Natafuta Mwanamke Mwenye Sifa Zifuatazo!

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Jan 3, 2018
1,816
5,151
Ukihitaji salamu subiri kwanza nijipatie jiko,tofauti na hapo utaambulia vumbi la Kongo!


Mimi TUKANA UONE ninakuja kwenu wanawake wote kutoka pande zote za nchi ya Tanzania ambao mnautumia mtandao huu pendwa wa JF!

Dhumuni au Kusudio la Uzi huu ni kwamba nahitaji mwanamke atakayekuwa mama wa watoto wangu,Hivyo nimeonelea nije kwenu wana JF kwasababu humu ndani kuna kila sampo za wanawake kutoka kila pembe ya nchi yetu pendwa ya Tanzania.

SIFA ZANGU

1.Mimi ni maji ya kunde
2.Mimi nina kimo cha wastani
3.Umri wangu ni miaka 32
4.Elimu yangu ni kidato cha 6,Kisha nikapata Diploma ya Logistics &Transport Management
5.Ninamiliki nyumba na gari kadhaa
6.Nina akaunti katika benki 2 (Crbd & Equity)
7.Ukiacha nyumba ninayoishi hapa Dar es salaam lakini pia namiliki nyumba mikoa ya Arusha & Mbeya.
8.Namiliki pia kiwanja Maili moja mkoa wa Pwani
9.Sina Mke na Sijawahi kuwa nae
10.Nina mtoto mmoja wa kike yuko na mama yake Mkoani Arusha.
11.Mimi ni Mkristo

SIFA ZA MWANAMKE NIMTAKAYE

1.Awe na kimo cha kawaida
2.Awe mwenye rangi halisi (Mweusi au Mweupe)
3.Awe na Nywele halisi
4.Awe mtu anayemuamini Mungu (Muisilamu itakuwa vema zaidi)
5.Awe na Elimu ya kawaida (Darasa la 7 au Form 4)
6.Awe na umbo linaloeleweka
7.Awe na uzito wa wastani
8.Awe Hajawahi kuolewa
9.Akiwa na mtoto asizidi mmoja (Huyo mtoto nitamtunza kama mwanangu kwa kila kitu anachopaswa kufanyiwa mtoto yakiwemo mahitaji muhimu)
10.Awe tayari kupima afya yake
11.Awe Kabila lolote
12.Awe Msafi na Anayejali familia
13.Awe na akili timamu
14.Awe Tayari kupigwa Mikunyubenga (×2 kwa siku)
15.Awe mzuri wa sura na shepu (Shepu iwe ya wastani kwasababu sipendi matako makubwa)
16.Umri wake uwe kuanzia mika 28 - 35

N.B - Endapo tukipima afya na akiwa ameathirika sitomuacha,jambo la msingi awe anatumia dawa zake vizuri na kwa wakati ili asije kuniambukiza mumewe,pia nitampenda na kumjali!.

SIFA NISIZOZIPENDA KWA MWANAMKE HUYO.

1.Asiwe Mnywaji wa kileo cha aina yeyote.
2.Asiwe Mchafu,Mchoyo na Mlafi
3.Asiwe Muongo na M-mbeya
4.Asiwe Mvaa Mawigi
5.Asiwe Muweka Mikucha mirefu
6.Asiwe mvaa Mahereni makubwa
7.Asiwe Mvaa Vikukuu na Mashanga
8.Asiwe msuka manywele marefu hadi Kero!
9.Asiwe Mzururaji
10.Asiwe mtu wa Marafiki wengi
11.Asiwe mtu anayejikoboa (Kujipaka Mikorogo)
12.Asiwe mwenye Makalio makubwa
13.Asiwe na Miguu myembamba kama fito
14.Asiwe na Maziwa makubwa (Maziwa yaendane na umbo lake)
15.Asiwe mvaa Hovyo mbele za watu!
16.Asiwe mtu wa Kujirusha au Mpenda Starehe
17.Asiwe ametumika sana kama gari bovu,wote najua mmetumika ila angalau awe ni namba D

Mwenye sifa hizo kama yuko tayari anicheki PM ili tuanze kufahamiana na kuzoeana na kama itawezekana mwakani tufunge ndoa takatifu!.

Nitamuhudumia kila kitu kwakuwa atakuwa mke wangu,pia nitampatia mtaji wa kufanya Biashara yeyote atakayoitaka na mahali popote.

Nitamnunulia usafiri atakao uhitaji yeye,kama akiona gari za kwangu hazipendi basi yeye atasema anahitaji gari gani nimnunulie ili liwe linamuwahisha kwenye biashara na shughuli zake.

Kama hajui kuendesha gari nitampeleka kwenye vyuo vinavyotoa mafunzo ya udereva ili akajifunze huko.

VITU AMBAVYO SITAVIFANYA KWA MWANAMKE WANGU HUYO.

1.Sitamuendeleza kielimu (Elimu aliyoipata wakati anasomeshwa na wazazi wake ndiyo itakuwa hiyo hiyo!)
2.Sitomnunulia nguo za ndani (Chupi),Hizi atakuwa ananunua kwa pesa zake mwenyewe!.
3.Sitojenga kwa wazazi wake (Kama wazazi wake hawakujenga nyumba au kujengewa na watoto wao basi sitofanya hivyo mimi)
4.Sitasomesha ndugu zake wakiwemo wadogo zake( Kama wadogo zake hawajasomeshwa na wazazi wake basi kwangu waandike maumivu)


Nawasilisha kwenu kina dada warembo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom