Njilembera
JF-Expert Member
- May 10, 2008
- 1,496
- 607
Bintimkonge asante kwa kufafanua, ni kweli kabisa Tanzania haikuwa nchi pekee iliyokuwa na uhaba wa bidhaa enzi zile. Hata wenzetu wa Zambia ambao walionekana kuwa na unaffuu (kama mnakumbuka zile sabuni muruwa za bafuni kutoka Zambia enzi hizo) walitamba kwa siku chache tu kabla ya 'new international economic order' kuwakumbatia! Naamini kabisa ni kosa kufikiri kwamba matatizo/mafanikio ya uchumi kwa nyakati fulani yanawiana na sera binafsi za kiongozi fulani. Nionavyo Nyerere angekuwa ni kiongozi wa awamu ya tatu, ukuzi uchumi ungaliweza kuwafaidi wengi zaidi kuliko ilivyokuwa.
Dhana nninayoilaani kwa nguvu zote ni hii ya umimi au uyeye katika maendeleo ya taifa. Inavunja nguvu za wale wanaopenda kujenga. Tukiamini kuwa sio rais na wala nani tuliyemchagua anaweza kubadili mwenendo wetu wa maendeleo, tunajiwekea uwigo mkubwa wa maendeleo. Sharti ni moja tu hao viongozi wawe kweli ni matunda ya demokrasia ili wasimamie yale tunayoyataka, sio wao wajisemee eti uwazi na ukweli wakati sisi tunaamini tofauti, au ari mpya maisha bora wakati hata hatung'amua tuko na ari gani. Naamini ni dhambi kupachika majina ya viongozi kwa miradi mbalimbali, mara eti ni Daraja la sijui Mkapa(wapi na wapi jamaini Mkapa hajaanza uwaziri, watu walikuwa wanajadili ujenzi huo), Sijui BWMkapa Towers badala ya Mafuta House hali mradi huo ulikuwepo tangu miaka ya 1970 ikawa imecheleweshwa na Kumekucha Auction Mart kama wapangaji, na mradi ukaanza kwa mikiki kabla ya 1995. Tusiwape sifa watu bila sababu
Dhana nninayoilaani kwa nguvu zote ni hii ya umimi au uyeye katika maendeleo ya taifa. Inavunja nguvu za wale wanaopenda kujenga. Tukiamini kuwa sio rais na wala nani tuliyemchagua anaweza kubadili mwenendo wetu wa maendeleo, tunajiwekea uwigo mkubwa wa maendeleo. Sharti ni moja tu hao viongozi wawe kweli ni matunda ya demokrasia ili wasimamie yale tunayoyataka, sio wao wajisemee eti uwazi na ukweli wakati sisi tunaamini tofauti, au ari mpya maisha bora wakati hata hatung'amua tuko na ari gani. Naamini ni dhambi kupachika majina ya viongozi kwa miradi mbalimbali, mara eti ni Daraja la sijui Mkapa(wapi na wapi jamaini Mkapa hajaanza uwaziri, watu walikuwa wanajadili ujenzi huo), Sijui BWMkapa Towers badala ya Mafuta House hali mradi huo ulikuwepo tangu miaka ya 1970 ikawa imecheleweshwa na Kumekucha Auction Mart kama wapangaji, na mradi ukaanza kwa mikiki kabla ya 1995. Tusiwape sifa watu bila sababu