Ndoa na Mirathi inawaumiza Wanawake

Ipo hivi watu wakifunga ndoa hutangazwa kuwa ni Mwili mmoja, au kitu kimoja, kwa maana maamuzi sasa yanataka concer ya wote wawili.

Lakini mwanamke akifa kwenye ndoa, na mwanaume akiwa hai, hakutakuwa na ugomvi wa mali, kwa kuwa mali hazitakuwa na mpango wa kuganywa.

Lakini akifa mwanaume basi kila kitu kitagawanya hata kama mwanamke yuko hai

Hii inaonyesha kwamba wanandoa sio mwili mmoja ndo maana akifa mwanaume kuna kuwa na shida na sio mwanamke, au mwanamke sio sehemu kuu ya ndoa.

Hili ni kosa kubwa na huwa linawaumiza sana wanawake hasa walioshindwa kupata watoto katika ndoa zao.

Hapa natoa wito kwa ustawi wa jamii kuangalia swala hili ili iwe hata mirathi isiandikwe na mwanaume, bali iandikwe na wanandoa kwa umoja wao. Ili kutoa mamlaka kwa mtu mmoja huku mnasema kuwa wao ni kimoja.

Nawasilisha
Mathematical Equation hii kitu ni ngumu sana. Nilishangaa kuona hadi sasa mume akifa ati watoto wanamdai mama yao urithi. Tena kama mama alijenga nyumba na mumewe wanauza nyumba bila kujali Yule mama ataishi wapi wanagawana pesa, tena unakuta pesa yenyewe kidogo haitoshi hata kupata kibanda. Wanasepa na mama anaanza kuhangainga pa kukaa

Mwanzoni nilijua ni nje ya utaratibu wa kisheria nikamwambia mama mmoja hawezi kunyanyasika na mali yake aliyochuma na mume wake heri aende mahakamani. Kufika huko akaambiwa either akakubaliane na watotohuwe wamhifadhi au nyumba iuzwe

Dah hapa ndio naiona siasa na upotoshaji ulioko kwenye hii kitu wanayoiita haki. Yaani miaka yote wanawake tumekomaa kudai haki sawa, tumeenda hadi Beijing, tumepewa hadi nafasi za juu serikalini lakini tukifiwa na waume mashemeji, wakwe na watoto wana haki ya kuuza mali tulizochuma na wenza wetu
 
Nadhani umeandika mada yako kwa kutazama past experiences na historia ya matukio ya wajane kunyanyaswa.

But kwa hali ilivyosasa hizo situation ni very rare kutokea sababu ya elimu juu ya unyanyasaji wa ndugu za marehemu kwa watoto na mke wa marehemu.

Ila umeongelea upande m'moja, je umeshaona ndoa ya mwanamke mwenye pesa akifariki ndugu wa mke wanavyomjia juu mwanaume?!
Ndugu unaishi kwa beberu! Africa mume akishakufa, ndugu zake wanafuata chao, awe tajiri awe maskini, mke atanyang'anywa mpaka shuka.

Nenda mahakama za mwanzo Tanzania yote, angalia kesi zilizopo nyingi ni za mirathi. Hao kwa wale walioenda mahakamani kuna wale vijijini wanatumia mabaraza.

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Mathematical Equation hii kitu ni ngumu sana. Nilishangaa kuona hadi sasa mume akifa ati watoto wanamdai mama yao urithi. Tena kama mama alijenga nyumba na mumewe wanauza nyumba bila kujali Yule mama ataishi wapi wanagawana pesa, tena unakuta pesa yenyewe kidogo haitoshi hata kupata kibanda. Wanasepa na mama anaanza kuhangainga pa kukaa

Mwanzoni nilijua ni nje ya utaratibu wa kisheria nikamwambia mama mmoja hawezi kunyanyasika na mali yake aliyochuma na mume wake heri aende mahakamani. Kufika huko akaambiwa either akakubaliane na watotohuwe wamhifadhi au nyumba iuzwe

Dah hapa ndio naiona siasa na upotoshaji ulioko kwenye hii kitu wanayoiita haki. Yaani miaka yote wanawake tumekomaa kudai haki sawa, tumeenda hadi Beijing, tumepewa hadi nafasi za juu serikalini lakini tukifiwa na waume mashemeji, wakwe na watoto wana haki ya kuuza mali tulizochuma na wenza wetu
Absolutely right!
Nimeshuhudia kesi, watoto wanashitaki nyumba imeuzwa bila watoto kushirikishwa, unashangaa nyumba ya wazazi au watoto?? Ninaposema watoto ni mibaba na mimama iliyokomaa na ina maisha.

Cha msingi ni kuandika fair will, wosia unaachwa kwa wanasheria, ambao nao unaweza kupingwa mahakamani vilevile.

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Mathematical Equation hii kitu ni ngumu sana. Nilishangaa kuona hadi sasa mume akifa ati watoto wanamdai mama yao urithi. Tena kama mama alijenga nyumba na mumewe wanauza nyumba bila kujali Yule mama ataishi wapi wanagawana pesa, tena unakuta pesa yenyewe kidogo haitoshi hata kupata kibanda. Wanasepa na mama anaanza kuhangainga pa kukaa

Mwanzoni nilijua ni nje ya utaratibu wa kisheria nikamwambia mama mmoja hawezi kunyanyasika na mali yake aliyochuma na mume wake heri aende mahakamani. Kufika huko akaambiwa either akakubaliane na watotohuwe wamhifadhi au nyumba iuzwe

Dah hapa ndio naiona siasa na upotoshaji ulioko kwenye hii kitu wanayoiita haki. Yaani miaka yote wanawake tumekomaa kudai haki sawa, tumeenda hadi Beijing, tumepewa hadi nafasi za juu serikalini lakini tukifiwa na waume mashemeji, wakwe na watoto wana haki ya kuuza mali tulizochuma na wenza wetu
Kwa sababu hii tuna haja ya kuwaamsha Dawati la Jinsia, Ustawi wa jamii, na wanasheria wanaoshughulikia maswala ya kike wajue kuwa kuna shida na ndio sababu wamama ndio wanaongoza kuumiza kwa sababu ya mila au sheria mbovu zilizoko

Kabla ya kuraise sauti kwenda mbali tuanze na hiki

suggestion, hakuna kugawa mirathi au hakuna urithi hadi wanandoa wote wafariki, akifa mmoja aliyebaki ataendelea kumiliki kihalali
 
Absolutely right!
Nimeshuhudia kesi, watoto wanashitaki nyumba imeuzwa bila watoto kushirikishwa, unashangaa nyumba ya wazazi au watoto?? Ninaposema watoto ni mibaba na mimama iliyokomaa na ina maisha.

Cha msingi ni kuandika fair will, wosia unaachwa kwa wanasheria, ambao nao unaweza kupingwa mahakamani vilevile.

Everyday is Saturday................................:cool:
Hii kitu imekaa vibaya sana. Yaani mali yangu mwenyewe nimetafuta na mume wangu mtoto anishtaki ili nisiuze😎😎
 
Hii kitu imekaa vibaya sana. Yaani mali yangu mwenyewe nimetafuta na mume wangu mtoto anishtaki ili nisiuze😎😎
Bora awe na umri wa miaka 17 kuelekea chini, ni watu wazima, 30+, wanadiriki kusimama mahakamani na kunyoosheana vidole, aisee! Wanakuwa maadui, familia inasambaratika!

Na huko mahakamani nako ni drama tupu, hakuelewekagi ni appeals mpaka wanajikuta wapo, mahakama ya rufaa.

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
...........Mimi nadhani pia uelewa wa jamii husika pamoja na uvivu huchangia pakubwa tatizo hili.

Early 2002 marehemu mjomba angu alitengana na mkewe kwa sababu walizozijua wao mke akaondoka alikojua yeye,uncle akafariki 2006 tumefanya msiba baada ya maziko mkewe akasema anarudi kwenye nyumba yake kuendelea na maisha yake na watoto wake hakuna ktk ndugu hata mmoja aliyesema japo kwa kunong'ona kwamba asiruhusiwe.

Aliwahi fariki rafiki yake jamaa yangu (mtu kutoka kusini alikuwa zamani mchezaji wa bandari Mtwara na alihisiwa na ndugu zake kama aliyeshafanikiwa) ndugu wakaanza kugombania vitu mwili wa marehemu ukiwa bado mle chumbani alimofia na jamaa hakuwa hata na mali za maana alikuwa amepanga chumba kimoja maeneo ya Kurasini ila kiligombaniwa mpaka kijiko na ndugu walienda mbali mpaka kufikia kuushusha mwili wake kitandani alikofia wakauweka chini wagawane na kitanda,kipindi hiko nilikuwa mgeni wa mambo haya ila niliona ni jamii moja ya kipumbavu kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ipo hivi;

Mnapooana, mali mnazopata kwa kushirikiana hizi zinaitwa mali za familia/ndoa (matrimonial properties), hizi ni mali zinazomilikiwa na wanandoa kwa kuwa walishirikiana katika upatikanaji ama uchumaji wa hizo mali, humilikiwa kwa uwiano, labda asilimia 50 kwa 50 au 10 kwa 90 nk, yaani humilikiwa kutokana na kiwango cha uchangiaji wa mali hiyo kwa kila mwanandoa. Inapotokea mgogoro uhusuo mali hizi, kila mwanandoa hupaswa kuonesha ni namna gani na kwa kiasi kipi alishiriki uchumaji/upatikanaji wa mali hizo.

Hizi matrimonial properties hazihusiki chochote na watoto, ni mali za wanandoa tu, watoto si wanandoa. Mwanandoa mmoja anapokufa, mali hii hubaki kuwa ya wanandoa (yaani ya marehemu na mwenza wake aliyebaki) kwa uwiano uleule waliomiliki mali. Kama marehemu alikuwa na wosia, basi mgawo wa mali alitakiwa kugawa mali hiyo kwa sehemu tu ya alichokuwa anamiliki katika mali hiyo, mfano kama nyumba ilimilikiwa nae kwa asilimia 50, basi wosia wake utagawa mali yote aliyomiliki (asilimia 50) kwa warithi wake, ambapo mke na watoto na wazazi wa marehemu au hata watu wengine watakuwa ndio wanufaika. Mfano nyumba ina vyumba 4, uwiano wa umiliki ni 50% kwa 50% basi mali ya marehemu hapa ni vyumba 2, hivi tu ndiyo vinapaswa kujadiliwa katika mirathi, viwili vingine ni mali ya mwanandoa aliyebak. Izingatiwe kuwa huyu mke aliyebaki naye atastahili kupata sehemu ya hivyo vyumba 2 vya marehemu ukiachana na vile vyumba vyake viwili vya nyumba hiyo.


Marehemu kama hakuacha wosia juu ya mgawo wa mali yake basi ndipo mtu huomba mahakama imteue kuwa msimamizi wa mirathi ya mali za marehemu, napo ni kwa asilimia 50 tu ya mfano. Kutokana na familia zetu kutopenda kuwa na wanasheria wa familia au hata wa kutoa huduma wakati wa tukio tu, basi familia hizi pindi anapokufa baba huamua kujadili mali za familia kama mali za marehemu pekee kwa ukamilifu, mfano nyumba nzima huonekana kama ni ya mrehemu pekee. Matokeo yake mjane hujikuta anaporwa mali anayomiliki au hupewa sehemu anayomiliki tayari, yaani unamiliki gari halafu mtu anasema wewe tunakupa gari hili kama mirathi yako. Hili ni kosa japo sio la kisheria lakini hufanya mgawanyo mzima kuwa batili.

NINI KIFANYIKE?
  1. Familia zijizoeshe kuwa na wanasheria wa familia, wataokuwa wanawashauri mambo ya kisheria wakati wote. Mnaweza hata kukubaliana nae mkawa mnalipa fedha ndogo tu, mfano shilingi elfu 50 kwa mwezi (kwa kuzingatia uchumi wetu wa kati) kwa mambo yasiyokuwa kesi mahakamani, hii itawasaidia sana kwa mambo mengi ikiwa ni pamoja na wanafamilia kupata uelewa wa mambo kama haya.
  2. Wanandoa wanapochuma mali pamoja waziandike katika wosia wa pamoja (mutual /joint will) , wosia ambao automaticaly humpa umiliki wa mali za familia mwanandoa hai aliyebaki pale mwenza wake anapofariki dunia na zaidi wosia huu humfanya mwanandoa aliyebaki kushindwa kubadilisha chochote katika wosia huo, hivyo hbaki kama walivyokubaliana na marehemu.
  3. Serikali kama itabadilisha mtaala wa elimu, basi izingatie kuweka iweke hata kwa ngazi ya uelewa wa msingi (basics) elimu ya mambo haya ya ndoa na mirathi maana ndiyo tunayokutana nayo kila siku katika maisha yetu.

Sajo
 
Migogoro ya mirathi siyo maingizo mapya bali ni mwendelezo wa migogoro ya ndoa husika. Kama wanandoa walikuwa na migogoro ya chini kwa chini hiyo migogoro itadhihirika pia kwenye mirathi. Lakini kama ndoa ilikuwa na amani na kila upande basi hata mirathi haitasumbua.
 
Hivi mahali huwa inawakilisha nini katika ndoa.kama mnahitaji haki sawa basi ifikie hatua sasa binti kwanza atafute maisha akishaona angalau anaweza kuwa na mwenza aanze kumtafuta sio asubirie atafutwe yeye.
Ikiwezekana hivyo,basi kila kitu kitawezekana.ila kiuharisia tunaongozwa na mfumo,huwezi pingana na mfumo.
Vilevile jiulizeni,kwanini watoto mnaowapata katika ndoa zenu,mnawaita majina hasa kufata ukoo wa baba.
Mambo mengine c ya kufosi,hamsomi maandiko matakatifu juu ya nafasi ya mwanamke?.
Mnatuchosha bhana.
 
Umewasilisha vema Mkuu.
Ila mwanaume ni kichwa cha familia kwa hiyo akifa mwanamke bado mwenye jukumu la kulinda familia anabaki kuwa mwanaume na hii inamfanya kuendelea kubaki msimamizi na mlinzi wa familia.
Sidhani kama nimekuelewa vizuri.
Naomba kuwasilisha
Sasa mbona sheria inasema mali ni za wanandoa.
Kama unabisha nunu nyuma usimuusishe mke wake afu uwone baadae.
 
Back
Top Bottom