Ndugu Yenu Ali Haji Haji Anahitaji MsaadaWenu.

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
[h=2]Ndugu Yenu Ali Haji Haji Anahitaji Msaada Wenu.[/h]

Haji Ali Haji (32) ni mkaazi wa Chaani Mchezashauri ameanguka akiwa anaokoa zao la karafuu 2001, kwa sasa ni mlemavu wa viungo alilazwa Hospitali ya M/Mmoja mwaka mmoja lakini hali ngumu ya maisha imepelekea kukosa tiba ya uhakika na kukosa hisia kwa kutokwa haja kubwa na ndogo akiwa kitandani .

Hivi karibuni tu miezi mitatu iliyopita Haji alianguka tena na kigari chake na hivyo kuumia tena mguuu ambao kwa mujibu wa maelezo ya vipimo vya Daktari amevunjika mguu na hivyo anahitaji huduma ya dharura nyengine asafirishwe na kupelekwa Dar-es Salaam kwa matibabu zaidi ,lakini hali ngumu ya maisha anashindwa kupata tiba ya uhakika na kuendelea kudhoofika afya yake ndani kwa ndani.

Kwa hivi sasa Haji anahitaji msaada hivyo yule ambae anahitaji kumsaidia anaombwa kuwasiliana nae 0773704853 ama 0715414592 .KUTOA NI MOYO
 
Back
Top Bottom