Sinkala
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 1,773
- 684
Wale ambao card zao za NBC zilishachoka wana advantage zaidi, kwani NBC Visa + MasterCard sasa zinatolewa bure bila malipo. Changamkieni muwe na uwezo wa kuchukua pesa kwenye ATM za mabenki tofauti (ila kwa gharama zaidi kila muamala) ila walau itawasaidia wale wanaokuwa na shida ya fedha huku ATM za benki yao ikiwa haifanyi kazi. Lakini ndo hivyo, kama watu mlizoea kutofautisha ATM Card zenu kwa kuangalia picha, kwa sasa mtalazimika mkariri namba za card, kwani hakuna picha, vinginevyo unaweza ukajikuta umebeba kadi ya mkeo au mumeo, unafika kwenye ATM unashangaa umekosea password ! Sana sana signature ndio itasaidia kutofautisha, ila nayo ipo upande wa nyuma! Na wale mnaosafiri nje ya nchi sasa mna nafasi zaidi ya uhakika wa kuchukua fedha mkiwa huko. KAZI KWENU !!