Ni kweli kwamba kurasa za Ilani ya CCM zimeisha Zanzibar? Kwamba kila kilichoandikwa kimetekelezwa?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
876
4,101
Kauli inayotrend huko Zanzibar ni KURASA ZA ILANI YA CCM ZIMEKWISHA; hii inamaanisha kwamba kazi aliyokabidhiwa mzee Mwinyi amemaliza anasubiri kupewa majukumu mengine .

Lakini najiuliza nini kilichoandikwa kwenye hizo kurasa ambacho kimetekelezwa 100%, je barabara zimejengwa zote? Hapana, ukiende Pemba barabara alizojenga Shain chache ndo zipo hakuna mpya. Kwamba skuli zimekamilika na zina waalimu na vifaa? Hapana, skuli zina hali mbaya maeneo mengi. Kwamba, maslahi ya wafanyakazi yameboreshwa? Hapana, bado kila siku wanalilia maslahi ikiwemo nyumba za makazi. Kwamba Afya imeboreshwa? Hapana, kila siku wagonjwa wanaletwa Muhimbili na hakuna rufaa ya Muhimbili to Zanzibar

Nadhani hizi kauli hazina ukweli ila zimelenga kuonyesha kisiasa mambo ni bam BAM ila kiuhalisia big No
 
Waongo hao waliahidi meli kubwa 5 za uvuvi bahari ya hindi na kwamba zingeajiri watu elfu 40 ila hamna hata moja imeletwa.
 
Back
Top Bottom