tumeshapigwa bao kwenye kura ya maoni waislam wamejitokeza kwa wingi kuliko wakristo mpaka sasa mahakama ya kadhi na OIC inaweza ikapitishwa.
 
OIC ni kwa ajili ya kusaidia social services just kama wakristo wanavyodai mou inadhaminiwa na Wajerumani, Isotope acha matusi mihemko,dhihaka na jazba kama mleta thread anavyotutaka!

kama MOU ni kwaajili ya wakristo kwanini OIC iwe ya watanzania wote na ambao sio waislmu
 
watu wa mahakama wanaweza kusaidia hapa. tunaomba kujua kesi ambazo hazikuamuliwa sawasawa ambazo zinaweza amuliwa sawasawa na mahakama ya kadhi. zipo? ni kiasi gani?, je, kukitokea mabadiliko ya hapa na pale kwenye hiz mahakama zetu bado kutakuwa na mapungufu ya ku-necessitate mahakama ya kadhi? subir wasukuma na wanyamwez wadai mahakama zao. maana wako wengi.
 
Kaka am very much sure kwamba zinacomply na Quaran takatifu,mirathi mgawanyo wake umechukuliwa huko kama alivyoelekeza Muhamed SW hivyo ishu inayobaki ni kwa judge au hakimu kuzifuata kama inavyotakiwa,labda niweke mambo sawa hapa kuna baadhi ya waislamu hawataki kuzitumia sheria hizo kwa sababu ni za kibaguzi lakini hiyo haiondoi uwepo wa sheria husika,Hii ishu kwa sasa ndo muhimu kuliko hao mafisadi maana at end itaanza kupandikiza chuki baana ya pande mbili,hivyo sisi kama watz kwa.ujumla wetu tuungane kuilinda amani yetu

Ndg. 7Son
Nikweli mirathi,na mgawanyo wa Mali zina-comply na Qur'an Takatifu lakini ni partial compliance, inahitaji uzamivu wa kufahamu na kutekeleza,ikizingatiwa kwamba hiyo ni fani ktk. taaluma ya sheria za Kiislam.
Ndugu yangu nikitowe shaka kuwa Mahkama hii ni kwa walio amini na si vinginevyo na hulazimishwi kuifuata.
Kuhusu kupanda mbegu ya Chuki, It's quite immaterial Wewe mbona baadhi ya ndugu zako ni Waislam nami baadhi ya ndugu zangu ni Wakristo, there's a coexistence,and life should go on. Let's address core issues for the betterment of our people.REMEMBER GOD WILL ASK YOU "WHAT DID U DO FOR THE BENEFIT OF MANKIND "
 
Usione majivu ukafiri moto umezimika. Taarifa za jikoni zinaonesha kuwa maoni ya katiba ni mikoa ya mwanza na mbeya tu watu wengi hawataki mahakama ya kadhi na OIC, kwingine kote wanaitaka. Hii lazima itaibua hisia za uchakachshida huko mbele.

acha uongo kwa takwimu za mabadiliko ya katiba mpya inaonesha kuwa kati ya mikoa ya kanda ya ziwa shinyanga ndio inaonesha kuwa wanahitaji mahakama ya kazi, takwimu zinaonesha kuwa kati ya aslimia zaidi 80 waliotoa maoni wanakubaliana na mahakama ya kazi.
 
Hili haliwezekani katika nchi ambayo serikali yake haina dini. Mahakama zetu zinajitosheleza.
Nchi yetu ina dini ...Huoni Krismass Ikifika Miti Ofisini ...mataa ....Kadi kutoka ofisi moja hadi nyengine..zote kwa gharama ya serikali
 
Ndugu zetu waislam wanatakiwa waelewe kuwa imani ya dini inamhusu mtu mwenyewe na isiathiri imani ya mtu mwingine hivyo kuanzisha mahakama ya kadhi kwa nchi isiyo ongozwa kwa misingi ya kidini ni uchokozi na chokochoko za kuharbu amani tuliyo nayo hivi sasa.
 
