Neno La Leo: Ng'ombe Kipofu Na Ng'ombe Aliyevunjika Mguu!

Anachokosea ni kujaribu kumuiga Jenerali

Kumuiga Jenerali? Thubutu yake!

Nakumbuka Ngurumo alijibu makala moja ya Maggid akisema: Anachoandika huyu bwana ni msimamo wake na wala hasukumwi na ushawishi wa mtu yoyote. Inawezekana.

Ila hiyo haisemi kwamba huwa hasukumwi na chuki kwa watu au vitu fulani fulani. And hatred surely compromises intellectual thinking.
 
Majidi,
Mimi ningependa kujuza yafuatayo:
Pamoja na kuzunguka kwako kote lakini bado unaonyesha kuwa bado ungali unatetea walioko madarakani kutokana na mifano yako ya Ng'ombe,Kuku na Mfalme aliyeishi kunako kweusi.....kwako wewe ni kuwa bila watawala tuilo nao hatutaenda....na kuwa mwingineyo yeyote yule si mali kitu.....kujichanganya zaidi unakubali kuwa Watanzania wameshatoka gizani,ila unarudi tena kusema wamewastukia wataka vita....nani kasema anataka vita uloifafanua wewe ya mapanga na mashoka? Watu wanapozungumzia vita si maana ya kushikakana mashati kama wewe na watawala wetu mnavyotaka Watanzania wapotoke....ni vita ya kupambana na matatizo ya watanzania kuti
okana na uongozi uliopo kushindwa kutekeleza yale yapaswayo kutekelezwa.

Wewe umetembea sana duniani uliona wapi mtu aliyeajiriwa mabao yanpokuwa magumu kikazi basi analeta mke,watoto na kila awezaye kumsaidia ili atimize wajibu wake kiajira? Au uliona wapi timu ya mpira yenye kukabiliwa na mechi ngumu ikaamua kuteua marefa,uwanja,muda wa mechi,washangiliaji na kisha yenyewe kutoa mgeni rasmi atakaye ipa Kombe?...hivi hii timu ikisema tumetwaa ubingwa kabla ya siku ya mechi itakuwa inasema uongo?

Lkini itakuwa ajabu sana kama timu hii hii itaanza kulalamika kabla ya mechi kuwa wapinzani wao wtaleta fujo,watamwaga damu nk wakati yenyewe ina kila aina ya mbinu kushinda kama nilivyoeleza awali.Ni kwa sababu inajua hata refa akiiachia ifunge haina wafungaji kw ahivo sasa inataka ushindi wa mezani.
 
mmmhhhhhhh kweli mie simuelewi. Sasa nimemuuliza hajibu. Nikiandika vibaya anatishia kujinyonga. Mi nadhani naomba nimuazime kamba akajinyonge kisha akishamaliza kujinyonga anirudishie kamba yangu.

ah kujinyonga tena? sasa na hayo mafao ya kazi atakula nani?
 
Maggid,

Anapata wakati mgumu sana katika hii forum, kwani hapa anakutana na watu wanaofikiria nje ya boksi; zaidi ya yote, watu wengi hapa wameweka maslahi ya taifa mbele. Mimi nachukizwa sana na article nyingi za huyu Mheshimiwa kutokana na upendeleo wa zairi anaouonyesha kwa Kikwete na chama. Huyu mtu anasafiri vijijini kila siku, ameona mateso ambayo mamilioni ya watanzania waishivyo vijijini wanayopitia lakini anashindwa kuona uwiano katika ya umaskini na sera mbovu za chama tawala.

Ni juzi tuu, mtoto wa Kikwete alitimuliwa hapo Iringa, Maggid aliogopa hata kupost picha kwenye Blog yake. Rais alipokuwa Iringa na kumsafisha mtuhumiwa wa kesi ya rushwa Mwakalebela, Maggid kama kawaida yake alikula kobisi. Inapokuja kwa Dr. Slaa, Maggid anapinga tuu bila sababu za msingi ! Juzi alionyesha rangi zake za asili pale alipojaribu kumtie(kumjumuisha) Dr. Slaa na ugonjwa wa Mr. Kihovella, nilimwandikia email kali sana kwenye comments section ya blog yake na kawaida hakuipost.
 
Maggid,

Anapata wakati mgumu sana katika hii forum, kwani hapa anakutana na watu wanaofikiria nje ya boksi;
huyo hata kufikiria kwenye boksi hayupo... labda anafikiria some place which doesnt exist

naskia anataka kujiua, ni kweli?
 
I vowed not to reply to Maggid's posts but let me ask rather than replying him

is there a way you can improve you presentation skills? tumasoma habari nyingi sana ndefu lakini hatuchoki, ya kwako inakosa kitu fulani, its like you are struggling even to understand yourself

Au basi unaweza ukawa unatoa summary ya hizo barua zako?

Acid ndugu yangu,

Kuna wanaojibu kwa kuuliza. Nami nakuuliza; Je, umevunja kiapo chako cha kutokujibu posts zangu?
 
huyo hata kufikiria kwenye boksi hayupo... labda anafikiria some place which doesnt exist

naskia anataka kujiua, ni kweli?

Mpwa,
Asikuumize kichwa huyu.....anachokonoa ili watu waseme JK uwezo hana kutokana na dini yake..aanze maneno...hatuendi huko sisi...wako watu wa dini yake wenye uelewa sana tu
 
Acid ndugu yangu,

Kuna wanaojibu kwa kuuliza. Nami nakuuliza; Je, umevunja kiapo chako cha kutokujibu posts zangu?
Maggid, sijajibu post bali nimeuliza swali... hivi kusibu na kuuliza ni sawa??
 
Maggid,

Anapata wakati mgumu sana katika hii forum, kwani hapa anakutana na watu wanaofikiria nje ya boksi; zaidi ya yote, watu wengi hapa wameweka maslahi ya taifa mbele. Mimi nachukizwa sana na article nyingi za huyu Mheshimiwa kutokana na upendeleo wa zairi anaouonyesha kwa Kikwete na chama. Huyu mtu anasafiri vijijini kila siku, ameona mateso ambayo mamilioni ya watanzania waishivyo vijijini wanayopitia lakini anashindwa kuona uwiano katika ya umaskini na sera mbovu za chama tawala.

Ni juzi tuu, mtoto wa Kikwete alitimuliwa hapo Iringa, Maggid aliogopa hata kupost picha kwenye Blog yake. Rais alipokuwa Iringa na kumsafisha mtuhumiwa wa kesi ya rushwa Mwakalebela, Maggid kama kawaida yake alikula kobisi. Inapokuja kwa Dr. Slaa, Maggid anapinga tuu bila sababu za msingi ! Juzi alionyesha rangi zake za asili pale alipojaribu kumtie(kumjumuisha) Dr. Slaa na ugonjwa wa Mr. Kihovella, nilimwandikia email kali sana kwenye comments section ya blog yake na kawaida hakuipost.

Rufiji,

Unayoyaandika hapa hayana chembe ya ukweli. Ni hisia zako tu. Na huyo mgonjwa Mr. Kihovela ni nani? Halafu unashangaa kuwa comments zako hazikuchapwa kule Mjengwablog. Hebu rudi tena kwenye ulichokiandika, angalia facts halafu tuma comments zako, bila shaka zitachapwa.
Mjengwablog si jukwaa la majungu wala kuwatuhumu na kuwahukumu watu kwa kuwataja majina, bila ushahidi.
 
Rufiji,

Unayoyaandika hapa hayana chembe ya ukweli. Ni hisia zako tu. Na huyo mgonjwa Mr. Kihovela ni nani? Halafu unashangaa kuwa comments zako hazikuchapwa kule Mjengwablog. Hebu rudi tena kwenye ulichokiandika, angalia facts halafu tuma comments zako, bila shaka zitachapwa.
Mjengwablog si jukwaa la majungu wala kuwatuhumu na kuwahukumu watu kwa kuwataja majina, bila ushahidi.

Kwa hiyo hukutaka kujinyonga?
 
Ndugu zangu,

Wahehe wana msemo; Isenga imbofu na isenga indenyeefu.

Kwamba ng’ombe kipofu ni sawa tu na ng’ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Ng’ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu naye hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.

Tunavyoenenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng’ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako na hata mahala pako pa kazi.

Leo kuna wanaotafuta visingizio vya kuingia vitani. Kuna wanaodai wanapigana kuwatetea wanyonge walio gizani. Walio gizani nao wameanza kuona katika giza hilo hilo, maana wamekuwa gizani kwa muda mrefu.

Wameshtuka. Wanahoji mantiki ya vita vinavyopiganwa kwa niaba yao. Na walioamua kuingia vitani nao wanaonekana kutojiandaa vema na vita hivyo, wanaelekea kushindwa, maana wanapigana vita vya kinafiki. Na kamwe usiingie kwenye vita kama hujajiandaa.

Mwingine atasema; vita vingine havina budi kupiganwa hata kama hujajiandaa kupigana na kushinda. Hapana, huendi vitani ili mradi tu unakwenda vitani , kama vile unakwenda harusini. Vita si lelemama.
Katika dunia hii inasemwa; chagua vita vyako. Haina maana uchague vita kama unachagua mashati ya mitumba Kariakoo. Ina maana kubwa. Pima kwanza, soma alama za nyakati. Chagua vita inayoshindika, iliyo ya muhimu kupiganwa na unayokuwa na hakika ya kuwa umejiandaa vema kulipa gharama ya ushindi. Kwamba unachokipigania si cha kinafiki.

Angalia kwanza kwenye kabati lako, kabla hujaanza kutangaza kwa watu, kuwa kabati la jirani yako lina mzoga unaonuka, huenda nawe unao, umeanza kutoa harufu, lakini unahisi tu harufu ya mzoga wa jirani yako!

Wengi wetu tumekutana na hali ya kuwaona jogoo wawili wakipambana. Kawaida ya mpambano wa majogoo wawili ni kuvutia watazamaji. Na kila mtazamaji huwa na hulka ya kuchagua jogoo wake wa kumshangilia; kama ni jogoo mweusi na mwekundu, basi, kutakuwa na mashabiki wa jogoo mweusi na wale wa mwekundu. Yahitaji ujasiri kuamua kuwa katikati, kutochagua jogoo wa kumshabikia.

Na hutokea, kwa yule ambaye jogoo wake ameshindwa pambano, basi, atatoka mahali hapo kwa masikitiko, akiwa na unyonge, kisa? Jogoo wake kashindwa! Ni hulka ya mwanadamu. Yahitaji ujasiri kuamua kuwa katikati, kutochagua upande. Kutochagua jogoo wa kumshabikia. Wapo wanadamu wenye ujasiri huo. Pambano linapoendelea au linapomalizika, basi, huweza kutoa tathmini isiyoegemea upande mmoja.

Ndio, tunapaswa pia kutumia bongo zetu katika kutoa hukumu, na si kuongozwa na mapenzi ya moyoni tu. Hivyo ndivyo wafanyavyo mahakimu na majaji wanapoamua mashauri mahakamani. Usiishie tu kumlaani jogoo mwekundu anayeonekana kuwa na maumbile makubwa kwa kumtwanga jogoo wako mweusi mwenye maumbile madogo. Ukiumiza kichwa, unaweza kubaini , kuwa jogoo mwekundu alikuwa na sababu na haki za kumtwanga jogoo wako mweusi. Unatakiwa kuwa na ujasiri wa kuyaangalia mapungufu ya jogoo wako mweusi. Si wengi wenye kutaka kuifanya kazi hii ya kuumiza vichwa, kutafakari mapungufu yao na yale ya wanaowashabikia.

Naam. Maisha ni mapambano, kuna kushinda na kushindwa. Ushindi una gharama. Mwanadamu jiandae na gharama ya ushindi. Ushindi waweza kuwa ghali mno. Unaweza kupambana ukashinda, lakini gharama ya ushindi yaweza kuwa jamaa na marafiki wa wote uliowashinda watageuka kuwa maadui zako, yawezekana
watakuwa maadui kwako kwa muda mrefu tu. Watakukasirikia, watafanya yote nawe upate maumivu.

Hivyo, mwanadamu usifikiri tu gharama ya kushindwa, fikiri pia gharama ya ushindi. Na wakati mwingine, ni gharama inayostahili kulipwa. Franklin Roosevelt alikuwa Rais wa zamani wa Marekani. Alifahamu faida na hasara za kuwa na maadui. Waliompinga katika sera zake za kiuchumi aliwaita " Watiifu wa Kiuchumi" Na akasema; wamejiunga kwa pamoja kunichukia na nakaribisha chuki zao kwangu!

Kama unapigana vita ya muhimu, kama vita hivyo vyaweza vikawa vya kushinda (winnable). Na kwamba umejiandaa kulipa gharama ya chuki ya muda mrefu ya utakaowashinda, basi, ingia vitani, na kama la, tafuta suluhu au rudisha majeshi nyuma kimpangilio ( tactical retreat).

Swali ni hili; utafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani au la?

Miaka mingi iliyopita alitokea Mfalme wa Epilus aliyeitwa Pyrrhic. Mfalme huyu aliamua kuingia vitani kulikabili jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi, ni jeshi la Warumi. Lakini kabla ya Mfalme kuingia baharini na vikosi vyake kuitafuta Italia ya Warumi, msaidizi wake wa karibu, Cineas, aliomba mazungumzo ya faragha na Mfalme. Alitaka kumwuliza maswali na kumshauri.

Cineas alimtamkia Mfalme; “ E bwana Mfalme, Warumi wanasadikika kuwa na jeshi kubwa , lenye nguvu na lenye mashujaa wengi. Ndio maana wameteka nchi nyingi. Je, Mungu akitusaidia, tukaja kuwashinda Warumi,
tutafanya nini na ushindi wetu? Mfalme akajibu: “ Mbona hilo ni swali jepesi sana. Mara ile tukiwashinda Warumi, hakutatokea jeshi kutoka mji wowote wa Italia litakaloweza kupambana nasi.”

Cineas alitulia kidogo, kisha akamwuliza Mfalme: “ Tukishaikamata Italia ya Warumi, kipi kitafuatia?”
Mfalme akajibu: Sicily ni kisiwa chenye hazina za thamani kubwa, itakuwa rahisi sana kukiteka kisiwa hicho.”
Cineas aliendelea kuuliza: “ Bwana Mfalme, unaongea juu ya mambo ya kusadikika, lakini una maana kukitwaa kisiwa cha Sicily kutakuwa na maana ya kukoma kwa vita?” Mfalme akajibu: “Hapo tutakuwa tumeikaribia Afrika. Na tukishaikamata Afrika ni nani hapa duniani atathubutu kutukabili kivita?” “Hakuna” Alijibu Cineas, kisha akauliza; “ Na baada ya hapo tutafanya nini?”

Mpaka hapo Mfalme hakujua Cineas alikuwa anampeleka wapi kwa lojiki ya kifikra. Mfalme akajibu:
“Baada ya hapo, tutapumzika, tutakula raha. Tutakula na kunywa. Tutabaki tukichekeshana na kucheka, siku nzima.”

Kama ni hivyo, alisema Cineas; “ Ni kitu gani kinachotuzuia kufanya hayo yote sasa bila kwenda vitani?
Mfalme hakuielewa mantiki ya Cineas. Akakaidi ushauri. Akavipeleka vikosi vyake kupambana na Warumi. Baada ya vita ngumu, jeshi la mfalme liliwashinda Warumi. Hata hivyo, lilipata hasara kubwa ya kupoteza watu na kuwa na majeruhi wengi. Jeshi lake likadhohofika sana. Likajaribu kuitwaa Sparta, likashindwa vibaya sana. Mfalme aliwindwa na hatimaye akakakamatwa kama kuku na kuawa kwa kupigwa mawe kwenye mitaa ya Argos.

Isenga imbofu na isenga indenyeefu. Ng’ombe kipofu ni sawa tu na ng’ombe aliyevunjika mguu.

Na hilo ndilo ‘Neno Leo.’

Maggid,
Iringa.

"Numerous politicians have seized absolute power and muzzled the press. Never in history has the press seized absolute power and muzzled the politicians.
-- David Brinkley
 
Maggid, sijajibu post bali nimeuliza swali... hivi kusibu na kuuliza ni sawa??

Ndugu yangu Acid,
Na hilo ndilo jibu lako kwa swali langu. Unaendelea kuvunja kiapo chako!
 
Title yenyewe tenge...ng'ombe akipata ulemavu huchinjwa haraka asilete usumbufu sasa sijui mwenzetu huko Iringa hamuwachinji manakaa nao?
 
Enzi za Mwalimu komedi huwa inanifurahisha sana pale Masanja anaposema 'pumbafu zenu' hahhaha waliopo kwenye kundi hili ni wengi mmojawapo ni Maggid. Huu uandishi wa habari wako wa chini ya mwembe una mapungufu mengi sana. Acha kuwa hypocritic wewe Maggid si useme ukweli unamtetea nani na nani unamponda.. Hata kama tunafanya kwa manufaa ya walio chache shida yako nini na hao waliopo madarakani wanafanya kampeni kwa ajili ya nani si kwa ajili yao binafsi na familia zao na mafisadi wenzao.
 
Rufiji,

Unayoyaandika hapa hayana chembe ya ukweli. Ni hisia zako tu. Na huyo mgonjwa Mr. Kihovela ni nani? Halafu unashangaa kuwa comments zako hazikuchapwa kule Mjengwablog. Hebu rudi tena kwenye ulichokiandika, angalia facts halafu tuma comments zako, bila shaka zitachapwa.
Mjengwablog si jukwaa la majungu wala kuwatuhumu na kuwahukumu watu kwa kuwataja majina, bila ushahidi.

Maggid,

Majibu yako hapo juu yanadhihirisha ni kwa jinsi gani ulivyokunywa maji ya bendera. Juzi uliandika ya kwenye blog yako kuwa aliyesulubiwa na Slaa yuko, ukimaanisha aliyekuwa Mwenyejiti wa CHADEMA Iringa (Ndg. Kapwani), yuko hoi hospitalini. Na nilikuandika email kali sana nikikuambia ya kuwa heading yako inalengo la kum-tie Dr Slaa na ugonjwa wa huyu Bwana, ni jambo la kusikitisha to say the least! Leo nimeangalia Blog yako nimeona umebadilisha Kichwa cha habari na kusema ...Ben Kapwani Taabani Hospitalini. Naona ingawa ukupost ujumbe wangu , ujumbe ulifika na ndio maana ulibadilisha kichwa cha habari. Angalia mmoja wa wasomaji wako alivyojibu baada ya kusoma hiyo habari ya ugonjwa wa Bwana Ben:

"Hivi kwanini hata nduguze Kapwani hawamshtaki huyo mtu aliyemdhalilisha ndugu yao mpaka kupata struke? Mie ningekuwa na hata ujamaa tu na huyo bwana mbona ningeivalia njuga hiyo kesi mpaka nione mwisho wake."

Huyu mtu aliyejitambulisha kwa jina la Anonymous ali-react hivyo kutokana na heading yako. Nadhani Maggid utakuwa mkweli na kukiri katika hili baraza ya kuwa kichwa cha habari ulikibadilisha!

Pili, suala la Mwakalebela. Hivi mbona ulikuwa mwepesi wa kumlaumu Slaa kwa kumsema Kapwani, lakini ukusema lolote pale Kikwete alimvyomsafisha Mwakalebela mbele la alaiki ya wana Iringa. Jee unadhani watu wa TAKUKURU walijisikiaje? Hivi vitu vyote vinafanya watu wa kuquestion credibility yako kama Mwana habari.
 
Ndugu zangu,

Wahehe wana msemo; Isenga imbofu na isenga indenyeefu.

Kwamba ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Ng'ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu naye hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.

Tunavyoenenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng'ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako na hata mahala pako pa kazi.

Leo kuna wanaotafuta visingizio vya kuingia vitani. Kuna wanaodai wanapigana kuwatetea wanyonge walio gizani. Walio gizani nao wameanza kuona katika giza hilo hilo, maana wamekuwa gizani kwa muda mrefu.

Wameshtuka. Wanahoji mantiki ya vita vinavyopiganwa kwa niaba yao. Na walioamua kuingia vitani nao wanaonekana kutojiandaa vema na vita hivyo, wanaelekea kushindwa, maana wanapigana vita vya kinafiki. Na kamwe usiingie kwenye vita kama hujajiandaa.

Mwingine atasema; vita vingine havina budi kupiganwa hata kama hujajiandaa kupigana na kushinda. Hapana, huendi vitani ili mradi tu unakwenda vitani , kama vile unakwenda harusini. Vita si lelemama.
Katika dunia hii inasemwa; chagua vita vyako. Haina maana uchague vita kama unachagua mashati ya mitumba Kariakoo. Ina maana kubwa. Pima kwanza, soma alama za nyakati. Chagua vita inayoshindika, iliyo ya muhimu kupiganwa na unayokuwa na hakika ya kuwa umejiandaa vema kulipa gharama ya ushindi. Kwamba unachokipigania si cha kinafiki.

Angalia kwanza kwenye kabati lako, kabla hujaanza kutangaza kwa watu, kuwa kabati la jirani yako lina mzoga unaonuka, huenda nawe unao, umeanza kutoa harufu, lakini unahisi tu harufu ya mzoga wa jirani yako!

Wengi wetu tumekutana na hali ya kuwaona jogoo wawili wakipambana. Kawaida ya mpambano wa majogoo wawili ni kuvutia watazamaji. Na kila mtazamaji huwa na hulka ya kuchagua jogoo wake wa kumshangilia; kama ni jogoo mweusi na mwekundu, basi, kutakuwa na mashabiki wa jogoo mweusi na wale wa mwekundu. Yahitaji ujasiri kuamua kuwa katikati, kutochagua jogoo wa kumshabikia.

Na hutokea, kwa yule ambaye jogoo wake ameshindwa pambano, basi, atatoka mahali hapo kwa masikitiko, akiwa na unyonge, kisa? Jogoo wake kashindwa! Ni hulka ya mwanadamu. Yahitaji ujasiri kuamua kuwa katikati, kutochagua upande. Kutochagua jogoo wa kumshabikia. Wapo wanadamu wenye ujasiri huo. Pambano linapoendelea au linapomalizika, basi, huweza kutoa tathmini isiyoegemea upande mmoja.

Ndio, tunapaswa pia kutumia bongo zetu katika kutoa hukumu, na si kuongozwa na mapenzi ya moyoni tu. Hivyo ndivyo wafanyavyo mahakimu na majaji wanapoamua mashauri mahakamani. Usiishie tu kumlaani jogoo mwekundu anayeonekana kuwa na maumbile makubwa kwa kumtwanga jogoo wako mweusi mwenye maumbile madogo. Ukiumiza kichwa, unaweza kubaini , kuwa jogoo mwekundu alikuwa na sababu na haki za kumtwanga jogoo wako mweusi. Unatakiwa kuwa na ujasiri wa kuyaangalia mapungufu ya jogoo wako mweusi. Si wengi wenye kutaka kuifanya kazi hii ya kuumiza vichwa, kutafakari mapungufu yao na yale ya wanaowashabikia.

Naam. Maisha ni mapambano, kuna kushinda na kushindwa. Ushindi una gharama. Mwanadamu jiandae na gharama ya ushindi. Ushindi waweza kuwa ghali mno. Unaweza kupambana ukashinda, lakini gharama ya ushindi yaweza kuwa jamaa na marafiki wa wote uliowashinda watageuka kuwa maadui zako, yawezekana
watakuwa maadui kwako kwa muda mrefu tu. Watakukasirikia, watafanya yote nawe upate maumivu.

Hivyo, mwanadamu usifikiri tu gharama ya kushindwa, fikiri pia gharama ya ushindi. Na wakati mwingine, ni gharama inayostahili kulipwa. Franklin Roosevelt alikuwa Rais wa zamani wa Marekani. Alifahamu faida na hasara za kuwa na maadui. Waliompinga katika sera zake za kiuchumi aliwaita " Watiifu wa Kiuchumi" Na akasema; wamejiunga kwa pamoja kunichukia na nakaribisha chuki zao kwangu!

Kama unapigana vita ya muhimu, kama vita hivyo vyaweza vikawa vya kushinda (winnable). Na kwamba umejiandaa kulipa gharama ya chuki ya muda mrefu ya utakaowashinda, basi, ingia vitani, na kama la, tafuta suluhu au rudisha majeshi nyuma kimpangilio ( tactical retreat).

