Ni Kweli Sera za CCM zimeshindwa?

Embu tuangalie sera yao ya elimu kwa mfano. Kwa miaka ishirini iiliyopita wamekuja na kila mpango wa kuinua elimu na kuboresha sekta ya elimu. Wakiongozwa na MKUKUTA na mipango meingine ya MMEM n.k tulitarajia kuwa elimu yetu ingekuwa bora zaidi. Je, tunaweza kusema kuwa mipango yetu mingi ya kuinua elimu ambayo imekunywa fedha nyingi sana za umma imefanikiwa kuboresha elimu ya TAnzania hasa ukizingatia mfano wa juzi tu ambapo nusu ya wanafunzi waliofanya mtihani wa sekondari nchini wamefeli?
 
Ni vizuri tungejua yafuatayo kabla ya kujadili kwamba sera zimeshindwa au zimeshinda

a. Tulitegemea nini au tuwe wapi kwenye sector ipi? in the first place

b. Kwa wakati gani au time period ipi tufikie wapi na kivipi

c. Tuko wapi, tumeshindwa kiasi gani na kwanini?

Kusema tu sera zimeshindwa bila kufahamu tulikuwa na malengo gani na tumefikia kiasi gani ni -generalize na kuleta emotional and sensational useless infomation..

sera ipi imefeli??? na ulitegemea tungekuwa wapi kwa muda gani??
 
Ni vizuri tungejua yafuatayo kabla ya kujadili kwamba sera zimeshindwa au zimeshinda

a. Tulitegemea nini au tuwe wapi kwenye sector ipi? in the first place

b. Kwa wakati gani au time period ipi tufikie wapi na kivipi

c. Tuko wapi, tumeshindwa kiasi gani na kwanini?

Kusema tu sera zimeshindwa bila kufahamu tulikuwa na malengo gani na tumefikia kiasi gani ni -generalize na kuleta emotional and sensational useless infomation..

sera ipi imefeli??? na ulitegemea tungekuwa wapi kwa muda gani??

Sera yao mojawapo ni ile iliyozaa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi kati ya 2007-2017 (nimebandika kwenye mada nyingine). Mpango ule ulitaka ifikapo mwaka 2012 afya ya msingi (primary healthcare) iwe imemfikia kila Mtanzania na miaka mitano ya mwisho 20121-2017 iwe ni ya kuconsolidate gains zilizofikiwa. Je, afya msingi imewafikia Watanzania wote?
 
Embu tuangalie sera yao ya elimu kwa mfano. Kwa miaka ishirini iiliyopita wamekuja na kila mpango wa kuinua elimu na kuboresha sekta ya elimu. Wakiongozwa na MKUKUTA na mipango meingine ya MMEM n.k tulitarajia kuwa elimu yetu ingekuwa bora zaidi. Je, tunaweza kusema kuwa mipango yetu mingi ya kuinua elimu ambayo imekunywa fedha nyingi sana za umma imefanikiwa kuboresha elimu ya TAnzania hasa ukizingatia mfano wa juzi tu ambapo nusu ya wanafunzi waliofanya mtihani wa sekondari nchini wamefeli?

Elimu kuna shida kuu tatu,

a. Hatujaamua ni lugha ipi ya kufundishia standard kwa wanafunzi wa Tanzania; kumekuwa na mchanganyiko usio rasmi ambao uanaleta confusion kwenye flow of knowlege; mwanafunzi anaanza na kilugha (kabila lake)-Kiswahili-English; anaishia kutojua zote..

b. Tumeweka resources nyingi kwenye majengo (siyo mbaya lakini it has to change now) ipelekwe kwa human capital

c. Hakuna consistency kwenye authorities (to many educational authorities ambao hawana link) mfano; VETA, NECTA, NACTE, TCU ni mchanganyiko usioeleweka na usio na manufaa kwa wanafunzi hata soko la ajira, ni gharama za bure kwa serikali
 
Tumeona mengi kuanzia kwenye nishati, madini, maji na kilimo. Na wiki hii tumeshuhudia makubwa zaidi katika afya na elimu ambapo kumomonyoka kwa sekta hizo kunadhihirishwa zaidi. Je ni hak kusema kuwa sera za chama tawala kwa kweli zimeshindwa?

