NBC bank ni kero, hivi wenzangu mnawaelewa elewa?

Kireka1980

JF-Expert Member
Mar 18, 2008
302
43
Hawa NBC ni kweli wana matawi nchi nzima na mashine zao zinaccept visa card japo atm card zao sio visa!
Nilienda kwenye branch yao ya mlimani city siku ya jumapili (inakuwa wazi) nilitaka kudraw 1.5m nilichukua tahadhari zote kama vile kwenda na balance niliyoipata baada ya kukaa kwenye folen ya ATM. kufika dirishani baada ya foleni ndefu sana yule teller (mmama) akaniambia 'samahani branch uliyofungulia account ni ubungo na leo hawafungui so hatuwezi kukuhudumia' nikamuuliza kwa nn? akajibu kudraw nje ya branch yako lazima watutumie fax kwanza, SIJUI HATA FAX YA NINI MUNGU WANGU WAKATI SIKUMTUMA MTU, BALANCE YA THAT TIME NINAYO CAD NINAYO NILIKUWA FULL!
Nikaondoka nikarudi nyumbani mpoole, na jamaa niliyekuwa nimeenda kumchukulia hiyo cash akaniona mwongo. NISIANDIKE SAANA
 
Kuna tatizo kubwa sana la 'customer care' hapa nchini. Majibu ya watoa huduma katika mabenki ya kibiashara yanakatisha tamaa kama sio kukera. Labda hii inatokana na mis appropriateness ya watu katika fani zao. Nimeona katuni moja ya Kipanya, jamaa yuko kaunta anajitambulisha kuwa ana digrii ya kilimo toka SUA (plz no offense kwa SUASO) ni teller katika commercial bank. Nikajisemea hapa kaazi kweli kweli.

Kingine hawa jamaa nasikia sijui operations zao (server) ziko SA, na kuna aina ya controls ambazo bila SA hawawezi kufanya kitu. Labda iwe changamoto kwa watawala wetu kuwabana wawekezaji ili kuboresha huduma za kijamii. Pole Kireka, I understand your frustrations
 
NBC one of the worst Banks in the country.Kuanzia tarehe 26 June nimetumiwa fedha kwa mtindo wa money transfer na imewachukua zaidi ya siku sita,(YES! SITA), kukamilisha transaction hiyo.Matawi yote yapo hapa hapa Dar es salaam.
AND THEY CLAIM TO BE IN BUSINESS!!!!
 
Pole sana mkuu kwa yaliyokukuta!mimi ilishanitokeaga ila ilikua tofauti kidogo na wewe!nilikua natakla hela nying kidogo sasa nikaunga que kwenye ATM nikachukua balance nikaunga que kwenye line ya ku draw!kufika kwa teller anasema siwez kukulipa hela zote hizi so inatakiwa uende kwa bulk tellers!nikawa mpole nikaenda kufika kwa bulk teller anasema hii balance umeichukua wapi?inatakiwa uwe na mfanyakaz wa benk ndio akuchukulie balance na aweke sign yake!du nikachoka kwa vile nilikua na shida nikasema sawa! anaechukua hiyo balance yaan huyo mtu wao wa benk alikua ameenda lunch so ikabd nisubiri ilikua ni majira ya saa saba kasoro mchana!nilikaa hadi majira ya 1.30pm ndio akaja bwana mkubwa tukaenda kuchukua balance.

Sasa mimi nikamuuliza why inakua hivi?akasema kuna wasanii walikua wanatengeneza zile ATM statements na walishapigwa si chini ya milion 100 hivi!sasa nikamuuliza why cashier kabla ya kulipa asiangalie account ili kujua kama kuna hizo hela na pia kwenye account ya mteja kuna picha yake so anaweza kuangalia kama je mteja ni mwenyewe ama la!

Akasema jamaa wame disable teller hawez ku view balance wala nini!bas nikachomoa hela zangu zote sasa hv nina safe hm nadumbukiz ataratibu taratibu!

Polen wazee mabenk ya bongo hayana tija!
 
why cashier kabla ya kulipa asiangalie account ili kujua kama kuna hizo hela na pia kwenye account ya mteja kuna picha yake so anaweza kuangalia kama je mteja ni mwenyewe ama la!

Akasema jamaa wame disable teller hawez ku view balance wala nini!bas nikachomoa hela zangu zote sasa hv nina safe hm nadumbukiz ataratibu taratibu!

Polen wazee mabenk ya bongo hayana tija!

ukweli ni kwamba katika server zao hakuna data zaidi ya transactions (D/C) tu. Hakuna picha wala signature ya customer wanadai wanaogopa bandwidth costs.

wote haya yametukuta na upande wangu siitumii tena hiyo benki kwani nu usmbufu mwanzo mwisho
 
ukweli ni kwamba katika server zao hakuna data zaidi ya transactions (D/C) tu. Hakuna picha wala signature ya customer wanadai wanaogopa bandwidth costs.

wote haya yametukuta na upande wangu siitumii tena hiyo benki kwani nu usmbufu mwanzo mwisho

Mimi nahisi hii inaweza ikawa ni danganya toto tu. Hii (NBC) ni mojawapo ya benki ambazo magazeti hasa Mwanahalisi yaliripoti akaunti za mafisadi ikiwemo mzee wa vijisenti, Meremeta n.k. Huenda umefanyika mpango maalum wa kuhakikisha kuwa wafanyakazi wa benki hawapati access kwenye hizi akaunti ili wasitoe taarifa kwa waandisji wa habari na mafisadi waendelee kujificha vizuri huko.
 
Nimetoka saizi NBC tawi la Kichwele hapo kuchukua pesa wanasema hawana pesa duh! nimechukia mpaka basi yaani mida hii hii hawa NBC sijui ndo wanafilisika ngoja nihamishe pesa zangu zote isije ikawa ya DECI.
 
bas nikachomoa hela zangu zote sasa hv nina safe hm nadumbukiz ataratibu taratibu!
Dah! asanteni sana kwa kuniamsha toka usingizini,maana ni juzi tu nimetoka kuchukua fomu zao.ma-bank mengi ni ya kibabaishaji tu na kila kukicha yanaongezeka.Inatupasa kuwa makini sana nazo.

Mkuu unadhani ufumbuzi watatizo hilo ni kuziweka nyumbani? angalia TRA (majambazi)wasije kuzichukua.
 
Mie mwenyewe nina akaunti katika benki hii, kimsingi huduma zao ni mbovu sana. Kuna wakati nilikwenda kuhudumiwa pale katika tawi chuo kikuu, wahudumu niliokutana nao ilikuwa kero tupu, wana majibu ya mkato sana wakati bila sisi hawawezi kujiita benki. Likewise, ATM zao za Mwenge na Sinza Kijiweni muda mwingi haziko kazini (kama sio muda wote).Mbaya zaidi, kadi yao si VISA, hivyo huwezi kuchukua pesa katika ATM za benki nyingine iwapo una kadi ya NBC.

Kama wana masikio na wasikie na warekebishe kasoro hizi, kinachofuata ni kufunga akaunti!
 
Nbc kweli huduma zenu mbaya sana sana....wana urasimu usio na faida wala msingi.....jamani hebu acheni utongo tongo wa akili zenu na akili mgando...badilikenii sasa banki iwe ya ushindani sio ya mazoea.....
 
Bank sio mbaya ila tatizo ni watendaji wao. bank kama bank ina mipango mizuri kwa wateja wake ila anaweza kutokea mtumishi mmoja akaudhi wateja.

Mfano CRDB tawi la Vijana Dar wana kauli mbaya karibia wote utadhani uongozi wa bank ulijua ukawapanga wote tawi moja. Hivyo tuwe tunaangalia kama ni tatizo la mtu mmoja ni system nzima ya bank
 
ukidraw hela kwenye ATM ukaomba bal. utakuta kuna utofauti na hela unayoijua wewe,but ukidraw next time unakuta iko ok.SIJUI HUWA WATEGA!!!!!!!!!!
 
wadau hii benk imechoka vya kutosha hawana kitu kinachoitwa CUSTOMER CARE kabisa wote wamenuna tu bila sababu.

USHAURI WA BURE
Kama mdau na mteja japo akaunti yangu nipo njiani kuifunga ningeshauri management wafanye OVERHAUL ya ukweli hasa kwa staff wanaofanya kazi kwa mazoea (business as usual) waajiriwe vijana wenye kiu na kufanya kazi na walio na sifa sio hao staff wa enzi hizo ambao hawajui maana ya biashara walizoea kufanya kazi enzi za benki moja wkt sasa zipo benk lukuki.

KUMBUKENI NBC
THE CUSTOMER YOU SERVE IS THE CUSTOMER YOU HAVE
asanteni
 
Labda hii inatokana na mis appropriateness ya watu katika fani zao. Nimeona katuni moja ya Kipanya, jamaa yuko kaunta anajitambulisha kuwa ana digrii ya kilimo toka SUA (plz no offense kwa SUASO) ni teller katika commercial bank. Nikajisemea hapa kaazi kweli kweli.


Nafikiri mkuu hauna point hapo na haujaelewa mjadala halisi? je elimu ya chuo fulani na ubaya wa huduma za benki kuna uhusiano gani? tatizo la kwamba lazima kutumwe fax na SUA ZINA MAHUSIANO.

Tatizo liko hapa kwamba hudima kwa ujumla za NBC zinaboa sana sana haswa hilo la kutumwa fax wakati mtandao wao umeunganishwa tanzania nzima. Benki hii hii karibu kila mwisho wa mwezi mtandao wao una fail na wanasema server iko S AFIRCA. jE TUTAFIKA?
 
Pole mzee. Unachosema inawezekana ni kweli suala la kuvuja taarifa za account za mafisadi limezua mambo mengi mojawapo ni hilo ambalo limesababisha staff wa benk wachache tuu kuwa na access ya balace ya mteja. Hizo ndizo gharama za ufisadi ndani ya nchi, zipo nyingi pia, mfano mojawapo ni kama mlivyoona serikali inataka kutunga sheria kuhusu umiliki wa vyombo vya habari. Hao watu wana pesa nyingi na ndio wateja wakubwa wa bengi hizo unategemea benk zitamsikiliza nani kati ya wewe na hao. wao hawasumbuki hivyo, wakiingia benki wanamwona menager tu na kuhudumiwa. Ni vizuri mabenki pia yakajitahidi kuwafundisha staff wao huduma nzuri kwa wateja (customer care), kama wateja wameanza funga account zao hiyo ni balaa.
 
Leo nimepoteza karibu siku nzima tawi lao la mlimani city, ...hii nbc ni shida
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom