Ngara: Taarifa ya Kupokea Mamilioni ya Fedha Kutoka kwa Rais Samia Kwenda Jimbo la Ngara

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,902
945
Mbunge wa Jimbo la Ngara Mhe. NDAISABA GEORGE RUHORO anapenda kuwajulisha wananchi wote wa Jimbo la Ngara kuwa kazi yake ya uwakilishi inaendelea kulipa baada ya kushiriki kuipitisha Bajeti ya Serikali sambamba na kufuatilia fedha za kujenga miundombinu mbalimbali ndani ya Jimbo la Ngara.

Taarifa njema ni kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ametuma TZS 1,926,600,000.00 kwa ajili ya matumizi yafuatayo;

1. TZS 600,000,000.00 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba, Madawa na vitendanishi kwenye vituo vya Afya na zahanati.

2. TZS 1,125,000,000.00 -Ujenzi wa Madarasa MAPYA 45 KWENYE SHULE TAKRIBANI ZOTE ZA SEKONDARI zilizopo wilayani Ngara.
3. TZS 201,600,000.00 - Ujenzi wa Matundu 96 ya vyoo kwenye shule za sekondari.

Fedha hizi zimekwishafika Ngara hivyo Mhe. Ruhoro anaendelea kuwapongeza Mkuu wa Wilaya ya Ngara Kanali MATHIAS KAHABI na Ndugu SOLOMON KIMILIKE - Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara pamoja na Madiwani wote chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mhe. Willbard Bambala kwa kuzipokea fedha hizi, kuzigawa na kuanza kusimamia utekelezaji wa miradi hii maramoja.

Utoaji wa taarifa hii ni mwendelezo wa utekelezaji wa ahadi ya Mbunge RUHORO ya kutoa taarifa kwa umma ili kuushirikisha juu ya maendeleo na kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa mama yetu kipenzi cha Watanzania na Wanangara DKT SAMIA SULUHU HASSAN.

Orordha ya Mgawanyo wa fedha ni kama ilivyo ambatanishwa hapa chini.

Sarah Kenneth
Kaimu Katibu wa Mbunge

WhatsApp Image 2024-01-15 at 20.03.44.jpeg
 
Uwazi na ukweli katika shughuli za umma.

Ila acha kulazimisha wananchi waweke picha yako katika maofisi yao.

Mfalme ni mmoja tu, ukishindana naye, atakubomoa
 
Back
Top Bottom