Usione majivu ukafiri moto umezimika. Taarifa za jikoni zinaonesha kuwa maoni ya katiba ni mikoa ya mwanza na mbeya tu watu wengi hawataki mahakama ya kadhi na OIC, kwingine kote wanaitaka. Hii lazima itaibua hisia za uchakachshida huko mbele.
hivi hizi mahakama ya kadhi na IOC zikiwepo zina athar yoyote katika nchi na kwa udhoefu hiz nchi ambazo zinazo kuna mgogoro wowote umejitokeza hadi iwe issue kwa hapa kwetu? mi naona wache wajiunge maadam sheria za nchi hazivurugwi ama kuingiliwa kwa namna yoyote vile.
 
Hii ni aibu kwa nchi tajiri kama yetu ambayo tuna kila kitu, halafu eti tunawaza kujiunga kwenye jumuia fulani kwa kigezo cha misaada! Du huu ni ujinga tunataka Mungu atupe nn? Akitupa hiyo OIC ndio utakuwa mwisho wa umasikini wetu? Hatukui tu? Tutaendelea kuwa watoto wa kunywa maziwa hata lini? Inatia hata kichefuchefu kwa habari hizi, eti iwekwe kwenye katiba hivi tuna akili kweli? Je nchi yetu ingekuwa kama Ethiopia tungefanyaje? Inauma viongozi wetu kila wazo tunakubali kwani sie madodoki?

mkuu naungana na wewe nakumbuka kuna mtu siku moja alikuja na thread akidai serikali ya tanzania kuna haja ya kujiunga na israel katika mahusiano ya kibalozi hata kwa sababu ni nchi iliyotukuka. yani kweli bado mawazo ya kudanganywa kifikra bado yapo kwa enzi hizi kweli jamani? ama kweli kazi ipo ya elimu kwa mtz.
 
OIC ni kwa ajili ya kusaidia social services just kama wakristo wanavyodai mou inadhaminiwa na Wajerumani, Isotope acha matusi mihemko,dhihaka na jazba kama mleta thread anavyotutaka!

kwani mmeshindwa kusaidiwa na hao waarab....ni mpaka mlazimishe nchi nzima ijiunge huko?

someni elimu dunia muweze kuona tofauti ya mambo sio mnajaribu kufananisha vitu ambavyo ni tofauti
 
Haina shida ili mradi mahakama hiyo isiendeshwe kwa kodi za wananchi wote na Kadhi pia asilipwe na serikali,kuwe na mfuko maaluum kama vile Islamic foundation nk zichangie kuendesha mfumo huo.,Na hata OIC sio shida ikiwepo kwani itawasaidia wote wale wanaoteseka mifumo mibovu ya riba kutoka mataifa ya magharibi.

ungeongezea na mahakama kuu/rufaa ya tanzania ndio ziwe na maamuzi ya mwisho nchi hii .... pia wale waislamu wasiotaka kuitumia wasilazimishwe kuitumia!!

OIC wakitaka kujiunga huko kama wao sawa, ila tusijiunge kama nchi!! serikali haina dini bali watu wake ndio wenye dini
 
Mimi Muislam na nimeoa ndoa ya kiislamu kutapo tokea Muungu aipushe mbali mgogoro kati yetu
Ni lazima tuyamalize lishera kama uislam unavo sema sasa jee
Sheria ya ndia ya 1971 inatambua ndoa za kiislam kuhukumiwa kwa taratibu hizo ? Jawabu hapana upo ushahidi wa kesi nyingi kuamuliwa kufata mazingira ya ushahi na kuamuliwa kinyume chake
Sasa jee ni lazima kuwe na mahakama ya kadhi ? Mawazo yangu sio lazima ila tunaweza kubadilisha sheria ya ndoa na kuweka kipemgele cha kutambua ndoa za kiislam na kuweka sheria ya kuwa ndoa hizo zitahukumiwa na taratibu za kiislam
Na sheria hizo ndo ziwe juu ya sheria nyengine
Ni kama vile Customary law zinavotambuliwa kwa baadhi ya makabila
Hivo tunaweza kubadilisha tu sheria ya ndoa kukidhi haja hii ya waislam bla ya kuingiza gharama nyengine
Ama kuhusu kujiunga na OIC sio lazima hasa kwa Tanzania kuna upinzani kutoka upande wa pili
Hoja yao ni kuwa huu ni umoja nchi za kiislam na tanganyika sio nchi ya kiislam so sio lazima
Lakini hili linaweza likubaliwe katika katiba mpya kwamba ushirikiano wa nje usiwe ni jambo la muungano hivo Zanzibar ni nchi ya kiisllam
Kwa wingi wao wanaweza kujiunga


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

huwezi kuwa na muungano halafu unaruhusu sehemu moja ya muungano ijihusishe na mambo ya nje.... hilo la zanzibar kujiunga na OIC haliwezekani bila kuvunja muungano

mkuu naomba nisaidie ..... hizo tofauti za sheria za mahakama zetu za JMT na taratibu za kiislam ni zipi? ....
 
Tumeshapigwa bao kwenye kura ya maoni waislam wamejitokeza kwa wingi kuliko wakristo mpaka sasa mahakama ya kadhi na OIC inaweza ikapitishwa.

haitapita .... chezea wafadhili wewee! .... tungekua tunajitosheleza kwa asilimia kubwa sawa, lakini kila siku bakuli ulaya na marekani unafikiri kuna chance ya hao jamaa kukubaliana na hiyo kitu?
 
Haina shida ili mradi mahakama hiyo isiendeshwe kwa kodi za wananchi wote na Kadhi pia asilipwe na serikali,kuwe na mfuko maaluum kama vile Islamic foundation nk zichangie kuendesha mfumo huo.,Na hata OIC sio shida ikiwepo kwani itawasaidia wote wale wanaoteseka mifumo mibovu ya riba kutoka mataifa ya magharibi.

labda zanzibar!
 
Ndg. 7Son
Nikweli mirathi,na mgawanyo wa Mali zina-comply na Qur'an Takatifu lakini ni partial compliance, inahitaji uzamivu wa kufahamu na kutekeleza,ikizingatiwa kwamba hiyo ni fani ktk. taaluma ya sheria za Kiislam.
Ndugu yangu nikitowe shaka kuwa Mahkama hii ni kwa walio amini na si vinginevyo na hulazimishwi kuifuata.
Kuhusu kupanda mbegu ya Chuki, It's quite immaterial Wewe mbona baadhi ya ndugu zako ni Waislam nami baadhi ya ndugu zangu ni Wakristo, there's a coexistence,and life should go on. Let's address core issues for the betterment of our people.REMEMBER GOD WILL ASK YOU "WHAT DID U DO FOR THE BENEFIT OF MANKIND "

nina swali dogo hapa .... kwenye hiyo mirathi, kama mjane ni mkristo.....sheria ya kiislam inasemaje?..... na kwenye talaka kama mmoja ni mkristo. sheria inasemaje pia hasa kama hao wakristo au waislamu hawataki kuhusishwa na hizo mahakama za kadhi?
 
hivi hizi mahakama ya kadhi na IOC zikiwepo zina athar yoyote katika nchi na kwa udhoefu hiz nchi ambazo zinazo kuna mgogoro wowote umejitokeza hadi iwe issue kwa hapa kwetu? mi naona wache wajiunge maadam sheria za nchi hazivurugwi ama kuingiliwa kwa namna yoyote vile.

umeanza vizuri, umemaliza vibaya mkuu ...... waulize watu na kupata references za kutosha

OIC na mahakama za kadhi zitaingilia sheria na katiba ya nchi .....
 
Tumeshapigwa bao kwenye kura ya maoni waislam wamejitokeza kwa wingi kuliko wakristo mpaka sasa mahakama ya kadhi na OIC inaweza ikapitishwa.
nakubaliana na wewe kabisa hapa Jaji Warioba keshapigwa bao hii tume imemzunguka na nakumbuka Edwin Mtei Muasisi wa CHADEMA alisema Tume ya Katiba imejaa Waislamu watu wakambeza sasa matokea yanaanza kuonekana Eti Mbeya na Morogoro ndio wanaokataa mahakama ya Kadhi Mikoa mingine imekubali
Yaleyale ya Misri na Brotherhood
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom