nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]JUMATANO, JULAI 25, 2012 04:45 GABRIEL MUSHI NA MARIAM AYUBU
ALIYEKUWA mgombea ubunge Jimbo la Moshi Mjini kupitia chama cha NCCR Mageuzi, Faustine Sungura, amezidi kumkaba koo Mbunge wa jimbo hilo, Philemon Ndesamburo (CHADEMA) baada ya kumshitaki kwa Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Kin-Moon.
Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Moshi kutupilia mbali madai ya kesi yake aliyoifungua Desemba, 2010, kupinga uteuzi wa waliokuwa wagombea wenzake katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Sungura ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Kampeni na Uchaguzi za chama hicho, alisema ameamua kuchukua hatua hiyo kwa sababu aliyekuwa jaji wa kesi yake amemuonea.
Alisema aliyekuwa jaji wa kesi hiyo, Jaji Moses Mzuna, aliiendesha kesi yake kwa upendeleo, kinyongo lakini pia kinyume cha sheria.
Baada ya tume ya uchaguzi kuwateua wagombea wenzangu katika Jimbo la Moshi Mjini mimi sikuridhika nao, nikaweka pingamizi zangu ambazo zilitupiliwa mbali na Tume hiyo na kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi nilifungua shauri N0 1/2010 la kesi ya uchaguzi dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Philemon Ndesamburo.
Aidha kutokana na ukiukwaji wa sheria katika kesi hii, Julai 12, 2010, nilifungua maombi namba 39/2010 juu ya kiasi cha dhamana ya kulipa mahakama au kusamehewa kulipa dhamana yoyote, kwa kuwa ukifungua kesi unatakiwa kulipa dhamana ya shilingi milioni nane au kuandika mali zenye thamani ya vitu visivyopungua milioni tano.
Mara baada ya mahakama kuridhika kuwa sina fedha, Jaji Mzuna alitoa uamuzi akinieleza kuchangisha fedha ndani ya siku 14 kutoka kwa marafiki zangu, ingawa uamuzi huo ulikuwa ni kinyume cha sheria.
Kwa kuwa sikuridhishwa na uamuzi huo, niliwasilisha tena maombi yangu na kupewa namba 11/2012 lakini pasipo halali na wala sheria, Jaji alitolea uamuzi maombi hayo bila kusikiliza na kuyafukuza makamani, hii ni kinyume cha ibara ya 13 (6) (a) ya Katiba ya nchi.
Kutokana na hali hiyo Januari 6, mwaka huu wadaiwa wangu walipokea hati ya wito kuwasilisha nyaraka mahakamani na walitakiwa kusajili nyaraka zao kabla ya Januari 28, mwaka huu lakini badala yake walisajili Mei 9, mwaka huu ambapo pia mimi nilipewa nakala ya hati hiyo na kuipitia.
Hata hivyo baada ya kugundua ina makosa nililipia ada ya ukaguzi na kukagua jalada la Ndesamburo na kukuta hati ya kiapo kinzani, pia ina makosa na kuifungulia pingamizi la hati yake, lakini baada ya mahakama kugundua hilo ilimuita na kumtaka akale kiapo kwa wakili kukamilisha hati yake na kuirudisha siku hiyo hiyo ya Mei 9, mwaka huu.
Lakini aliirudisha Mei 10 na mahakama kusikiliza pingamizi hilo na kunituhumu kuwa nimeghushi nyaraka hizo kwa sababu zilizopo mahakamani zinadai Ndesamburo alirudisha hati ya kinzani Mei 9, lakini niliyokuwa nayo mimi inasema alirudisaha Mei 10, mwaka huu, alisema.
Alisema kutokana hali hiyo, ameamua kulishughulikia suala hilo kwa mbinu za kiutawala zaidi kwa kumuandikia barua Rais Kikwete na Katibu Mkuu wa UN, TAKUKURU, kwa IGP Mwema, LHRC, Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kwa ajili ya kuchunguza zaidi sakata hilo na kujionea namna alivyoonewa.
ALIYEKUWA mgombea ubunge Jimbo la Moshi Mjini kupitia chama cha NCCR Mageuzi, Faustine Sungura, amezidi kumkaba koo Mbunge wa jimbo hilo, Philemon Ndesamburo (CHADEMA) baada ya kumshitaki kwa Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Kin-Moon.
Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Moshi kutupilia mbali madai ya kesi yake aliyoifungua Desemba, 2010, kupinga uteuzi wa waliokuwa wagombea wenzake katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Sungura ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Kampeni na Uchaguzi za chama hicho, alisema ameamua kuchukua hatua hiyo kwa sababu aliyekuwa jaji wa kesi yake amemuonea.
Alisema aliyekuwa jaji wa kesi hiyo, Jaji Moses Mzuna, aliiendesha kesi yake kwa upendeleo, kinyongo lakini pia kinyume cha sheria.
Baada ya tume ya uchaguzi kuwateua wagombea wenzangu katika Jimbo la Moshi Mjini mimi sikuridhika nao, nikaweka pingamizi zangu ambazo zilitupiliwa mbali na Tume hiyo na kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi nilifungua shauri N0 1/2010 la kesi ya uchaguzi dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Philemon Ndesamburo.
Aidha kutokana na ukiukwaji wa sheria katika kesi hii, Julai 12, 2010, nilifungua maombi namba 39/2010 juu ya kiasi cha dhamana ya kulipa mahakama au kusamehewa kulipa dhamana yoyote, kwa kuwa ukifungua kesi unatakiwa kulipa dhamana ya shilingi milioni nane au kuandika mali zenye thamani ya vitu visivyopungua milioni tano.
Mara baada ya mahakama kuridhika kuwa sina fedha, Jaji Mzuna alitoa uamuzi akinieleza kuchangisha fedha ndani ya siku 14 kutoka kwa marafiki zangu, ingawa uamuzi huo ulikuwa ni kinyume cha sheria.
Kwa kuwa sikuridhishwa na uamuzi huo, niliwasilisha tena maombi yangu na kupewa namba 11/2012 lakini pasipo halali na wala sheria, Jaji alitolea uamuzi maombi hayo bila kusikiliza na kuyafukuza makamani, hii ni kinyume cha ibara ya 13 (6) (a) ya Katiba ya nchi.
Kutokana na hali hiyo Januari 6, mwaka huu wadaiwa wangu walipokea hati ya wito kuwasilisha nyaraka mahakamani na walitakiwa kusajili nyaraka zao kabla ya Januari 28, mwaka huu lakini badala yake walisajili Mei 9, mwaka huu ambapo pia mimi nilipewa nakala ya hati hiyo na kuipitia.
Hata hivyo baada ya kugundua ina makosa nililipia ada ya ukaguzi na kukagua jalada la Ndesamburo na kukuta hati ya kiapo kinzani, pia ina makosa na kuifungulia pingamizi la hati yake, lakini baada ya mahakama kugundua hilo ilimuita na kumtaka akale kiapo kwa wakili kukamilisha hati yake na kuirudisha siku hiyo hiyo ya Mei 9, mwaka huu.
Lakini aliirudisha Mei 10 na mahakama kusikiliza pingamizi hilo na kunituhumu kuwa nimeghushi nyaraka hizo kwa sababu zilizopo mahakamani zinadai Ndesamburo alirudisha hati ya kinzani Mei 9, lakini niliyokuwa nayo mimi inasema alirudisaha Mei 10, mwaka huu, alisema.
Alisema kutokana hali hiyo, ameamua kulishughulikia suala hilo kwa mbinu za kiutawala zaidi kwa kumuandikia barua Rais Kikwete na Katibu Mkuu wa UN, TAKUKURU, kwa IGP Mwema, LHRC, Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kwa ajili ya kuchunguza zaidi sakata hilo na kujionea namna alivyoonewa.