Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Hivi tatizo lenu nini? ulimbukeni au ndio bendera kufata upepo?? Nimesikia leo asubuhi RFA eti mashabiki wa soka Dar waliamua kuandamana kushinikiza kocha wa timu ya Taifa ajiuzuru atafutwe kocha mwingine. Mi nadhani hawa watu hawana kazi za kufanya na huenda hata uwezo wao wa kufikiri nina mashaka nao...Eh!! Hivi kweli kwa mtu mwenye akili timamu kushindwa kwa timu ya taifa ya Tanzania linaweza kukufanya mtu mzima uache shughuli zako ukaandamana?
Mi nadhani hayo maandamano yalitakiwa yawe ya kushinikiza uongozi wote wa TFF na Wizara ya Michezo uondoke madarakani mara moja. tatizo la kushindwa Tanzania katika medani ya soka jamani si kocha....jamani eh! Kwani tukijikwaa na kuanguka tunakimbilia kulaumu tulipoangukia badala ya kulaumu tulipojikwaa ambapo kumelekea sisi kuanguka?
Hakuna kitu kinachonikera kama kuona TFF na huyo Raisi wake na wengine wanavyokosa ubunifu na hasa katika kipindi hiki cha utandawazi....Leo eti wana weka mashindano ya Copa Coca Cola mashindano yakiisha wanatajwa wachezaji wazuri waliochaguliwa sijui kunatokea jinamizi gani mwisho wa siku kila kitu ...kimyaaaaa!! Hivi Tanzania tunategemea kupata mafanikio bila ya kuwa na mipango endelevu kuanzia ngazi ya chini jamani? Hivi kweli hata leo akiletwa kocha kama Alex Ferguson, Pep Guadiola, Morinho ndio mafanikio yatapatikana? Mi nasema "NO"...Watanzania tunapenda mambo mazuri bila kuvuja jasho...hapa namaanisha mipango, gharama na kujitoa kikweli....Kwani akija Mbwna Samata au huyo Thomas Ulimwengu ndio nini?
Juzi Clouds fm kwenye kipindi cha sports extra alihojiwa Zamoyni Mogella.alisema kitu kimoja kuwa wachezaji wa Tanzania kwa kizazi cha leo hawajitambuai, hawajui wajibu wao uwanjani, hawajitumi, wavivu na hawana malengo....Sasa hapo linaongezeka na hilo la TFF na Wizara ya michezo mbovu isiyo na mipango. Mtaandamana Sana na kubadirisha makocha lakini vichapo ni pale pale!!! wameniboa sana...:ballchain::smash:
Mi nadhani hayo maandamano yalitakiwa yawe ya kushinikiza uongozi wote wa TFF na Wizara ya Michezo uondoke madarakani mara moja. tatizo la kushindwa Tanzania katika medani ya soka jamani si kocha....jamani eh! Kwani tukijikwaa na kuanguka tunakimbilia kulaumu tulipoangukia badala ya kulaumu tulipojikwaa ambapo kumelekea sisi kuanguka?
Hakuna kitu kinachonikera kama kuona TFF na huyo Raisi wake na wengine wanavyokosa ubunifu na hasa katika kipindi hiki cha utandawazi....Leo eti wana weka mashindano ya Copa Coca Cola mashindano yakiisha wanatajwa wachezaji wazuri waliochaguliwa sijui kunatokea jinamizi gani mwisho wa siku kila kitu ...kimyaaaaa!! Hivi Tanzania tunategemea kupata mafanikio bila ya kuwa na mipango endelevu kuanzia ngazi ya chini jamani? Hivi kweli hata leo akiletwa kocha kama Alex Ferguson, Pep Guadiola, Morinho ndio mafanikio yatapatikana? Mi nasema "NO"...Watanzania tunapenda mambo mazuri bila kuvuja jasho...hapa namaanisha mipango, gharama na kujitoa kikweli....Kwani akija Mbwna Samata au huyo Thomas Ulimwengu ndio nini?
Juzi Clouds fm kwenye kipindi cha sports extra alihojiwa Zamoyni Mogella.alisema kitu kimoja kuwa wachezaji wa Tanzania kwa kizazi cha leo hawajitambuai, hawajui wajibu wao uwanjani, hawajitumi, wavivu na hawana malengo....Sasa hapo linaongezeka na hilo la TFF na Wizara ya michezo mbovu isiyo na mipango. Mtaandamana Sana na kubadirisha makocha lakini vichapo ni pale pale!!! wameniboa sana...:ballchain::smash: