Black Rose, Faiza Foxy,Topical,
..je asiye Muislamu anaruhusiwa kuwa hakimu ktk mahakama ya Kadhi?
..je wanawake wanaruhusiwa kuwa mahakimu ktk mahakama ya Kadhi?
Kwa mtizamo na ujinga wako ndio tutaendelea kudharauliwa tu.
Amka wewe!! Inferiority complex is not my nature and it will never be.
Bahati mbaya sana waislam waelewa na wasomi mara nyingi wanakaa kimya hawasemi wanaachia wajinga kama wewe wakurupuke na kutufanya siye wote tuonekana mazuzu.
Muda umefika to put a stop to this nonsense! itafika siku watu kama wewe tutawazuia kufungua midomo yenu msiendelee kutuaibisha.
Mod mmoja humu JF ana signature inasema hivi:
FICHA UPUMBAVU WAKO, USIIFICHE HEKIMA YAKO!
Hayo maneno yako tu yanazidi kukuweka mbali na uislam..hahahaha, katonta bana, haya endelea kumwagwa uharo wako! Wewe ndiyo muislamu mwenyewe hakuna kama wewe humu JF
Wewe ni umejiunga juzi JF umeishajua kama Invisible ni Mod..hahahahahah!!!
Hewala! Mimi maneno yangu yenye staha, yanazidi kuniweka mbali na usilam,ila yako ya matusi ndio yanakuvuta karibu!
Huu ndio upeo wa akili yako nakusamehe.
Ndugu yangu,Ninakuelewa unachokisema.Hapo kwenye bold, mko wangapi hadi mqualify kuwa na hiyo mahakama na itoe haki bila kuumiza wengine?Nakupata vizuri sana.Sijui ushajaribu kujishughulisha kujua nini kinatokea huko Kenya ambapo kuna mahakama ya Kadhi tena kikatiba?
Kenya , Mahakama ya Kadhi ilianzishwa kwa makubaliano baina ya late Kenyatta, rais wa Kwanza wa Kenya, na Sultan wa Zanzibar for a 10 mile coastal strip ambayo ilikuwa incorporated kwa Republic of Kenya at independence.Utaona dhahiri hii ilikuwa ni "biashara" na siyo utashi wa kisiasa ( political will and commitment).Moja ya central arguments kwa waliokuwa wana advocate for Kadhi courts ziingizwe kwenye hii Katiba yao mpya ni kwamba hizi mahakama zilikuwepo kwenye Katiba ya Kenya since independence.Nadhan hata Waislam wa Tanzania wanatumia hii argument bila hata kujua chanzo cha hizo mahakama kuwemo kwenye mfumo wa Kenya.Basi mngejibidisha kujua hizo mahakama zimekuwa zinafanyaje kazi huko Kenya kabla ya kudai ziingie kwenye mfumo huku Tanzania.
Mwaka jana 2010 December, League of Muslim Women of Kenya (LMWK) lilifanya tathmini kwa kuwaita kwenye dialogue wanawake wa Kiiislam, waje watoe uzoefu wao katika kuzitumia mahakama za Kadhi courts, na pia kujifunza kutoka kwa administrators wa hizo mahakama kuhusu role and mamlaka (jurisdiction) ya hizi mahakama. Mkutano huo ulihudhuriwa na panel ya makadhi wanne, walioongozwa na Sheikh Ahmed Mohdhar, ambaye alikuwa Acting Chief Kadhi na Kadhi wa Nairobi.Nitawanukulia yaliyojiri kwenye ule mkutano kama ifuatavyo:
The Kadhis took time to explain to the women the workings of the Kadhis courts and responded to concerns and questions raised by the women. The participants shared their experiences using the courts including challenges they encountered in attempting to access justice. A number of critical issues emerged on the problems that women encounter in accessing justice through the Kadhis courts. Among the challenges identified by the women were :
Sasa nyie mnataka haya matatizo nayo yaje Tanzania kwanini?
- lack of information about the location of the Kadhis courts,
- discriminatory practices and lack of public relation skills among some court clerks, and
- lack of finances to pay court fees.
- The women also cited the shortage of court process servers which often resulted in them (women) having to personally effect service on the defendants who in most cases would be their estranged husbands. As one participant observed: The idea of having to ask a woman who has filed a case to go and serve papers to a person they are accusing makes it difficult for the case to commence, for in most cases it is hard to serve the papers.
- The women further mentioned the lack of female Kadhis and courts clerks as another barrier to access to justice.
- They mentioned that discussing matters involving pertinent personal issues was difficult and at times embarrassing as all the officers in the Kadhis courts were male.
Umesema vema kwamba wanawake wanaotaka kutumia mahakama za State wawe huru. Kuna point hujaizungumzia.UWEPO WA OPTIONS NYINGI ndani ya mfumo wa utoaji haki.Tanzania kama nchi nyingi za Kiafrika zenye Waislamzilivyo, bado zina tatizo hili na ndio maana hata zikiwepo Kadhi Courts hazileti maana kama ilivyokusudiwa.Watu bado wanakimbilia jadi/mila zao katika mambo yao ya maisha hata kama ni waislam.Sasa hivi Tanzania hali ndiyo ilivyo.Utafiti wangu umenionyesha kwamba, mahakama hizo za State nazo zinatoa option - kutumia sheria za dini, mila au state. Kwa waislam, huenda tatizo ni kukosekana waamuzi huko mahakama walio na ueledi wa sheria za kiislam.Nadhani tungeanzia hapo kuimarisha weledi.
Wakatabahu,Blackie
[/LIST]Duh.. unajua siku hizi mbili umenifanya nifikirie kweli. Maana muda wote ambao tumekuwa tunazungumzia "kadhi" miye mawazoni namuona mbaba fulani akiwa hivyo. Swali ni je, wanawake Waislamu wa Tanzania wanajua wanayo haki ya kuwa kadhi?
Black Rose,
..asante kwa majibu yako.
..je, according to QURAN, kuna nafasi yoyote ile ya uongozi ambayo mwanamke hapaswi kushika??
Bibie, umeeleza vizuri sana niseme nimeona point mbili kwenye hii habari niliyo quote:
1. Kwamba waislamu wahangaike sana na kuwa waadilifu kwanza na wapatikane wengi nafikiri unakosea kusubiri hali hiyo kutokea kwasababu waislamu kama watu wengine wengi wanaweza kupenda dunia kuliko ahera sasa sisi tunaotaka ibada zetu hatuwezi kuwasubiri maana hilo kwa mazingira yaliyopo lina changamoto nyingi..na ujue kuwa mchaMungu ni choice..kwa hoja hiyo ni dhaifu hata kama tuko wachache tupewe haki yetu ya mahakama ya kadhi
2. Umeonyeonyesha uzoefu wa kenya, well sitegemei kwamba mahamaka ya kadhi isiwe na changamoto kokote duniani, zinaweza kuwepo changamoto za weledi, fedha nk. lakini bila kuanza jambo utakaogopa changamoto hadi lini??
Nafikiri hoja ya kuogopa ni mbaya zaidi ni afadhali kuanza na kujifunza na kurekebisha changamoto kila siku kama ilivyo taasisi yeyote ile
Mkuu vipi tena sentesi za namna hii? wewe unadhani wake zetu, dada zetu hawafahamu haki zao kwanini? waislamu wanawake wanajua haki zao kwakuwa haki hizo hazitoki kwa kadhi ila kwenye kitabu kitakatifu (qura'n na sunna)..
Kwahiyo naomba usijidai unawajali sana wake zetu, dada zetu wakati wewe tunafahamu uko upande gani kwenye dini??
Mimi si mwelewa sana wa mambo ya Sharia Dada Black Rose lakini nasikia kuwa katika dini hii wanawake wanawekwa nafasi ya chini sana, yaani wanaume wanakuwa favored kuliko wanawake (sijui kama ni kweli) lakini kama ni kweli je haiwezekani kuwa mahkama hii itakuwa ni hatari kwa wanawake hawa?
Natanguliza samahani zangu kwanza pale nitakapokuwa nimewakosea)
Hapana mpendwa.Dini yetu ya Islam ni dini ya amani na haki.
Mwanamke katika Uislam, ana haki zake na siyo kama watu wanavyoamini.Hayo mengine ni utamaduni, ustaarabu na hata utashi wa wale wanaomzunguka.Yatosha tu kusema kuwa "uonevu" unaoonekana kutendewa wanawake siyo maagizo au maamrisho ya Kuraan! Ukiisoma hii mada na michango iliyomo utaona tatizo siyo Uislam bali ni watu ndani ya Uislam.Hawa watu ndio watakuwa kikwazo kwa haki za wanawake kuanzia majumbani hadi watakapofikishana huko kwa Kadhi.
tatizo lako unafikiri Waislamu wako kwenye familia yako au yenu peke yako. Hauwezi kabisa kufikiria labda watu kama miye tuna wadogo zetu walioingia Uislamu au wameolewa na Waislamu! Na tunapozungumzia "Waislamu" tunazungumzia ndugu zetu wenyewe!
BR.. inakuwaje
a. Ambapo mwanamke ni Mkristu na mke ni Muislamu na yule Mke anataka kutafuta haki kwa kutumia Kadhi na mume Mkristu hatambui mamlaka ya kadhi?
b. Mwanamme ni Muislamu na mwanamke ni Mkristu na mume anataka mahakama ya kadhi ndio iamue mambo ya ndoa wakati mwanamke anataka Mahakama ya Kanisa iamue (chukulia kesi ya kwanza ndoa ilifungwa Kikristu, na pili ndoa ilifungwa Kiislamu). Huyu mwanamke atalindwa vipi?
c. Watoto ni Wakristu na wazazi Waislamu na hoja ni mirathi. Inakuwa vipi hapo?
Asante.
Asante kwa mawazo yako mazuri. Ni kweli unavyosema kuwa wale wachache waadilifu wanajiskia kuhitaji chombo chao waweze kujiskia kamili kwenye masuala ya imani.
Tuendelee kuchambua na kuelimishana.Nadhani hadi sasa kuna wenzetu wanajifunza moja au mawili kutoka kwetu.
Nimependa has point yako niliyoikoleza wino (BOLD) kwamba changamoto zisiogopwe bali zitafutiwe jinsi ya kukabiliana nazo. Kuna wenzetu wao wanadhani hakuna changamoto. Na hata wakajaribu kutoa mfano wa Kenya.Na ndio maana nikaweka mfano huo na changamoto zake.
Mkuu japo hujaniuliza na wengine wanaweza kunisaidia kama wana ufahamu
a +b: Jibu lake ni kuwa ndoa kati ya mke mkiristo na mume muislam kuna school of thought mbili; kuna wale wanaoamini kuwa ndoa hiyo ni halali kwakuwa wanawake wa kikristo na kiyahudi ni halali kwa waislamu kwakuwa wanamuamini Mungu moja; kuna wale wanaosema wanawake wa kikristo si halali kwakuwa wanaamini mungu watatu lakini wakiyahudi ni halali. wanazuoni wanaoendesha mahakama ya kadhi inabidi wakaubaliane kwanza wafuate which school of though in rule accordingly;