Natasha Ismail
JF-Expert Member
- Jul 14, 2008
- 747
- 640
Wakulungwa tunaelewa mbona.kwa mtazamo wangu, pamoja na yote, hapo (kwenye nyekundu) ndipo ilipo hoja kuu ya mtoa mada......nikitumia maarifa ya o'level ya uchambuzi wa kazi za kifasihi naona kabisa mtoa mada anasumbuliwa na aina ya maisha iliyopo sasa kwa vijana wetu;
mifumo ya maisha imebadilika badilika, imevurugwa vurugwa! hakuna ukakamavu wala kugangamala....vijana wamekuwa lainiiiiii, wanashindana na dada zao kutembea na vioo vya kujirembea kwenye vipochi na hatimae ushoga umetapakaa.....wajanja wa siku hizi ni wale wanaoweza kucheza video games vizuri au kuyaelezea mavazi ya kina diamonds vizuri, lakini si wale tena wanaofanya, angalau, mambo ya kishujaa.
watoto wa kiume sasa wanalindwa kama wanavyolindwa watoto wa kike maana ukishangaa tu utakuta wameraruliwa malinda, hawawezi hata kujitetea.....wako lainiiiiii. kijana wa kidato cha nne anagoma kwenda shule eti kisa mama yake hajamtumia hela ya kutumia shuleni.
kijana wa kidato cha nne anaomba ruhusa shule aende kwa mama yake ili akamshonee suruali yake iliyotatuka kidogo mapajani.
mnaokejeli uzi huu mmenishangaza sana!
ahsante sana mtoa mada, umenitafakarisha sana kuhusu yajayo ya vijana wetu hawa!!