Nawachukia Sana mashabiki na wapenzi wa soka Tanzania............!!!

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Hivi tatizo lenu nini? ulimbukeni au ndio bendera kufata upepo?? Nimesikia leo asubuhi RFA eti mashabiki wa soka Dar waliamua kuandamana kushinikiza kocha wa timu ya Taifa ajiuzuru atafutwe kocha mwingine. Mi nadhani hawa watu hawana kazi za kufanya na huenda hata uwezo wao wa kufikiri nina mashaka nao...Eh!! Hivi kweli kwa mtu mwenye akili timamu kushindwa kwa timu ya taifa ya Tanzania linaweza kukufanya mtu mzima uache shughuli zako ukaandamana?

Mi nadhani hayo maandamano yalitakiwa yawe ya kushinikiza uongozi wote wa TFF na Wizara ya Michezo uondoke madarakani mara moja. tatizo la kushindwa Tanzania katika medani ya soka jamani si kocha....jamani eh! Kwani tukijikwaa na kuanguka tunakimbilia kulaumu tulipoangukia badala ya kulaumu tulipojikwaa ambapo kumelekea sisi kuanguka?

Hakuna kitu kinachonikera kama kuona TFF na huyo Raisi wake na wengine wanavyokosa ubunifu na hasa katika kipindi hiki cha utandawazi....Leo eti wana weka mashindano ya Copa Coca Cola mashindano yakiisha wanatajwa wachezaji wazuri waliochaguliwa sijui kunatokea jinamizi gani mwisho wa siku kila kitu ...kimyaaaaa!! Hivi Tanzania tunategemea kupata mafanikio bila ya kuwa na mipango endelevu kuanzia ngazi ya chini jamani? Hivi kweli hata leo akiletwa kocha kama Alex Ferguson, Pep Guadiola, Morinho ndio mafanikio yatapatikana? Mi nasema "NO"...Watanzania tunapenda mambo mazuri bila kuvuja jasho...hapa namaanisha mipango, gharama na kujitoa kikweli....Kwani akija Mbwna Samata au huyo Thomas Ulimwengu ndio nini?

Juzi Clouds fm kwenye kipindi cha sports extra alihojiwa Zamoyni Mogella.alisema kitu kimoja kuwa wachezaji wa Tanzania kwa kizazi cha leo hawajitambuai, hawajui wajibu wao uwanjani, hawajitumi, wavivu na hawana malengo....Sasa hapo linaongezeka na hilo la TFF na Wizara ya michezo mbovu isiyo na mipango. Mtaandamana Sana na kubadirisha makocha lakini vichapo ni pale pale!!! wameniboa sana...:ballchain::smash:
 
hilo nalo neno yaani hawa tff ndio hamna kitu kabisaa hiyo wizaro ipo kwa ajili ya posho tu mkuu sajenti
 
hilo nalo neno yaani hawa tff ndio hamna kitu kabisaa hiyo wizaro ipo kwa ajili ya posho tu mkuu sajenti
..naona jamaa wamegeuza ka-mradi kao ka kujipatia posho za kuendelea kuishi mjini...bure kabisa!!
 
TFF ni kimaslahi mnooooo, hamna chama cha michezo ambacho kipo kwenye mrija wa pesa kuliko hao jamaa.

Wanachojua wao ni kupeleka timu uwanjani wakusanye mapato tu!

Nashangaa timu ya wasichana Twiga inafanya vizuri lakini hata hawaisaidii inakuwa omba omba!!!
 
Tuna mipango ya zima moto.Wale watoto waliokwenda Brazil wakachukua kombe la dunia kwa watoto wako wapi? Mipango mibovu.Kuna kiongozi mmoja pale TFF anapokuita kwenye timu ya taifa anataka 10% usipompatia huitwi wala hupangwi.TEGETE,KIGI,NGASA ndo waliipeleka Stars CHAN leo wapo nje.Sasa nguvu zote kwa Mademu,wanajituma kuliko Waume.Nchi yenye Wanaume takriba milioni 20 hatuna timu ya taifa?TFF Wajiuzulu hawawezi kazi.
 
Hivi tatizo lenu nini? ulimbukeni au ndio bendera kufata upepo?? Nimesikia leo asubuhi RFA eti mashabiki wa soka Dar waliamua kuandamana kushinikiza kocha wa timu ya Taifa ajiuzuru atafutwe kocha mwingine. Mi nadhani hawa watu hawana kazi za kufanya na huenda hata uwezo wao wa kufikiri nina mashaka nao...Eh!! Hivi kweli kwa mtu mwenye akili timamu kushindwa kwa timu ya taifa ya Tanzania linaweza kukufanya mtu mzima uache shughuli zako ukaandamana?

Mi nadhani hayo maandamano yalitakiwa yawe ya kushinikiza uongozi wote wa TFF na Wizara ya Michezo uondoke madarakani mara moja. tatizo la kushindwa Tanzania katika medani ya soka jamani si kocha....jamani eh! Kwani tukijikwaa na kuanguka tunakimbilia kulaumu tulipoangukia badala ya kulaumu tulipojikwaa ambapo kumelekea sisi kuanguka?

Hakuna kitu kinachonikera kama kuona TFF na huyo Raisi wake na wengine wanavyokosa ubunifu na hasa katika kipindi hiki cha utandawazi....Leo eti wana weka mashindano ya Copa Coca Cola mashindano yakiisha wanatajwa wachezaji wazuri waliochaguliwa sijui kunatokea jinamizi gani mwisho wa siku kila kitu ...kimyaaaaa!! Hivi Tanzania tunategemea kupata mafanikio bila ya kuwa na mipango endelevu kuanzia ngazi ya chini jamani? Hivi kweli hata leo akiletwa kocha kama Alex Ferguson, Pep Guadiola, Morinho ndio mafanikio yatapatikana? Mi nasema "NO"...Watanzania tunapenda mambo mazuri bila kuvuja jasho...hapa namaanisha mipango, gharama na kujitoa kikweli....Kwani akija Mbwna Samata au huyo Thomas Ulimwengu ndio nini?

Juzi Clouds fm kwenye kipindi cha sports extra alihojiwa Zamoyni Mogella.alisema kitu kimoja kuwa wachezaji wa Tanzania kwa kizazi cha leo hawajitambuai, hawajui wajibu wao uwanjani, hawajitumi, wavivu na hawana malengo....Sasa hapo linaongezeka na hilo la TFF na Wizara ya michezo mbovu isiyo na mipango. Mtaandamana Sana na kubadirisha makocha lakini vichapo ni pale pale!!! wameniboa sana...:ballchain::smash:

Ndiyo maana mimi nimeamua kuwa mshabiki wa MANCHESTER
 
Back
Top Bottom