Huyu naibu katibu mkuu wa chama chetu lazima tumtazame vinginevyo atakimaliza chama.
Uchaguzi wa kata nne za udiwani Arusha, alipoenda kule upepo ukabadilika na tukapigwa 4-0.
Uchaguzi wa jana maeneo yote alikopita Nchemba wiki jana,ccm imeangukia pua
Karatu alivikwa hadi uchief lakini jana matokeo mmhhh....
Bukoba mjini penye mitaa zaidi ya 60,ukawa wamebeba zaidi ya 40.
Biharamulo, Ngara,Ukerewe na kote alikopita tena wiki jana hali ya matokeo sio nzuri hata kidogo.
Lakini jamani jamaa zangu wa humu ambao huwa tunahakikisha ccm inatetewa ilimradi kila jioni tuchukue buku saba; wako wapi tangu jana mchana?
Ritz1,Lizaboni,Faizafox,Chabruma,Simiyu yetu,Mwana Diwani,T2015CCM,n.k njooni bwana chama jf kinaangamia
Nyie si mnaangalia umati wa watu wanaokuja kuchukua tshirt na kofia? Wenzenu wajanja. Kula watakula kwako lakini kura ni siri yao.