Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Abiria waliokuwa safarini kwenda Mwnza leo kwa ndege za 540 na Precision air wamekwamba uwanja wa ndege wa JNIA na hali ni mbaya.
Precision Air wamebadili ndege yao iliyokuwa iondoke saa 5 asubuhi (kwa kutumia ndege aina ya Boeng) bila taarifa na kusababisha usumbufu mkubwa sana kwa abiria. Baadhi yao wamehamishiwa kwenye ndege za saa 8.30 mchana na saa 12 jioni. Wakati huo huo, kuna abiria ambao wamecheleweshwa hadi kesho.
Jambo ambalo linakera sana ni kwamba wakubwa wa shirika hili hawapo ofisini kutoa majibu kwa abiria ambao wanateseka bila sababu.
Ndege ya 540 imekwama kuondoka toka jana na hadi sasa hakuna maelezo ya maana! Baadhi ya abiria wako airport hadi sasa!
Precision Air wamebadili ndege yao iliyokuwa iondoke saa 5 asubuhi (kwa kutumia ndege aina ya Boeng) bila taarifa na kusababisha usumbufu mkubwa sana kwa abiria. Baadhi yao wamehamishiwa kwenye ndege za saa 8.30 mchana na saa 12 jioni. Wakati huo huo, kuna abiria ambao wamecheleweshwa hadi kesho.
Jambo ambalo linakera sana ni kwamba wakubwa wa shirika hili hawapo ofisini kutoa majibu kwa abiria ambao wanateseka bila sababu.
Ndege ya 540 imekwama kuondoka toka jana na hadi sasa hakuna maelezo ya maana! Baadhi ya abiria wako airport hadi sasa!