Kibirizi
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 604
- 146
Wana JF naomba mwenye kujua, kama endapo nitaagiza laptop nje ya nchi kuna ushuru wowote TRA, bandarini au Airport, hofu yangu kubwa isije kuwa hizi laptop zinazo uzwa nje zikawa na ushuru kama wa magari. Kwa sababu kwenye mtandao naona zinauzwa bei poa sana, naogopa nisije lia kilio cha kusaga na meno pindi itakapokuwa imewasili bandarini au uwanja wa ndege. Mwenye ufahamu tafadhari anijuze. Natanguliza shukurani za dhati.