Naumia sana nikikumbuka usumbufu wa kaka ulivyomfanya mama awe analia na kupata stress, wengine mpo ambao mliona mama anakosa raha kisa mtoto?

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,081
Ilikuwa 2005 hai 2007 wakati kaka akiwa na miaka 16 hadi 18, alikuwa anamfanya mama alie sana na mimi nilikuwa najisikia vibaya sana kumuona mama analia machozi na kupiga ukunga wa maumivu, very painfull!

Kaka alihamishwa shule kibao kwa utoro, uhuni, n.k. Alijiunga na makundi mabovu ya wavuta bangi, wanywa pombe enzi hizo vizroba ndio vilikuwa vinatrend sana, tunashukuru hakuingia kwenye madawa tu maana tulikuwa mkoani.

Nyumbani anatoroka usiku kwenda disko. Kaka alianza kuuza vitu vya pale nyumbani kama glasi, deki, baiskeli, n.k. Mzee kashatoa dozi nzito hadi jirani alikuja kumstop, mzee alitoa kipigo kizito cha takribani nusu saa yani hakuna mapumziko, alikuwa anampiga kwa mkanda wa ngozi na kuna muda anamtandika kule mwisho wa mkanda kwenye kachuma, mzee aliwahi hadi kumtishia kuwaita mapolisi lakini bro alikuwa kapinda si mchezo.

Asubuhi ikifika tunaenda kumcheki chumbani kwake hayupo basi mama analia sana na mimi naumia, mchana unakuta tu mama katulia machozi yanamlenga.

Mama alishampeleka kwa wachungaji na hata akapelekwa kusomewa visomo lakini wapi, walidhani ni pepo ila kiukweli ilikuwa ni stage ya ukuaji.

kaka alikuwa msumbufu sana ila kama utani vile licha ya kurudia form 4 mara 2 baada ya hapo hakuwa msumbufu aliweza kusoma hadi masters huko nje na leo hii hapa navyoongea ana cheo chake kizuri tu na biashara zake zinaendelea vizuri, ana tabia nzuri kabisa mfano wa kuigwa.

Kila nikikumbuka stress alizompa mama huwa nasikitika sana nikikumbuka mama alivyokuwa analia.

Je, kuna mwengine hii hali iliwahi kutokea kwao?
 
Aina hii ya watoto wapo,yani anakuwa pasua kichwa,wapo mpaka wazazi waliopata maradhi ya pressure na kisukari kwa ajili ya kuumizwa na matendo ya aina hii ya watoto,huwa ni hatari sana,wanaweza hata kusababisha ndoa ikavunjika,kwani mara nyingi wanao watetea ni wamama,maana hakuna baba anaeweza kuvumilia ujinga,sasa inapofikia kwenye kumuadhibu unakuta wamama wanaingilia kati,pale ndipo tatizo linapozidi kuwa kubwa...
 
Aina hii ya watoto wapo,yani anakuwa pasua kichwa,wapo mpaka wazazi waliopata maradhi ya pressure na kisukari kwa ajili ya kuumizwa na matendo ya aina hii ya watoto,huwa ni hatari sana,wanaweza hata kusababisha ndoa ikavunjika,kwani mara nyingi wanao watetea ni wamama,maana hakuna baba anaeweza kuvumilia ujinga,sasa inapofikia kwenye kumuadhibu unakuta wamama wanaingilia kati,pale ndipo tatizo linapozidi kuwa kubwa...
Yani acha tu, ila uzuri wazazi wetu wa zamani walikuwa wanatoa dozi wote ukizingua, nae mama alikuwa anamsaidia mzee kutoa dozi.
 
Teenager alikuwa. Au FOOLISH AGE tuseme. Wote tumepitia huko.

Ila kuna wengine walishindwa kutoka ndo yakawa maisha yao mpk leo. Wanangu wengi wa KINONDONI tuliokuwa ktk mkumbo wa aina hiyo.

Niw wanatumia DOZI pale MWANANYAMALA ya kupunguza Athari za madawa kulevya wengine wamekufa eidha wakiwa njiani kuelekea south na ulaya wengine hawajulikani mpk leo wako wapi mana edhi hizo ndo ulikuwa mkumbo wa kuzamia meri wengine walifanikiwa kufika south na wengine wapo ulaya now tulikuwa na maisha ya kufikilika wengi tuliwaza kuishi ULAYA na AMERICA tulipenda statehe uhuni mwingi ubabe

Hakika hilo jambo likikukuta mwanao au mwanafamilia mnatakiwa mumshirikishe MUNGU mumuombee msimtenge na kumlaani mtoto.

Lkn katika kujenga MSINGI nafikili ndio ulinisaidia hata mimi ni KUSOMA MADRASA(elimu ya dini) nikiwa mdogo japo nilikuwa naenda kwa FORCE (viboko) lkn ndio kipindi waliniweza nilivyofika umri huo kwanzaa nilikuwa na ubavu hata mtaani niliogopeka ukijumlisha BANGI na MIHADARATI mingine kasoro pombe tu ndo sikuiweza na Sikuwahi kuinywa na KUNDI nililokuwa nalo na namna FAMIRIA yangu ilivyokuwa watu wa dini waliamini majirani
Nimelogwa.

Lkn si baba wala mama aliyenitolea neno baya mfn wa kunilaani au vyvyte vile kimaneno. Siku zote waliniombea na hali hii ndo ikawa inaniumiza sana mpk mwenyewe tu nikajitenga na MAKUNDI mahovu nikawa mwema

Wasomesheni DINI watoto zenu wangali wakiwa wadogo mnawaweza kuna umri ukifika hamtawaweza na ELIMU ya DINI ndio itakayowaokoa.
 
Mungu ni mwema akitulia na kujitambua mbaya akizeeka na utundu/ukorofi wake aisee mama anaweza kufa
 
Teenager alikuwa
Au FOOLISH AGE tuseme
Wote tumepitia huko
Ila kuna wengine walishindwa kutoka ndo yakawa maisha yao mpk leo
Wanangu wengi wa KINONDONI tuliokuwa ktk mkumbo wa aina hiyo
Niw wanatumia DOZI pale MWANANYAMALA ya kupunguza Athari za madawa kulevya wengine wamekufa eidha wakiwa njiani kuelekea south na ulaya wengine hawajulikani mpk leo wako wapi mana edhi hizo ndo ulikuwa mkumbo wa kuzamia meri wengine walifanikiwa kufika south na wengine wapo ulaya now tulikuwa na maisha ya kufikilika wengi tuliwaza kuishi ULAYA na AMERICA tulipenda statehe uhuni mwingi ubabe

Hakika hilo jambo likikukuta mwanao au mwanafamilia mnatakiwa mumshirikishe MUNGU mumuombee msimtenge na kumlaani mtoto
Lkn katika kujenga MSINGI nafikili ndio ulinisaidia hata mimi ni KUSOMA MADRASA(elimu ya dini) nikiwa mdogo japo nilikuwa naenda kwa FORCE ( viboko) lkn ndio kipindi waliniweza nilivyofika umri huo kwanzaa nilikuwa na ubavu hata mtaani niliogopeka ukijumlisha BANGI na MIHADARATI mingine kasoro pombe tu ndo sikuiweza na Sikuwahi kuinywa na KUNDI nililokuwa nalo na namna FAMIRIA yangu ilivyokuwa watu wa dini waliamini majirani
Nimelogwa
Lkn si baba wala mama aliyenitolea neno baya mfn wa kunilaani au vyvyte vile kimaneno
Siku zote waliniombea na hali hii ndo ikawa inaniumiza sana mpk mwenyewe tu nikajitenga na MAKUNDI mahovu nikawa mwema

Wasomesheni DINI watoto zenu wangali wakiwa wadogo mnawaweza kuna umri ukifika hamtawaweza na ELIMU ya DINI ndio itakayowaokoa
Mtoto anapofika hii foolish age ni kwamba anaona ni ujanja kuvuta bangi, kunywa pombe, kuwa katika kundi, n.k. hivi vitu kwao vinasukumwa sana na kutoa ushamba kwa kujaribu, kuiga maisha ya mitandaoni, n.k.

Kiukweli huwa ni kumwachia tu Mwenyezi Mungu hapa maana akili inakuwa imevurugika si mchezo, wapo wengi tu walipata mafundisho utotoni lakini zile homoni za kubalehe zikianza kuchakata kwa wengine huwa ni tatizo, cha kuombea tu ni kwamba wajirudi kama walivyokuwa.
 
Mimi mwenyewe nilikua hivo ila sikua mwizi tu, nilikua mhuni sana yaan mama alishaongea mpka basi sisikii .

Hii ilichangia na mtaa niliokulia wahuni ni wengi ma kampani ya vijana wenzangu pia
 
Ilikuwa 2005 hai 2007 wakati kaka akiwa na miaka 16 hadi 18, alikuwa anamfanya mama alie sana na mimi nilikuwa najisikia vibaya sana kumuona mama analia machozi na kupiga ukunga wa maumivu, very painfull!

Kaka alihamishwa shule kibao kwa utoro, uhuni, n.k. Alijiunga na makundi mabovu ya wavuta bangi, wanywa pombe enzi hizo vizroba ndio vilikuwa vinatrend sana, tunashukuru hakuingia kwenye madawa tu maana tulikuwa mkoani.

Nyumbani anatoroka usiku kwenda disko. Kaka alianza kuuza vitu vya pale nyumbani kama glasi, deki, baiskeli, n.k. Mzee kashatoa dozi nzito hadi jirani alikuja kumstop, mzee alitoa kipigo kizito cha takribani nusu saa yani hakuna mapumziko, alikuwa anampiga kwa mkanda wa ngozi na kuna muda anamtandika kule mwisho wa mkanda kwenye kachuma, mzee aliwahi hadi kumtishia kuwaita mapolisi lakini bro alikuwa kapinda si mchezo.

Asubuhi ikifika tunaenda kumcheki chumbani kwake hayupo basi mama analia sana na mimi naumia, mchana unakuta tu mama katulia machozi yanamlenga.

Mama alishampeleka kwa wachungaji na hata akapelekwa kusomewa visomo lakini wapi, walidhani ni pepo ila kiukweli ilikuwa ni stage ya ukuaji.

kaka alikuwa msumbufu sana ila kama utani vile licha ya kurudia form 4 mara 2 baada ya hapo hakuwa msumbufu aliweza kusoma hadi masters huko nje na leo hii hapa navyoongea ana cheo chake kizuri tu na biashara zake zinaendelea vizuri, ana tabia nzuri kabisa mfano wa kuigwa.

Kila nikikumbuka stress alizompa mama huwa nasikitika sana nikikumbuka mama alivyokuwa analia.

Je, kuna mwengine hii hali iliwahi kutokea kwao?
Vipi boss,mama amebahatika kumwona brother akiwa mpya wa tabia?
Km wazazi wako wapo hai Ni faraja na furaha kwao wanapoona vijana wao wakibadilika na kuwa watu wema
 
Mimi mwenyewe nilikua hivo ila sikua mwizi tu, nilikua mhuni sana yaan mama alishaongea mpka basi sisikii .

Hii ilichangia na mtaa niliokulia wahuni ni wengi ma kampani ya vijana wenzangu pia
Sasa umebadilika?
 
Back
Top Bottom