mama D
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 19,760
- 35,212
Mathematical Equation hii kitu ni ngumu sana. Nilishangaa kuona hadi sasa mume akifa ati watoto wanamdai mama yao urithi. Tena kama mama alijenga nyumba na mumewe wanauza nyumba bila kujali Yule mama ataishi wapi wanagawana pesa, tena unakuta pesa yenyewe kidogo haitoshi hata kupata kibanda. Wanasepa na mama anaanza kuhangainga pa kukaaIpo hivi watu wakifunga ndoa hutangazwa kuwa ni Mwili mmoja, au kitu kimoja, kwa maana maamuzi sasa yanataka concer ya wote wawili.
Lakini mwanamke akifa kwenye ndoa, na mwanaume akiwa hai, hakutakuwa na ugomvi wa mali, kwa kuwa mali hazitakuwa na mpango wa kuganywa.
Lakini akifa mwanaume basi kila kitu kitagawanya hata kama mwanamke yuko hai
Hii inaonyesha kwamba wanandoa sio mwili mmoja ndo maana akifa mwanaume kuna kuwa na shida na sio mwanamke, au mwanamke sio sehemu kuu ya ndoa.
Hili ni kosa kubwa na huwa linawaumiza sana wanawake hasa walioshindwa kupata watoto katika ndoa zao.
Hapa natoa wito kwa ustawi wa jamii kuangalia swala hili ili iwe hata mirathi isiandikwe na mwanaume, bali iandikwe na wanandoa kwa umoja wao. Ili kutoa mamlaka kwa mtu mmoja huku mnasema kuwa wao ni kimoja.
Nawasilisha
Mwanzoni nilijua ni nje ya utaratibu wa kisheria nikamwambia mama mmoja hawezi kunyanyasika na mali yake aliyochuma na mume wake heri aende mahakamani. Kufika huko akaambiwa either akakubaliane na watotohuwe wamhifadhi au nyumba iuzwe
Dah hapa ndio naiona siasa na upotoshaji ulioko kwenye hii kitu wanayoiita haki. Yaani miaka yote wanawake tumekomaa kudai haki sawa, tumeenda hadi Beijing, tumepewa hadi nafasi za juu serikalini lakini tukifiwa na waume mashemeji, wakwe na watoto wana haki ya kuuza mali tulizochuma na wenza wetu