Nikitazama nchi ilipofikia, nashindwa kuamini kama kuna mtu yeyote anayeweza kuipeleka Tz pale ninapoota iwe, hivyo natamani tu siku moja niwe raisi mwenyewe!!!!!!
Nikitazama nchi ilipofikia, nashindwa kuamini kama kuna mtu yeyote anayeweza kuipeleka Tz pale ninapoota iwe, hivyo natamani tu siku moja niwe raisi mwenyewe!!!!!!
Kazi kweli kweli. sijapata picha unaposema "nashindwa kuaminikama kuna mtu yeyote anayeweza kuipeleka Tz pale ninapoota iwe" Je wewe si mtu? umeshauriwa utangaze sera zako, na pia kachukue fomu.
Kuna wakati nilishawahi kuuliza kama "kuwa rais ni kazi ngumu au rahisi?" Kwa bahati mbaya alinijibu mtu mmoja tu. Nafikiri kuifikisha nchi huko unakofikiria siyo sawa na mbili kutoa moja. Ni complicated process. Itakulazimu utumie nguvu sana ambazo zinaweza kuwa risk kwako pia. Watanzania walio wengi ni maneno mengi zaidi kuliko utekelezaji. Usitarajie watafanya kama unavyoagiza, na ukitaka kudeal na individual person unaweza kujikuta unapoteza hicho kiti cha Urais. Si ajabu ukajikuta unafanya kazi ya kuwakandamiza watu wa hali ya chini huku ukiwainua watu wa karibu yako ili wakulinde, kama alivyofanya Mkapa au anavyofanya Kagame. Namna pekee ya kuibadilisha Tanzania ni kuwa na idadi kubwa ya wabunge wasiokubali rushwa wala wasiokubali kudanganywa kwa vitu vidogo vidogo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.