Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

See God now!!!!

Mungu anatutoa mbali, anatupeleka mbali....Glory to the Most high alone.

As long as your happy,I'm happy and GOD is Happy..
Enjoy life My friend Humble..Wewe ni mtu poa sana.... Na unastahili kila kilicho chema kwenye hii Dunia...

NB,Usiwe unapotea namna hii hapa jukwaani..Wewe una vitu vyako special sana sana...Hatuvipati popote hapa...Amini kwamba.
Absolutely true! Mungu huwa hachelewi anakuja kwa wakati sahihi tu. Nashukuru Mungu kilikuwa kipindi kifupi kigumu saana lakini nilijifunza mengi saana.

Kwa vile nilikuwa na pesa awali hata kuomba msaada nilishindwa maana nilikuwa nawaza watu watanicheka na Mama yangu hakuwahi kujua maana nilijua nitampa mawazo tu kumwambia whole situation. So I fought this battle all alone.

Triumphantly, nilipita Salama lile bonde la dhiki kuu. Usiombe kukosa pesa wakati awali ulikuwa nazo unaweza kuwa mwehu maana unaona aibu kufanya kazi mbovu sababu ulikuwa nazo mwanzoni.

Mungu ni mwema, nimerudi barabarani na technically wewe ni miongoni mwa marafiki zangu wa hapa JF I wish hata siku moja tuonane tu.
 
Absolutely true! Mungu huwa hachelewi anakuja kwa wakati sahihi tu. Nashukuru Mungu kilikuwa kipindi kifupi kigumu saana lakini nilijifunza mengi saana.

Kwa vile nilikuwa na pesa awali hata kuomba msaada nilishindwa maana nilikuwa nawaza watu watanicheka na Mama yangu hakuwahi kujua maana nilijua nitampa mawazo tu kumwambia whole situation. So I fought this battle all alone.

Triumphantly, nilipita Salama lile bonde la dhiki kuu. Usiombe kukosa pesa wakati awali ulikuwa nazo unaweza kuwa mwehu maana unaona aibu kufanya kazi mbovu sababu ulikuwa nazo mwanzoni.

Mungu ni mwema, nimerudi barabarani na technically wewe ni miongoni mwa marafiki zangu wa hapa JF I wish hata siku moja tuonane tu.

Mungu ni mwema sana sana Humble...Nafurahi kuona ulipita katika lile bonde la uvuli wa mauti salama

Sasa ni nini? Ukiwa mjini nichek tu Rafiki yangu..Nipo available napambana...

Karibu.
 
Umenikumbusha mbali, nilikopa godoro nikailaza chini sikuwa na kitanda akaniongezea na stuli ya kukalia halafu nikaoa siku 15 mbele wakati wa jion wife anasonga ugali jamaa anapiga hodi karibu mara paap nataka pesa ya godoro na ya stuli mbele ya wife daah nikamuomba aniongezee siku 15 inafika asubuhi napiga mswaki kurudi ndani nikakuta wife kabeba vitu vyake kampelekea daah
Wanawake hawajifikiriagi mara mbili hao watu sijui waliongea nini na shetani, swala la tunda nadhani lilikua topic ya mwisho kabisa
 
Nimesoma hii Comment yako machozi yamenilenga

Iko hivi Mkuu...Kuna watu ni Daraja,Baraka katika maisha ya watu wengine....Hata wewe pia...

Hujawahi kuona unaweza kuwa kwenye changamoto fulani halafu Mungu anamleta mtu wewe mwenyewe huelewi..Then huyo mtu atakusaidia kwenye hiyo changamoto.. ukivuka hapo anaondoka na siyo mmegombana... ni ukaribu tu unapungua..Maana yake ni nini? Kazi yake ameimaliza...Anatakiwa akafanye kingine kwa wengine na wengine tena...Hawa watu wanaitwa "Destiny Helper"
Kweli kabisa ndugu.
 
Ili kuimarika kuna mapitio mengine ni muhimu kuyapitia ili yawe ukumbusho wa kukosa pale ukipata.

Ila kiukweli kabisa hakuna faraja kwenye ufukara.

Nakumbuka kuna kipindi nilipigika ikawa natembelea washkaji mida ya misosi kiasi cha kujua ratiba ya mlo wa masela wote.

Kuna msela wangu (Mungu amlaze mahala pema) ilikuwa ikifika jioni ananipigia simu kuniita tukapige story, kumbe alishajua hali yangu na ule wito ulikuwa ni msaada indirectly maana alihakikisha nakula ndio naondoka.

Na kila nikiondoka mkewe ananipa kikontena cha msosi ananiambia shem naona chakula cha leo umekipenda beba na hiki utakula baadae.

Hawakujua jinsi gani walikuwa wakinisevu.
Mungu amlaze mahala pema Hakika Alikuwa mwenye Utu Sana, Kama huyo mkewe yupo usiache kumtembelea
 
Wanawake hawajifikiriagi mara mbili hao watu sijui waliongea nini na shetani, swala la tunda nadhani lilikua topic ya mwisho kabisa
Kuna vitu vinafanyika ili kutimiza unabii, sasa kwa vile haikusemwa tuwalaumu wanawake kwa kosa la pale Eden au tuwachukie wanawake basi inawezekana ni unabii ulitimizwa, Sasa tunakiwa twende na kauli mbiu yetu ya kufanya kazi kwa jasho ili tupate riziki.
 
Mungu amlaze mahala pema Hakika Alikuwa mwenye Utu Sana, Kama huyo mkewe yupo usiache kumtembelea
Unajua shida nyingi zinatupata wanadamu hasa Afrika kwa kuyakataa maarifa, imagine tumeambiwa tusaidiane sisi kwa sisi lakini watu hata yule anayejua huyu anashida kweli nimsaidie yeye anakwepa, na waliofanya sisi tuharibikiwe tunyimane misaada ni wale waliotumia misaada ya wenzao vibaya mfano kubweteka tu unaposaidiwa au kuomba na vya ziada bila kupewa hawa watu wabaya wanatakiwa waundiwe kikao Cha kukemewa kila pande za nchi.
 
Unajua shida nyingi zinatupata wanadamu hasa Afrika kwa kuyakataa maarifa, imagine tumeambiwa tusaidiane sisi kwa sisi lakini watu hata yule anayejua huyu anashida kweli nimsaidie yeye anakwepa, na waliofanya sisi tuharibikiwe tunyimane misaada ni wale waliotumia misaada ya wenzao vibaya mfano kubweteka tu unaposaidiwa au kuomba na vya ziada bila kupewa hawa watu wabaya wanatakiwa waundiwe kikao Cha kukemewa kila pande za nchi.
Hakika Mkuu
 
Kufulia wanakuita kwa kimombo "Broke", kwa kinaijeria "sapaa", kusikiage tu!

Nakumbuka niliwahi kuwa na bajeti ya 200 kwa siku, nakula mhogo wa kuchemsha imeisha hio hadi kesho, pesa ikakata nikawa nafunga safari natembea lisaa ni nje ya mji kidogo naenda kukwea miti ya mapera, nakula na huo ndo unakuwa mlo wangu wa siku nzima. (shughuli ya uwani haikuwa ndogo)

Nilikuwa napenda sana mambo ya simu na niliweza kuzichambua vizuri kwenye camera, ram, ubora, chaji, n.k, hii ilifanya watu wawe wanakuja kuniomba ushauri kununua simu ipi kwa bajeti waliyonayo ila mimi nilikuwa na kitochi kimechoka.

Nilianza kuhesabu majina kwa simu huku nikisema nani anaweza kuniazima bila kuanza kunipa darasa la maisha ama kunitangaza.

Sendo yangu ilikatika upande moja nikawa naipiga msumali ijishike, baada ya siku 3 inaachia napigilia tena, ilijaa matundu kibao.

Nilikuwa natoa nguo zote kwenye tenga na kuanza kusachi moja moja kama ina hela naambulia patupu, kesho narudia nazikunguta kwa nguvu, lakini wapi.
Sitasahau nilivyoanza kukopa hela kwenye applications za mikopo nilizokuwa nazidharau nikiona matangazo yangu Facebook. Sasa picha linaanza kuna siku nataka kukopa TENI kwenye Moja ya application za MIKOPO wakaomba picha yangu ya kuscan nilikuwa bar then nakimbia toilet kupiga picha kwa Siri ghafla umeme ukakata daah ilikuwa noma sana wakuu. Chanzo Cha yote hayo ni kupitia ugumu wa kuichumi usiombe yakukute
 
Nimesoma comments zoote
Kwa hakika maisha ni tough
Neno moja lisikauke kinywani ni AHSANTE MUNGU
binafsi sikuwahi kupitia maisha magumu hata kidogo
Kwetu tupo 6
Ila mshua alipambana kadri ya alivyoweza kuweka mambo level nyumbani
Leo wa tatu kati ya sisi sita tunaweza kusema tunajitegemea

Wazazi wanapambana sana sana Sanaa kujenga tabasamu kwetu
Thus mama au mzee wanapotaka chochote hua sisiti kutoa pesa
 
Back
Top Bottom