National Insurance Corporation(NIC) Limefungwa?

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159
Heshima Mbele,

Kwa taarifa nilizonazo ambazo nimepewa toka kwa mkulu mmoja wa shirika la Bima ni Kwamba Serikali imeagiza shirika hilo lifungwe wakati serikali ikiamua ni nini kifanyike kulinusuru shirika hilo.

Habariz a ndani kabisa zinasema kuna baadhi ya watu wanataka kulichukua shirika hilo kama wawekezaji kwa bei ya kutupwa(Majina ninayo nasubiri kwanza) .Watu hao ni baadhi ya viongozi wenye sauti kubwa katika serikali.

Habari hizi zinasema kufa kwa shirika hilo kumechangiwa sana na Mkurugenzi Mkuu Mama Ikongo na baadhi ya maafisa wa juu wa shirika hilo akiwamo Mkurugenzi wa Fedha na Utawala
 
Kuhusu madeni
hadi kufikia Desemba 2006, lilikuwa na rasilimali zenye thamani ya sh bilioni 59.3 ambazo zinajumuisha majengo yenye thamani ya sh bilioni 35.4, yaliyoenea nchi nzima na hisa katika mashirika mbalimbali sh bilioni 14.3 na mali nyingine na madai mbalimbali yanayofikia sh bilioni 9.6
.

Haya wakuu,Nani alilifiisha shirika hili hapa
 
NIC restructuring takes off
PIUS RUGONZIBWA
Daily News; Thursday,February 05, 2009 @07:31

About 490 workers of the National Insurance Corporation (NIC) Limited have been laid off to pave a way for the firm’s restructuring process. The lay off comes after the approval of the cabinet for NIC’s restructuring following recommendations by Members of Parliament, international financial institutions and other stakeholders.

The Tanzania Union of Industrial and Commercial Workers Organization (TUICO) branch Chairman, Mr Michael Mwakyusa, confirmed in Dar es Salaam yesterday that workers were ready for the lay off provided they were paid their terminal benefits according to an earlier agreement.

Mr Mwakyusa said they were aware that about 5.1bn/- had been set aside for the exercise and from yesterday evening they started collecting their cheques. “We are also aware that the Consolidated Holdings Corporation has been preparing the cheques since last (Tuesday) night …but since we were involved in the process from the beginning, we are not worried that things will not go according to the plan,” said Mr Mwakyusa.

Yesterday, NIC issued a public notice announcing the termination exercise but in what could be seen as a controversy, the company said the offices would be closed for two days today and tomorrow and reopen next Monday. According to Mr Mwakyusa, they were earlier told by the management that they would be allowed to re-apply for jobs, but the vacancies have not been advertized.

The notice issued by NIC Board Chairman Dr Hamisi Kibola indicated that procedures for fresh recruitment of staff in line with the needs of the corporation had been put in place. “During the implementation of this task, NIC offices will not offer any services for two days - Thursday and Friday, the services shall resume on Monday, February 9, 2009, during this period, the respective services shall continue to be provided by all NIC agents and brokers throughout the country,” reads the notice in part.

Although Mr Mwakyusa said he had no much details on how the restructuring process would be carried out, Dr Kibola said in the notice that the termination was in line with an agreement that was reached between NIC employees through their Union, Government and CHC and arrangement for new staff recruitment was underway.

Contacted for comment on the development, the NIC Managing Director, Mrs Magreth Ikongo said through her secretary that all enquiries on the matter should be directed to CHC. CHC Director General Ms Edwina Lupembe told the 'Daily News' by phone that she was not in the position to talk on the issue and advised this paper to contact her colleague in the office, Mr Shaban Ngalupia, who she said was handling the matter.

Mr Ngalupia was not available for comment as he was reported to have been attending another important meeting at the CHC offices situated on Samora Avenue. On March last year, an agreement was signed before the High Court - Labour Division between representatives of NIC Management, Workers Union and CHC on the package needed to pay the workers and it was agreed after verification that 5.2bn/- was needed for paying the workers.
 
