Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 943
NDUGU SHEMSA MOHAMMED AONGOZA KAMATI YA SIASA MKOA WA SIMIYU KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM WILAYA YA MEATU
Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Simiyu chini ya Mwenyekiti wake ndugu Shemsa Seif Mohammed tarehe 22/11/2023 imeendelea na ziara yake ya kukagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi 2020/2025 ndani ya Mkoa wa Simiyu, Wilaya ya Meatu, Jimbo la Meatu
Katika Jimbo la Meatu jumla ya Miradi 6 yenye thamani ya bilion 10.829 iliyotolewa na Serikali ya Awamu ya sita chini ya Mwenyekiti wa CCM ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekaguliwa.
Miradi hiyo ni pamoja na;
1. Utafiti wa Maji, Uchimbaji wa kisima na Bwawa kata ya Bukundi, Kijiji Cha Lukale iliyogharimu Tsh. 60,000,000/=
2. Ujenzi wa Matundu 10 ya Vyoo Shule ya Msingi Kasala iliyogharimu Tsh.11,000,000/=
3. Mradi wa kupeleka Umeme Vijijini (REA) III R2, Kijiji Cha Lukale iliyogharimu Tsh. 1,167,703,951/=
4. Ujenzi wa Daraja la Itembe iliyogharimu Tsh. 8,400,000,000/=
5. Ujenzi wa Lami Mwanhuzi Km 1.25 na Taa zinazotumia Nishati ya Jua yenye thamani ya *Tsh 999,303,450/= na
6. Matengenezo ya Barabara ya Rest House - Mwanzagamba iliyogharimu Tsh. 190,451,580/=
Hata hivyo, Kamati ya Siasa ya Mkoa Simiyu imeridhishwa kwa kiasi kikubwa na Utekelezaji wa Miradi hiyo
Attachments
-
WhatsApp Image 2023-11-23 at 15.53.15.jpeg178.7 KB · Views: 5
-
WhatsApp Image 2023-11-23 at 15.53.15(2).jpeg179.9 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-11-23 at 15.53.15(3).jpeg192.9 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-11-23 at 15.53.17.jpeg254.1 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-11-23 at 15.53.16(1).jpeg198.8 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-11-23 at 15.53.16.jpeg217.8 KB · Views: 5