Mkuu hapo upo perfect 100% kwani inajidhihirisha wazi wazi
 
Sera yao mojawapo ni ile iliyozaa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi kati ya 2007-2017 (nimebandika kwenye mada nyingine). Mpango ule ulitaka ifikapo mwaka 2012 afya ya msingi (primary healthcare) iwe imemfikia kila Mtanzania na miaka mitano ya mwisho 20121-2017 iwe ni ya kuconsolidate gains zilizofikiwa. Je, afya msingi imewafikia Watanzania wote?

Wewe unaonaje au una information ya hali ikoje hadi sasa? tumeshindwa kufikia kwa kiasi gani?
 
CCM wamefanikiwa kwenye sera ya ubinafsishaji ambayo ndio chanzo cha ufisadi pamoja na sera ya kuwalinda mafisadi
 
Elimu kuna shida kuu tatu,

a. Hatujaamua ni lugha ipi ya kufundishia standard kwa wanafunzi wa Tanzania; kumekuwa na mchanganyiko usio rasmi ambao uanaleta confusion kwenye flow of knowlege; mwanafunzi anaanza na kilugha (kabila lake)-Kiswahili-English; anaishia kutojua zote..

b. Tumeweka resources nyingi kwenye majengo (siyo mbaya lakini it has to change now) ipelekwe kwa human capital

c. Hakuna consistency kwenye authorities (to many educational authorities ambao hawana link) mfano; VETA, NECTA, NACTE, TCU ni mchanganyiko usioeleweka na usio na manufaa kwa wanafunzi hata soko la ajira, ni gharama za bure kwa serikali

Hayo unayoyasema ndio sehemu tu ya utekelezaji wa sera zenyewe ( au kutotekelezeka - kutegemea na unaangalia kutoka upande gani).
 
Wewe unaonaje au una information ya hali ikoje hadi sasa? tumeshindwa kufikia kwa kiasi gani?




well ndio maana ya hili swali hapa.. tushirikishane.. Kwa mfano, sera yao ya nishati imekuwa na malengo ya muda mrefu ya kuondoa tatizo la upungufu wa nishati ya umeme hata mwaka jana waliahidi kuwa sehemu kubwa uya tatizo ingekuwa imetatuliwa mwishoni mwa Disemba lakini ni kwa kiasi gani tumefikia lengo letu?
 
Hayo unayoyasema ndio sehemu tu ya utekelezaji wa sera zenyewe ( au kutotekelezeka - kutegemea na unaangalia kutoka upande gani).

Ni ngumu sana kuvunja taasisi ukishaanzishwa (resitance within) ndio kosa kubwa walilofanya ni kukubali kuwa na educational authority nyingi; ambazo pamoja na kuwa gharama zimekuwa na mtazamo tofauti kuhusu elimu na hatimaye utekelezaji mgumu...
 
Mzee Mwanakijiji,
Hii kitu inaitwa CCM ilishashindwa kitambo, hakuna cha sera wala ilani, na wananikera sana kujidai kila kitu kipo kwenye mpango wao wanaposhauriwa lakini huwaoni kutekeleza.
Nachukizwa zaidi na watu wanavyoonyesha kuelewa tatizo la CCM lakini ikifika wakati wa kutumia haki yao ya msingi wanafanya makosa hayohayo. Kwanini sisi watu tunaojua hatuwaelimishi na wenzetu? We are fed up, we need changes.
 
Sera zinaposimama kwenye misingi hafifu ya utekelezaji sio sera tena bali ni mawazo duni yaliyoshindwa kuleta mabadiliko yenye tija.
Chama tawala kinachanganya mambo mawili kwenye mfumo wake wa kuendesha nchi:
1.Ilani ya chama cha mapinduzi(sehemu kubwa ikiwa siasa yenye nguvu bila misingi ya utekelezaji).
2.Sera za kuendeleza nchi(mambo ya kitaaluma ambayo yanahitaji jitihada za makusudi ili kufanikisha utekelezaji wake)
Ningependa kutoa mfano:
Nilipata nafasi ya kushiriki kwa kiwango kidogo kwenye kuunda mpango mkakati wa kuendeleza sekta moja muhimu nchini.Baada ya kukusanya maoni ya wadau kwa ujumla kukawa na kikao cha wadau teule ili kuchambua sehemu muhimu za kuziwekea mkazo na kufanya masahihisho kwenye inception document ili kutengeneza first draft ya huo mpango mkakati.Tukaiomba wizara husika ituletee watendaji makini wanaoijua sekta ili kutoa mpango ambao umeshiba.Kwa mshangao wangu wakatuletea watu waliokuja wamebeba ilani ya CCM na kutaka hiyo ndiyo iongoze mjadala ya kutengeneza mpango mkakati.Haya ndiyo mambo yanayorudisha nyuma taifa hili.

Kwa maneno mengine ni kuwa wanaotaarisha ILANI YA CCM si wataalamu, na huandikwa na watu wasio na uelewa na mambo?
 
...hawa CCM wako hatua ya pili kutoka mwisho. Na itakapofika mwisho, ndipo Watanzania wengi tutakapoungana na kuimba: viva CHADEMA viva,viva NGUVU YA UMMA viva. Naisubiri sana hiyo siku inikute nikiwa bado niko hai!!
 
Kwa maneno mengine ni kuwa wanaotaarisha ILANI YA CCM si wataalamu, na huandikwa na watu wasio na uelewa na mambo?

Haswa!!Ilani inapaswa kuandikwa kitaalamu huku ikiwa synchronized kwa kiasi fulani taswira ya mikakati ya kuleta maendeleo na sio kulenga iwe tiketi ya kushinda uchaguzi tu.
 
...hawa CCM wako hatua ya pili kutoka mwisho. Na itakapofika mwisho, ndipo Watanzania wengi tutakapoungana na kuimba: viva CHADEMA viva,viva NGUVU YA UMMA viva. Naisubiri sana hiyo siku inikute nikiwa bado niko hai!!

Mkuu hiyo iko njiani na ushindi umeshaanza kuonekana. CCM tayari imeshapoteza dira haina tena sera kuleta maendeleo.
 
"Kwa sasa uti wa mgongo wa nchi hii ni rushwa, sio kilimo...Karibia kila mtu nchi hii anaishi kwa rushwa. Wanaodai uti wa mgongo wa taifa hili ni kilimo wanadanganya watanzania. Shughuli pekee kwa sasa ambayo karibia kila mtanzania anajihusisha nayo ni kupokea,kutoa rushwa au kuathiriwa na rushwa kwa njia moja ama nyingine" - Yahoo! Groups

Well said.
 
Well said.

Heri unayejua ccm kinasera, kwa uelewa wangu mdogo sera za ccm zilikoma miaka ya 1980's.BAADA YA HAPO NI 'LIPUALIPUA BORA LIENDE' kama taasisi kama TAKUKURU ZINGEFANYA KAZI KWA KUMUOGOPA MUNGU SEHEMU ZOTE TZ,CCM INGEBAKI HISTORIA KITAMBO.FIKA LUSHOTO UONE VIOJA VYA RUSHWA,UFISADI NA ULAFI.NAKUPONGEZA MCHOKOZI WA THREAD HII
 
Ningependa kweli kusikia majibu ya wapinzani kwenye swali hili ni nini hasa. Nina hofu kuwa wapo ambao wanaamini kabisa kuwa sera za CCM zimekosa tu watekelezaji kuwa wakipatikana watekelezaji basi sera hizi (nzuri kitabuni kama watu wanavyopenda kusema) zinaweza kufanikiwa. Je ni kweli?
 
Sera za CCM zimefanikiwa sana tena saaaaana Mzee MM hasa kwenye nyanja za Wizi, ubadhilifu wa Mali ya Umma, kulindana, wizi wa KURA, ushkaji na kutokuwa na uchungu na nchi hii. CCM ni chama cha wezi na sera yao kubwa ni kupora utajiri wa nchi hii, wenyewe mmesikia bungeni huko
 
Back
Top Bottom