voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
- Thread starter
- #61
Na umethibitisha kwamba huijui Ngorongoro inayoongelewa hapa.Wewe ni mjinga kama Kitenge. Toka lini Ngorongoro inapata mvua kidogo mwaka mzima? Ngorongoro ni ukanda wa juu unaopata mvua sawia kila mwaka. Tena mvua nyingi kuliko sehemu nyingi nchini.
Hatua ya kwanza iwe ya kuivunja hiyo NCAA mnayoitumia kujitajirisha kwa kufisadi na kujilipa posho kubwa kubwa.
Eneo likabidhiwa kwa TANAPA ili iwe national park. Utalii wa utamaduni umekwisha. Eneo la NCA liwe mbuga ya Taifa chini ya Tanapa kama ilivyo Serengeti, Tarangire au lake Manyara.
Wewe mjanja unafikiria....
Ngorongoro(Highlands).
Maeneo yanayojumuisha, ukanda wa mlima lemagurut, kakesio na kuzunguka Ngorongoro crater kwenye msitu wa tropical.
Mimi mjinga ninaiongelea......
Ngorongoro (Lowlands).
Bonde la olduvai kwenda mpaka Malambo,Naiyobi, Lake Natron na ukanda wa Oldoinyo Lengai.
Hizo ni kanda mbili tofauti na uelewa wako mdogo
Midimay.
Kiwango cha mvua kinachopatikana Olduvai na Ukanda huo mpaka Malambo ni cha chini zaidi.
Kulinganisha na maeneo ya Makao,Kimba,Ole misgiyo,Ole kepusi,Nainokanoka, Olmoti na Empakai.
Na ndio sababu huwa siku zote mgogoro uko kwenye kuzuia wafugaji kuja kuchungia ng'ombe zao kwenye huo ukanda wa msitu kuizunguka Crater.
Sababu pana uoto mzuri na vyanzo vikuu vya maji.
Vyanzo vya maji ya Ngorongoro ni msingi wa uhai na matumizi ya ukanda mzima wa Ngorongoro,Karatu,Lake eyasi.
Pamoja na kuwa chanzo kikuu cha Underground water forest ya uoto wa hifadhi ya ziwa
#Manyara.
Hatukurupuki kuandika humu bali tunaandika kile tulichokiishi na kukifanyia kazi.
Karibu sana Midimay