Swali ni hili; utafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani au la?

Miaka mingi iliyopita alitokea Mfalme wa Epilus aliyeitwa Pyrrhic. Mfalme huyu aliamua kuingia vitani kulikabili jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi, ni jeshi la Warumi. Lakini kabla ya Mfalme kuingia baharini na vikosi vyake kuitafuta Italia ya Warumi, msaidizi wake wa karibu, Cineas, aliomba mazungumzo ya faragha na Mfalme. Alitaka kumwuliza maswali na kumshauri.

Cineas alimtamkia Mfalme; " E bwana Mfalme, Warumi wanasadikika kuwa na jeshi kubwa , lenye nguvu na lenye mashujaa wengi. Ndio maana wameteka nchi nyingi. Je, Mungu akitusaidia, tukaja kuwashinda Warumi,
tutafanya nini na ushindi wetu? Mfalme akajibu: " Mbona hilo ni swali jepesi sana. Mara ile tukiwashinda Warumi, hakutatokea jeshi kutoka mji wowote wa Italia litakaloweza kupambana nasi."

Cineas alitulia kidogo, kisha akamwuliza Mfalme: " Tukishaikamata Italia ya Warumi, kipi kitafuatia?"
Mfalme akajibu: Sicily ni kisiwa chenye hazina za thamani kubwa, itakuwa rahisi sana kukiteka kisiwa hicho."
Cineas aliendelea kuuliza: " Bwana Mfalme, unaongea juu ya mambo ya kusadikika, lakini una maana kukitwaa kisiwa cha Sicily kutakuwa na maana ya kukoma kwa vita?" Mfalme akajibu: "Hapo tutakuwa tumeikaribia Afrika. Na tukishaikamata Afrika ni nani hapa duniani atathubutu kutukabili kivita?" "Hakuna" Alijibu Cineas, kisha akauliza; " Na baada ya hapo tutafanya nini?"

Mpaka hapo Mfalme hakujua Cineas alikuwa anampeleka wapi kwa lojiki ya kifikra. Mfalme akajibu:
"Baada ya hapo, tutapumzika, tutakula raha. Tutakula na kunywa. Tutabaki tukichekeshana na kucheka, siku nzima."

Kama ni hivyo, alisema Cineas; " Ni kitu gani kinachotuzuia kufanya hayo yote sasa bila kwenda vitani?
Mfalme hakuielewa mantiki ya Cineas. Akakaidi ushauri. Akavipeleka vikosi vyake kupambana na Warumi. Baada ya vita ngumu, jeshi la mfalme liliwashinda Warumi. Hata hivyo, lilipata hasara kubwa ya kupoteza watu na kuwa na majeruhi wengi. Jeshi lake likadhohofika sana. Likajaribu kuitwaa Sparta, likashindwa vibaya sana. Mfalme aliwindwa na hatimaye akakakamatwa kama kuku na kuawa kwa kupigwa mawe kwenye mitaa ya Argos.

Isenga imbofu na isenga indenyeefu. Ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu.

Na hilo ndilo ‘Neno Leo.'

Maggid,
Iringa.
Kwa hiyo warumi ndiyo ccm eeeh?
pole sana kwa kujaribu kulazimishia mfano ambao hauna mantiki na unachowaza
 
Mimi pamoja na elimu yangu nimeisoma na kusoma na kusoma na bado sijamuelewa. Mwenye elimu inayopita yangu maana hapa tunazidiana anisaidie kuifahamu. Na ikiwezekana yeye Maggid afanye hivyo nisije potoshwa. Asante.

Amesema yeye ana msapoti kikwete! na nyie mliobaki ni sawa na ng'ombe vipofu tunaomsapoti ng'ombe kiwete (Dr. Slaa) wote hatutafikia majani.

Hivi sijui Maggid kalishwa nini manake juhudi anazotumia kumpigia chapuo mkwere si za kawaida.
 
NENO LINGINE LA LEO

it's a lot easier to impress as the "big fish" in a " small pond". But When both the pond and the other "fish" are so much bigger, the one thought as a biggest fish might well get lost
 
Back
Top Bottom