GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Habarini wana JF, leo nimeamka na wazo jipya kidogo. Nimeona dada zetu wakiolewa na hawa jamaa wenye asili ya kiasia lakini sijawahi kuona wanaume wakioa dada zao. Hivyo nashindwa kujua kama upo uwezekano huo. Je! kama hapa Bongo ni ngumu nikiamua kuwafuatilia huko kwao India inawezekana? Naomba mtu mwenye ufahamu na nchi hiyo mila na taratibu zake za kindoa anijuze kwani nimeamua kutoka moyoni kutafuta Fedha kwa ajili ya mpango huo. Pia naomba mwenye maelezo ya kina juu ya gharama za usafiri wa kwenda India maisha ya huko si vibaya akanifahamisha pia!