Ndugu zangu wa jf naomc 2msaidie huyu ndugu yangu!!!

Nothing4good

Senior Member
Feb 19, 2011
180
55
Kuna ndugu yangu kaniomba ushauri naomba munisaidie. Huyu ni msichana mwenye miaka 22 sasa ameolewa miaka 4 iliyopita tatizo lake nikwamba mumewe kamwambia akakae kwao mpaka atakapomuhitaji ataenda kumchukua. Ni hivi huyu dada alifahamiana na huyu kaka akiwa 4m two na waliendelea na mahusiano yao mpaka alipomaliza 4m 4 ndipo wakaoana. Walifanya bonge la harusi ya kikatoliki halafu huyu kaka anafanya kazi nje ya nchi. Kila baada ya miezi mita2 huwa anarudi kumjulia hali mkewe anakaa siku mbili ta2 then anarudi kazini. Akamfungulia mkewe stationary awe anaiendesha. Cha kushangaza baada ya mwaka akamwambie mkewe asiende kuwatembelea ndugu zake (mwanaume) mkewe akauliza kwanini? Akajibiwa nimekuambia usiende full stop. Sasa bahati mbaya kukatokea msiba akaamua kwenda halafu atamuelewesha mumewe. Akiwa huko mumewe akampigia simu akamwambia ukitoka huko nenda kwenu lakini alipotoka huko akarudi kwake basi hayo yakaisha. Baada ya kama mwaka akapata mimba kwa bahati mbaya mimba ikatoka. Kumwambia mumewe kuwa mimba imetoka mume wake akawa anamwita muhuni sana wewe mwanamke umetoa mimba yangu baada ya ya hapo mumewe akamwambia kuanzia leo sitak uende stationary tena nimeshatafuta m2 wa kusimamia na hiyo kadi yako ya bank mpelekee mama yangu maskini dada wawa2 akafanya kama alivyoambiwa baada ya muda mume wake akamwambia nenda kwenu nikirud nitakuja kukuchukua bint akaenda. mumewe aliporud hakwenda kumchukua alienda mpaka kijijini kwao na kurudi na m2 anayedai ni mamdogo wake akamwambia huyo mamdogo asafishe chumba baada ya hapo akampigia simu mkewe na kumwambia wewe ni mshirikina imekutwa hilizi ufunguni mwakitanda. Sasa huyu dada anaomba ushaur afanye nini na alikuwa na wadogo zake wawili aliokua akiwasomesha kupitia biashara yake ya stationary? Wazazi wake hawana uwezo na yeye ndo mtoto wakwanza. Msaidien tafadhali
 
so complicated mpe pole.
Akamwone mchungaji (Reverend) manake kama mume anadai kukuta hirizi ni swala lisilosuluhishika bila dini.
 
Hii thread ungeileta asubuhi kabla sijachoka. Its painful indeed.

Huyu msichana nae bana hana maamuzi na mumewe anakuwa kama bora liende tu??

Ngoja nitachangia asubuhi maana hapa mkoloni kanikalia kooni
 
oooooops........................mwambie aolewe tena coz huyo bw.hana time nae tena inavooonesha.
 
Dah! mpe pole insikitisha sana, sana, japo maelezo ni ya upande mmoja, awe mvumilivu atafute kazi ya kufanya itakayomuingizia kipato, zaid amtegemee sana Mungu, na atulie kwanza asifikirie kutafuta mume mwingine kwa sasa.
 
Hii dunia ina vituko.

Huyo dada ajilaumu mwenyewe kwani inaonekana aliolewa ili kutatua matatizo ya kifamilia. Kumbe hakujua kwamba ndo anayakuza zaidi.

Hata ingekuwaje, kitendo cha kukubali kuolewa na mtu anayekutembelea baada ya miezi 3 kama boyfriend ni upuuzi (kama hakuna sababu ya msingi sana) na labda kuendekeza njaa. Pia kitendo cha kukubali kila amri ya mume ni ishara kwamba yeye aliolewa kama doll bila uwezo wowote wa kuamua jambo au kushiriki maamuzi katika ndoa. Inabidi ajifunze sasa, kwamba ndoa ni partnership na siyo utumwa.

Labda kwa kumsaidia aende mahakamani kudai haki yake (talaka), sheri inampa haki ya 50% ya mali zote walizokuwa wanamiliki kama wanandoa!!

Babu DC
 
Atakapomhitaji??Kama hamhitaji leo atamhitaji lini?

Kweli kama alidiriki kumleta mtu kuja kusafisha chumba walichokuwa wakilala na bado kamwambia alikutwa hirizi.... hivi hapo mpaka aje na nyundo akugonge kichwani ndo ujue kashakuacha...:A S 13: Mpe pole sana jamaa ndo ashamuacha hivyo!!!!!
 
Kwa kweli pole zake huyo dada! Inaonekana huyu bint aliolewa mapema sana.....miaka 18!!! Hapa naona alikosa mtu wa kumshauri, au alikataa ushauri, kwa sababu alikuwa in love. Alitakiwa asome shule kwanza, then mambo ya mapenzi baadaye! Sasa sijui baada ya kuolewa aliweza kujiendeleza kielimu! Nafikiri bado anaweza kwenda kuongea na mumewe, apate uhakika kabisa kwamba hamtaki tena, then atafute ushauri wa kisheria ili aweze kupata chochote na yeye.

Jamani ushauri kwa wadada wenzangu, hata kama umefall in love, kama una nafasi ya kusoma soma kwanza. Haya mambo ya mapenzi utayakuta tu! ni ushauri tu!
 
pole zake huyo mdada.....kama ana miaka 22 aolewe tena tu...aachane na huyo chizi.
 
Hivi nyie wanaume kwanini munanawafanyia hivi watoto wa wa2 hebu ona sasa kamuachisha mtoto wawa2 shule kana kwamba haitoshi kamuharibia na maisha tena nasema hivi kama hapa jf kuna mwanaume kama huyo!! Shame upon on your face
 
Wanaume bwana,unaweza fanya kitu mbaya sana....wakishatamani huko hawakosi sababu za kukutoa ndani......mi namshauri huyo dada awe mpole....amuite mumewe wazungumze wawekane sawa...kama mwanaume kaamua kuchukua mke mwingine bila sabau ya msingi na bila mwanamke kukosea hana haja ya kujificha na kudanganya,ampe uhuru wake kila mmoja achukue njia yake.ni ngumu kweli hasa kwa msichana ila nimejifunza ukilazimisha kitu utaumia mara tatu yake.....Mungu ni mwaminifu,ametuponya vidonda vingi sana ni vile hatuna muda wa kusema...time is a healer,akatulie kwa wazazi,arudi shule,she is still young.....asome kwa bidii chochote anachopenda na ili aache hayo ya kutegemea mwanaume na aweze kusaidia familia yake bila support ya mwanaume.....hajachelewa......zaidi ya yote asamehe,na amuombe sana Mungu na azidishe umakini kwenye maamuzi yake manake hawakosekani wa kumuongezea maumivu.....mpe pole sana....hakuna kukata tamaa,maisha lazima yasonge mbele.....ajiamini tu na kuzidisha sala!
 
Kama wadau walivyosema hapo juu, huyo dada kuna mahali alicheza karata zake vibaya (miscalculations). Ila bado ana nafasi.

Hivi kweli mtu anakuwa tayari amekaa kwenye ndoa na bado ana miaka 22 ina maana aliolewa akingari mtoto? Kwa nini wasichana wanafanya makosa makubwa namna hiyo? Tena si ajabu mume anamzidi kama miaka 10 hivi? Kwa maana nyingine msichana asiyejua maisha anaoelewa na jamaa ambaye tayari kamaliza mizinguko yoote ya majaribio!!

Hivi akina dada wanadhani ndoa ni mbio za marathoni kwama ukishinda unapata gold medal?
 
Huyo dada mbona kama anapelekwa pelekwa kama gari bovu! Aaaggr! Nenda kwenu, haya mme wangu, peleka kadi kwa mama, haya mme wangu. Siku ataambiwa avue nguo atembee uchi. Khaa!!
Amsubiri mumewe arudi wajadili kwanza.
Halafu ameolewa bado mdogo. Lol!
 
Hivi sisi wanaume tuna matatizo gani lakini? Hatuoni uchungu kuwatendea wenzetu hivi?
 
Kama wadau walivyosema hapo juu, huyo dada kuna mahali alicheza karata zake vibaya (miscalculations). Ila bado ana nafasi.

Hivi kweli mtu anakuwa tayari amekaa kwenye ndoa na bado ana miaka 22 ina maana aliolewa akingari mtoto? Kwa nini wasichana wanafanya makosa makubwa namna hiyo? Tena si ajabu mume anamzidi kama miaka 10 hivi? Kwa maana nyingine msichana asiyejua maisha anaoelewa na jamaa ambaye tayari kamaliza mizinguko yoote ya majaribio!!

Hivi akina dada wanadhani ndoa ni mbio za marathoni kwama ukishinda unapata gold medal?

Mapenzi alianza akiwa form 2!!!!! yaani sipati picha nilipokuwa form 2 kuwa na uhusiano na njemba.....................
na wazazi waliruhusu mtoto wao kuolewa akiwa na miaka 18? au sababu wana shida kwa hiyo wakaona wamtoe tu ili asaidie familia?
mshauri abaki kwao, huyo mume inaonyesha kabisa hana haja naye, alikuwa anamtafutia sababu tu.
 
Mapenzi alianza akiwa form 2!!!!! yaani sipati picha nilipokuwa form 2 kuwa na uhusiano na njemba.....................
na wazazi waliruhusu mtoto wao kuolewa akiwa na miaka 18? au sababu wana shida kwa hiyo wakaona wamtoe tu ili asaidie familia?
mshauri abaki kwao, huyo mume inaonyesha kabisa hana haja naye, alikuwa anamtafutia sababu tu.


FP,

Hivi kuolewa ni dili namna hiyo? Ngoja niombe ruhusa kwa bibi nichangamkia toto dogo.....!!!

Hata kama ni shida hawa wazazi walizidisha sana!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom