Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,116
Kim Kardashian hatimaye ametalakiana rasmi na mume wake YE aliyejulikana kama Kanye West baada ya ndoa yao kudumu kwa miaka minane.
Katika uamuzi wa mahakama uliotolewa kupitia njia ya video nyota huyo pia ameondoa jina la West kutoka katika jina lake la Kim Kardashian West na kuwa Kim Kardashian.
Kardashian, ambaye aliwasilisha ombi la talaka na rappa huyo December mwaka uliopita. Hata hivyo wawili hao sasa watalazimika kusuluhisha ugawanaji wa mali na malezi ya Watoto wao wanne.
Pia soma:
Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian inakimbilia kwenye talaka
Kim Kardashian aomba talaka kutoka kwa Kanye West baada ya miaka 6 na nusu ya ndoa
Chanzo: BBC