Historia ya watawala wetu "points to nothing else" isipokuwa ufisadi hata katika hili.Kuna wingu zito la ujinga wa kutupwa lililotanda juu ya watawala hawa."They do not think of anything else" isipokuwa kujipatia fedha ya aibu hata katika kipindi hiki ambapo wanajua fika kwamba ujinga wao uko wazi kwa wananchi wote.
Mungu aisaidie Tanzania jamani, "it's too much to bear."Mmm.

Heshima Mbele,

Kwa taarifa nilizonazo ambazo nimepewa toka kwa mkulu mmoja wa shirika la Bima ni Kwamba Serikali imeagiza shirika hilo lifungwe wakati serikali ikiamua ni nini kifanyike kulinusuru shirika hilo.

Habariz a ndani kabisa zinasema kuna baadhi ya watu wanataka kulichukua shirika hilo kama wawekezaji kwa bei ya kutupwa(Majina ninayo nasubiri kwanza) .Watu hao ni baadhi ya viongozi wenye sauti kubwa katika serikali.

Habari hizi zinasema kufa kwa shirika hilo kumechangiwa sana na Mkurugenzi Mkuu Mama Ikongo na baadhi ya maafisa wa juu wa shirika hilo akiwamo Mkurugenzi wa Fedha na Utawala
 
Bima ya Taifa yawafuta kazi wafanyakazi wake wote

SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC), ambalo ni kongwe na kubwa kuliko taasisi zote zinazotoa huduma hiyo nchini, jana lilianza kutekeleza mchakato wa kuachisha kazi wafanyakazi wake wote na kuwaajiri upya ili liweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Shirika hilo, lililokuwa na haki peke za kuendesha shughuli za bima nchini tangu mwaka 1967 wakati serikali ilipotaifisha mashirika binafsi, lilianza kuyumba mwaka 2000, miaka miwili baada ya serikali kulegeza masharti ya biashara na likatimua zaidi ya wafanyakazi 700 ili kupunguza gharama za uendeshaji, lakini tatizo la ufanisi linaonekana kuendelea.

Katika taarifa yake, mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NIC, Hamisi Kibola anaeleza kuwa zoezi la kuachisha kazi wafanyakazi wote linafanyika kutokana na makubaliano yaliyofikiwa kati ya wafanyakazi, serikali na kampuni ya Consolidated Holding Corporation.

Dk. Kibola alieleza kuwa wafanyakazi wote wa shirika hilo lililoanzishwa mwaka 1963 wameachishwa kazi na walitarajiwa kulipwa mafao yao kuanzia jana.

"Aidha, taratibu za kuajiri upya wafanyakazi tayari zimefanyika kulingana na mahitaji ya shirika," alisema Dk. Kibola.

Dk. Kibola alisema katika taarifa yake jana kuwa kutokana na zoezi hilo, shirika litasitisha huduma zake kwa siku mbili mfululizo, kuanzia leo na kurejeshwa upya Jumatatu ijayo.

"Wakati wa zoezi hili huduma, huduma za NIC zitaendelea kutolewa na madalali na wakala wa bima wa NIC waliopo nchini kama kawaida," alisema Dk. Kibola akizungumzia huduma za shirika hilo ambazo ni pamoja na bima ya maisha na nyingine.


"Marekebisho hayo yanahusisha kuachishwa kazi kwa baadhi ya wafanyakazi kuanzia Februari 4 mwaka huu na kuwalipa mafao yao kulingana na mikataba yao. Utaratibu wa kuajiri wafanyakazi wapya tayari umeandaliwa kwa mujibu wa mahitaji ya shirika," alisema Dk. Kibola.


Hata hivyo, hadi jana jioni wafanyakazi wengi walikuwa hawajalipwa stahili zao na wengi walikuwa wamekusanyika mitaa ya katikati ya jiji wakisubiri hundi zao.


"Hakuna kitu," alisema mfanyakazi mmoja ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe alipozungumza na Mwananchi majira ya saa 11:00 jioni. "Nilikuwa likizo na nikasikia kuwa tutalipwa leo. Nimekuja hapa tangu asubuhi, lakini hakuna kitu tulicholipwa hadi sasa. Labda sasa tusubiri kesho."


Mwaka 2006, kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi ilipinga mpango wa serikali wa kuliuza shirika hilo liuzwe kwa Sh3 bilioni na kuwaita viongozi wa Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC) ili kuwahoji kuhusu mpango huo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom