Nchi iko Pabaya Sana: Watanzania tufanye nini?

Nyami2010

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
227
50
Wana Jamii

Nionavyo mimi, hali ya NCHI ni TETE kuliko tulivyozoea. Baadhi ya viashiria ni hivi hapa:

1. Hazina ni kweupe. Mhe. Waziri Mkuchika alibainisha hili, japo Serikali imekuwa ikipinga muda mrefu. Ona sasa Mhe. Rais analazimika kupunguza baadhi ya maafisa wake kwenye safari za nje
2. Bunge kwa namna moja au nyingine halina imani na Rais. Mhe. Spika alisema Rais amebariki posho za Waheshimiwa Wabunge, Ikulu ikakana. Kumbuka sakata la Jairo na Luhanjo
3. Viongozi wetu wameanza kupeana sumu....hadi wanaogopa kupeana mikono. Sakata la Mhe. Mwakyembe
4. Ndani ya vyama hakupikiki. Magamba ya CCM, Mhe. Kafulila, Mhe. Hamad.....
5. Uchumi umekufa:
-Mfumko wa bei ni takribani 20% leo....ukitoka 4% mwaka 2005.
-Serikali imeshindwa kutoa fedha za maendeleo kwenye halmashauri zote nchini, Waziri wa TAMISEMI amekiri hayo Bungeni jana.
-Serikali imeshindwa kununua vifaa vya tiba na kutoa viposho vidogo vidogo kwa madaktari
6. Hali ya Maisha miongoni mwa Watanzania tulio wengi ni mbaya sana X sana!
7. Serikali kupitia Waziri Mkuu imekubali kuwa imeshindwa kuwaletea wananchi maisha bora. Tazama gazeti la Tanzania Daima la leo tar 3 Feb 2012.
8. Viongozi wa Serikali wakiwemo Wabunge wanajitazama wao tu...., wanaacha raia tunakufa..........
9.....ongeza list

Hivi katika hali kama hii, watanzania twaweza kufanya nini? Ebu tupeane mawazo na mikakati kisha tuamue, la sivyo tunazidi kuangamia!
 
Ingekuwa nchi nyingine,kingeshanuka,ila kwa sababu ni Tza watu watakwambia ooh amani hii ni lulu,wakati hayo yote uliyosema ndio viashiria vya kutokuwa na amani.
 
Mkuu!

Hakika hali ni tata mbaya kbs na Mi ninachoona cha kufanya ni Nguvu ya Umma inyanyuke tu kuinusuru Taifa letu ambalo hakuna raslmali ambayo hakuna.

Hasa uongozi wa ngazi ya juu ktk serikali tawala wote wangetakiwa wapanguliwe,Hawana faida kwa Watanzania wanatikiswa na uchumi duni iliyosababishwa na watu wachache kwa ajili ya matumbo yao.
Hili linaniuma sana!
 
Yote haya ni kwa ajili ya kupima uvumilivu na uaminifu wenu. Maana hali hii itakuja kuwa rejea katika miaka ijayo.........kama tuliweza kuvumilia mwaka 2011/12 .........
 
Wana Jamii

Nionavyo mimi, hali ya NCHI ni TETE kuliko tulivyozoea. Baadhi ya viashiria ni hivi hapa:

1. Hazina ni kweupe. Mhe. Waziri Mkuchika alibainisha hili, japo Serikali imekuwa ikipinga muda mrefu. Ona sasa Mhe. Rais analazimika kupunguza baadhi ya maafisa wake kwenye safari za nje
2. Bunge kwa namna moja au nyingine halina imani na Rais. Mhe. Spika alisema Rais amebariki posho za Waheshimiwa Wabunge, Ikulu ikakana. Kumbuka sakata la Jairo na Luhanjo
3. Viongozi wetu wameanza kupeana sumu....hadi wanaogopa kupeana mikono. Sakata la Mhe. Mwakyembe
4. Ndani ya vyama hakupikiki. Magamba ya CCM, Mhe. Kafulila, Mhe. Hamad.....
5. Uchumi umekufa:
-Mfumko wa bei ni takribani 20% leo....ukitoka 4% mwaka 2005.
-Serikali imeshindwa kutoa fedha za maendeleo kwenye halmashauri zote nchini, Waziri wa TAMISEMI amekiri hayo Bungeni jana.
-Serikali imeshindwa kununua vifaa vya tiba na kutoa viposho vidogo vidogo kwa madaktari
6. Hali ya Maisha miongoni mwa Watanzania tulio wengi ni mbaya sana X sana!
7. Serikali kupitia Waziri Mkuu imekubali kuwa imeshindwa kuwaletea wananchi maisha bora. Tazama gazeti la Tanzania Daima la leo tar 3 Feb 2012.
8. Viongozi wa Serikali wakiwemo Wabunge wanajitazama wao tu...., wanaacha raia tunakufa..........
9.....ongeza list

Hivi katika hali kama hii, watanzania twaweza kufanya nini? Ebu tupeane mawazo na mikakati kisha tuamue, la sivyo tunazidi kuangamia!

Hatuna cha kufanya, kwasababu tulishaamua kwamba kikwete hatufai na hatukumchagua lakini Tume ya Taifa ya uchaguzi ikatangaza kwamba ameshinda na ikatokea jimbo la Nyang'wale na Geita matokeo yanafanana kila kitu. Nadhani tumuachie Mungu au tumuweke mungu pembeni tuwatoe kwa nguvu wanao roga nchi yetu
 
Back
Top Bottom