Ndugai na genge lake wasituharibie nchi!

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,607
51,519
Mwalimu alishalionya Taifa, kuwa ukiona kuna watu wanapita na kupiga kampeni za kumtaka raisi aongezewe muda, kimsingi wanakuwa wanapigania matumbo yao maana hawana uhakika kama raisi ajaye atawapa nafasi walizonazo sasa.

Kwa muda mrefu sasa Spika Ndugai amekuwa akibehave kama kikaragosi fulani kisichojielewa kwa kuwa bussy kulinda positions za serikali hata kwenye mambo ya hovyo badala ya kusimama kidete kuisimamia serikali ifanye mambo sawasawa.

Alianza mambo yake ya hovyo wakati wa sakata la Tundu Lissu kwa kudai hajui alipo wakati anajua alipo na barua kati ya ofisi na familia za Lissu zipo, Akaja kwenye suala la CAG wakati ule akiwa ni profesa Assad, anekuwa akioneanea wabunge wa upinzani ndani ya bunge, Baadae akamtwaa mtu aliyehamia CCM na kumfanya kuendelea kuwa mbunge kwa tiketi ya Chadema wakati mbunge huyo amekaribishwa CCM na viongozi wa chama cha mapinduzi na kauli ya kuhamia chama hicho kaitoa mbele ya media, Sasa Funga kazi ni hii, ya KUTAKA MIHULA YA URAISI IBADIRISHWE RAISI AENDELEE KUKAA MADARAKANI.

Huyu naye eti ni Spika, Spika wa ajabu kabisa ambaye badala ya kuangalia future ya nchi yeye anaangalia maslahi ya muda mfupi ya kisiasa

Kwanza, ajue, au afundishwe na aelimishwe, kuwa, Vipindi katika katiba viliwekwa miaka ya 1980's baada ya Taifa kutambua kuwa sababu mojawapo ya mataifa mengi ndani ya Afrika kutumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, Mapinduzi ya mara kwa mara ilikuwa ni kukosekana kwa succession plan, yaani utaratibu mmoja wa kupasiana kijiti cha madaraka kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine, hali hiyo ilitengeneza sintofahamu iliyopelekea mambo ya mapinduzi. Je Ndugai anataka kutengenezea nchi yetu Utaratibu wa watu kuingia Msituni au Maasi ya Kijeshi kumuondoa mtawala wasiyemtaka?
Je Ndugai anataka nchi yetu ianze kutawaliwa kama nchi za Kifalme?, Maana ukiondoa term limit huwezi kuandika kuwa hiyo ni kwa ajili ya Magufuli tu, maana Magufuli ni binadamu siku akifa maana yake atakeyakaa kwenye hicho kiti atakuta akina Ndugai wameshamuandalia mazingira na yeye kuwa mfalme. Nchi gani ya ajabuajabu akina Ndugai wanataka kuirithisha vizazi vyetu?

Lakini Kauli ya Ndugai pia ni matusi kwa maraisi wetu mzee Mwinyi, Mkapa na Kikwete, maana hata hao pia wangewasikiliza watu wanaotaka tubadili katiba ili waendekee kutawala huenda hadi leo hii Mzee Ruksa au Mkapa au Kikwete ndiye angekuwa bado raisi, Je ina maana hawa wazee wetu walioheshimu vipindi vyao vya utawala na ambao waliignore kauli za wachunia tumbo walikuwa wajinga?

Ni aibu kubwa, tena ni aibu kubwa mno Taifa kuwa na Spika, mtu wa aina ya Ndugai. Yeye anaangalia nafasi yake ya uspika badala ya kuangalia faida pana za nchi ya kwa nini waasisi na viongozi waliofuata waliamua uamuzi wa busara kabisa wa kuweka vipindi vya uongozi. Waliweka hivyo ili iwe kama njia ya kufungua madirisha kila baada ya miaka kumi Taifa lipumue!

Yaani Ndugai anataka kuiambia nchi na CCM kuwa Taifa Zima halina mtu kama Magufuli?, Nyerere alikuwepo na kwa vigezo vyote alikuwa bora mara 90 kuliko Magufuli lakini busara zilimuongoza na kusema kuwa kwa kweli ili nchi yetu iwe na amani lazima tuwe na vipindi vya uongozi.

Na Ndugai aelewe, hii nchi haihitaji mtu mmoja kuiongoza ifanikiwe, hii nchi inahitaji mifumo mizuri na thabiti, badala ya kudhani ili Tuendelee tunamhitaji Magufuli, aanze kufikiri kuwa ili tuendelee tunahitaji mifumo iliyoimara, inayoweza kujiadjust kipindi tukipata kiongozi mwendawazimu na ambayo. itatoa ushirikiano mzuri pindi tukipata kiongozi mwenye hekima.

Ndugai na genge lake waache maslahi binafisi ajue tu kuwa Magufuli ni binadamu, ipo siku atazeeka, ipo siku atakufa Sasa asiliweke Taifa zima katika mikono ya mtu mmoja as if huyo mtu ataishi milele!. Leo unataka kubadili katiba Magufuli aendelee kutawala, kesho akiwa hayupo kwa sababu ambazo. nimezitaja kisha akaja mtawala kama Bokassa, Ndugai anataka Taifa tuendelee kutawaliwa naye kwa miaka lukuki isiyo na kikomo?

Ndugai na genge lake wasiijengee nchi mazingira ya kushawishi mapinduzi ya kijeshi na maasi katika nchi kwa kuondoa vipindi vya uongozi ambavyo hekima ya kuviweka ni kudiscourage vitu kama hivyo!

Ndugai umetukosea heshima sana Watanzania, Jiangalie!!
 
Ndugai amejisahau Sana. Anavunja katiba kupendelea chama chake bila aibu. Kama hili la kuamuru wabunge waliojiuzulu kuendelea na ubunge ni ajabu Sana.

Yaani kwa sasa ndugai yupo juu ya Katiba!

Hivi, hakuna sheria ya kuwajibisha mtu anayevunja Katiba ya nchi??!
 
Ndugai amejisahau Sana. Anavunja katiba kupendelea chama chake bila aibu. Kama hili la kuamuru wabunge waliojiuzulu kuendelea na ubunge ni ajabu Sana.

Yaani kwa sasa ndugai yupo juu ya Katiba!

Hivi, hakuna sheria ya kuwajibisha mtu anayevunja Katiba ya nchi??!
Sheria ya kuwawajibisha wanaouvunja katiba wameirekebisha wamejiwekea kinga waziri mkuu, makamu wa raisi, Spika naibu Spika, na Jaji mkuu huwezi kuwashitaki wao kama wao iwapo watafanya maamuzi ya hovyohovyo ya kuvunja katiba, hata kama wameyafanya makusudi!
 
Nduguye ASINA MAHALA!!(hana akili), ni kigogo chao hicho! urais ni miaka kumi tu full stop, kabla genge lake hawajafanikisha hilo waende kutembelea kaburi la Nkurunzinza na makaburi ya raia ya 2015 huko Burundi wakajifunze! ogopa kuwatibua watu wenye njaa na wasio na kazi! Nduguye hajui 92% bongo zaidi ya watu 45m wako sekta binafsi na isiyo rasmi wasio na mshahara wala uhakika wa mlo, wengi hawana mbele wala nyuma hawa wote ni watu wasio na tumbo kubwa na mashavu ya kumimina kama yake! binafsi wabunge wanaoleta mada hii ya kumuongezea Mkulu muda hunichefua mno! sababu kila Rais hunufaisha genge lake la watu flani hivyo ni lazima muda ukiisha atoke aje mwingine na genge jingine lifaidi!! haya majitu mapumbavu kupelekwa bungeni kutuwakilisha tayari wamejimilikisha nchi!
 
Tatizo ni sisi tumelala usingizi wa pono!
masoudkipanya_CBR7kcPjIf7.jpg
 
Hawana akili hao. Ndugai anawaza uspeaker tu. Anaogopa kuwa speaker wa term moja. Hapo umesema point kabisa. Unaondoa ukomo halafu akija patikana Rais wa hovyo mtabadili tena katiba ?Wasiirudishe nchi ilikotoka. Mwenye hotuba ya Nyerere kuhusu muda wa madaraka atuwekee. Nakumbuka nilisoma mahali Nyerere alisema hakuna Rais atakaengonza muda mrefu kama Nyerere tena unless awe dictator. Ni dictator tu ndo atakubali kuongoza zaidi ya 10 yrs.
 
Hawana akili hao. Ndugai anawaza uspeaker tu. Anaogopa kuwa speaker wa term moja. Hapo umesema point kabisa. Unaondoa ukomo halafu akija patikana Rais wa hovyo mtabadili tena katiba ?Wasiirudishe nchi ilikotoka. Mwenye hotuba ya Nyerere kuhusu muda wa madaraka atuwekee. Nakumbuka nilisoma mahali Nyerere alisema hakuna Rais atakaengonza muda mrefu kama Nyerere tena unless awe dictator. Ni dictator tu ndo atakubali kuongoza zaidi ya 10 yrs.
Mwenyewe alisema ataishia term ya pili.
 
WANATAKA KUMUUZIA MAGUFULI NCHI.
badae waje kulia lia kuwa nchi inaongozwa kishamba..
10 inatosha.
Tanzania ina sifa nzuri africa na duniani kote.
Kwenye kubadilishana madaraka.
Msije mkatuchafulia hii sifa.
Hayo mambo tuwaachie kagame na m7.
Sisi HAPA 10 MWISHO.
Ili uondoke KWA HESHIMA KAMA WENZIO.
 
Hakuna sheria inayoweza kuwazuia hawa watu kutupeleka ufalmeni Bali Wananchi pekee kupitia kura zao ambazo ni lazima wazilinde hawa wasirudi Bungeni.Wamejipambanua kuwa hawafuati na kuilinda katiba waliyoapa kuilinda.

Wamepoteza sifa wote na lichama lao,tuwakatae.Hawana uwezo wa kuiba kura zote tukiamua.Hii ndiyo nchi pekee tuliyopewa na Muumba wa mbingu na nchi,tusitishwe na propaganda.
 
Cha ajabu zaidi ni kwamba Raisi huyu hafai kabisa, hata hii miaka mitano tumefika kwa aibu, taabu, mateso, mauaji na upuuzi mwingi tu! Nchi hii ingekuwa na katiba kama ya South Africa, huyu angeondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani nae mapema tu...asingefikisha hata hii mitano!

Sasa ndio wendawazimu wanatuambia eti aendelee sijui npaka lini eti!... wanatuinaje hawa?
 
Ndugai amejisahau Sana. Anavunja katiba kupendelea chama chake bila aibu. Kama hili la kuamuru wabunge waliojiuzulu kuendelea na ubunge ni ajabu Sana.

Yaani kwa sasa ndugai yupo juu ya Katiba!

Hivi, hakuna sheria ya kuwajibisha mtu anayevunja Katiba ya nchi??!
Sheria ipo ila wameamua kuikanyaga wakijua hakuna watakachofanyiwa.Wametunga haraka sheria ya kutokushtakiwa ili wakamilishe transition to their Kingdom.Tumeporwa Tanzania aliyoijenga Mwl.Nyerere sasa tunaelekea Hima Empire(Bahima).
 
Yaani huyu Ndugai anatugeuza watanzania wote kama hatuna akiki kabisa.

Hivi ni Bunge gani kila kukicha linatafuta vifungu kwenye Katiba ili livifute ili kuendelea kujilimbikizia madaraka??

Hivi kwa Spika kujiwekea kinga ya kutoshitakiwa, si kama kajiweka sawa na muumba!
 
Ndugai amejisahau Sana. Anavunja katiba kupendelea chama chake bila aibu. Kama hili la kuamuru wabunge waliojiuzulu kuendelea na ubunge ni ajabu Sana.

Yaani kwa sasa ndugai yupo juu ya Katiba!

Hivi, hakuna sheria ya kuwajibisha mtu anayevunja Katiba ya nchi??!
Na nchi hii sijui kwa nini imekosa watu aisee, ndugai hapaswi kuendelea kunyang'anyana oxygen na Sisi! Kanatakiwa kafanyiwe pyu pyu pyu pyu!!
 
Back
Top Bottom