BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,983
Ndoa zawagawa wabunge
Imeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 4th November 2009 @ 09:14
Habari Leo
MBUNGE wa Kibakwe, George Simbachawene, amesema, kumzuia mtoto mwenye umri wa miaka 14 au 15 kuolewa kama yupo tayari kuhimili mikiki mikiki ya ndoa ni kumnyima haki yake ya msingi.
Simbachawene amesema, si busara kumzuia mtoto kuolewa baada ya kuhitimu elimu ya msingi kwa kuwa si wote wenye malengo ya kuendelea na elimu.
Mbunge huyo amesema, wapo watoto wenye umri wa miaka 16, ni mabinti wazuri wenye sifa za kuolewa. Kwa mujibu wa Mbunge huyo, jambo la msingi si kumzuia mtoto asiolewe, bali uthibitisho wa daktari kuwa anaweza kuingia kwenye taasisi hiyo.
Simbachawene amesema, watoto wa kike wanakua haraka, hivyo wakiwa tayari kuolewa, wazazi washirikishwe ili wapate haki ya ndoa.
Ameyasema hayo bungeni wakati anachangia muswada wa Sheria ya Mtoto wa mwaka 2009 unaohitimishwa leo.
Mbunge wa Viti Maalum, Suzan Lyimo, amesema, suala la umri wa kuolewa si la msingi kwa kuwa kuingia katika taasisi hiyo au kutoingia ni uamuzi wa mtu kwa kuzingatia mazingira husika.
Mbunge wa Viti Maalum, Martha Mlata, amehoji, mtoto anayeolewa akiwa na umri wa miaka 14 au 15 anafuata nini huko?
Kwa mujibu wa Mbunge huyo, kumruhusu mtoto mwenye umri huo aolewe ni sawa na kuruhusu watoto waoane.
"Hivi unategemea nini akiwa leba… Ni ugonjwa huo kwamba anaenda kutibiwa?" amehoji Mbunge huyo wakati anachangia Muswada wa Sheria ya Mtoto wa mwaka 2009.
"Mimi nakataa kabisa, na napinga sana" amesema Mbunge huyo na kupendekeza kuwa mtoto aolewe akifikisha umri wa miaka 18.
Mbunge wa Viti Maalum, Diana Chilolo, amepinga kuruhusu watoto kuolewa na hasa wanapoolewa na wazee.
Imeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 4th November 2009 @ 09:14
Habari Leo
MBUNGE wa Kibakwe, George Simbachawene, amesema, kumzuia mtoto mwenye umri wa miaka 14 au 15 kuolewa kama yupo tayari kuhimili mikiki mikiki ya ndoa ni kumnyima haki yake ya msingi.
Simbachawene amesema, si busara kumzuia mtoto kuolewa baada ya kuhitimu elimu ya msingi kwa kuwa si wote wenye malengo ya kuendelea na elimu.
Mbunge huyo amesema, wapo watoto wenye umri wa miaka 16, ni mabinti wazuri wenye sifa za kuolewa. Kwa mujibu wa Mbunge huyo, jambo la msingi si kumzuia mtoto asiolewe, bali uthibitisho wa daktari kuwa anaweza kuingia kwenye taasisi hiyo.
Simbachawene amesema, watoto wa kike wanakua haraka, hivyo wakiwa tayari kuolewa, wazazi washirikishwe ili wapate haki ya ndoa.
Ameyasema hayo bungeni wakati anachangia muswada wa Sheria ya Mtoto wa mwaka 2009 unaohitimishwa leo.
Mbunge wa Viti Maalum, Suzan Lyimo, amesema, suala la umri wa kuolewa si la msingi kwa kuwa kuingia katika taasisi hiyo au kutoingia ni uamuzi wa mtu kwa kuzingatia mazingira husika.
Mbunge wa Viti Maalum, Martha Mlata, amehoji, mtoto anayeolewa akiwa na umri wa miaka 14 au 15 anafuata nini huko?
Kwa mujibu wa Mbunge huyo, kumruhusu mtoto mwenye umri huo aolewe ni sawa na kuruhusu watoto waoane.
"Hivi unategemea nini akiwa leba… Ni ugonjwa huo kwamba anaenda kutibiwa?" amehoji Mbunge huyo wakati anachangia Muswada wa Sheria ya Mtoto wa mwaka 2009.
"Mimi nakataa kabisa, na napinga sana" amesema Mbunge huyo na kupendekeza kuwa mtoto aolewe akifikisha umri wa miaka 18.
Mbunge wa Viti Maalum, Diana Chilolo, amepinga kuruhusu watoto kuolewa na hasa wanapoolewa na wazee.