Ndugu Zangu,
Kusoma ni burudani pia. Wikiendi hii nasoma kitabu hicho pichani, Gamba La Nyoka, mwandishi ni Euphrase Kezilahabi. Kumbe, hata miaka hiyo kuna walioliona na kulijadili gamba la nyoka!
Ni kitabu kinachokurudisha msomaji nyuma kwenye historia. Unakiona kijiji ambamo wanakijiji wake wamekumbwa na mkanganyiko wa njia ipi ya kuifuata.
Wakiongozwa na mwenyekiti wao wanabaini hila na ghilba za viongozi wa Serikali, na Chama pia. Wanaamua kufanya mkutano wa siri kujadili mustabakali wao. Wamehakikisha, kuwa mkutano utafanyikia katikati ya pori, na kuwa vijibwa vya Serikali wakiwa na maana ya polisi wasijue chochote.
Swali, ni hili, yawezekana jambo hilo likawa siri hata wakifanyia mkutano porini?
Na hapa nanukuu maneno yaMwenyekiti wao wa kijiji anayesema haya wakiwa kwenye mkutano wa siri katikati ya pori;
Ndugu zangu Wanakijiji. Kama miti inatoa sauti itingishwapo na upepo, na majani hutoa milio wakati wa upepo mkali, hapana shaka, jambo tutakalolijadili hapa litakuja julikana. (CCJ, Nape, Mwakyembe, Mpendazoe na Sitta?!)
Mwenyekiti anaendelea kusema; " Ndugu zangu, mwanadamu hana wema. Usimwone kucheka. Akacheka akakusalimu na mdomoni kuitika. Japo kweli maneno yake matamu lakini ndani ni nyoka, ana sumu kali. Na heri sumu ya nyoka maana inaweza kutibiwa. Sumu ya binadamu haitibiki.
Wengine kati yetu wana tamaa, na tamaa huzaa sumu. Anasema Mwenyekiti wa Kijiji.
Ndugu zangu wanakijiji wenzangu wa mjengwablog, ngojeni Mwenyekiti wenu niendelee na uhondo wa kitabuni.
Wikiendi Njema.
Maggid
Iringa,
Ijumaa, Mei 20, 2011.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo
Kusoma ni burudani pia. Wikiendi hii nasoma kitabu hicho pichani, Gamba La Nyoka, mwandishi ni Euphrase Kezilahabi. Kumbe, hata miaka hiyo kuna walioliona na kulijadili gamba la nyoka!
Ni kitabu kinachokurudisha msomaji nyuma kwenye historia. Unakiona kijiji ambamo wanakijiji wake wamekumbwa na mkanganyiko wa njia ipi ya kuifuata.
Wakiongozwa na mwenyekiti wao wanabaini hila na ghilba za viongozi wa Serikali, na Chama pia. Wanaamua kufanya mkutano wa siri kujadili mustabakali wao. Wamehakikisha, kuwa mkutano utafanyikia katikati ya pori, na kuwa vijibwa vya Serikali wakiwa na maana ya polisi wasijue chochote.
Swali, ni hili, yawezekana jambo hilo likawa siri hata wakifanyia mkutano porini?
Na hapa nanukuu maneno yaMwenyekiti wao wa kijiji anayesema haya wakiwa kwenye mkutano wa siri katikati ya pori;
Ndugu zangu Wanakijiji. Kama miti inatoa sauti itingishwapo na upepo, na majani hutoa milio wakati wa upepo mkali, hapana shaka, jambo tutakalolijadili hapa litakuja julikana. (CCJ, Nape, Mwakyembe, Mpendazoe na Sitta?!)
Mwenyekiti anaendelea kusema; " Ndugu zangu, mwanadamu hana wema. Usimwone kucheka. Akacheka akakusalimu na mdomoni kuitika. Japo kweli maneno yake matamu lakini ndani ni nyoka, ana sumu kali. Na heri sumu ya nyoka maana inaweza kutibiwa. Sumu ya binadamu haitibiki.
Wengine kati yetu wana tamaa, na tamaa huzaa sumu. Anasema Mwenyekiti wa Kijiji.
Ndugu zangu wanakijiji wenzangu wa mjengwablog, ngojeni Mwenyekiti wenu niendelee na uhondo wa kitabuni.
Wikiendi Njema.
Maggid
Iringa,
Ijumaa, Mei 20, 2011.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo