Nasimama na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, lililotokea shule ya Sekondari Kiwanja Chunya lilitokea pia Sekondari ya Chidya, Mtwara 2008

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Sep 22, 2016
4,580
7,938
Mwaka 2008 Aprili wakati wa kufungua shule baada ya likizo fupi ya pasaka Chidya Secondary iliyopo wilayani Masasi mkoani Mtwara ulitokea mgomo uliosababishwa na wanafunzi kupikiwa uji usio na sukari kwa siku 2 mfululizo.

Wanafunzi wakaamua kufanya uharibifu wa mali za shule ikiwemo na gari kubwa (Lory) ya shule na kwa kulichoma moto na staff ya walimu ilichomwa moto kisha wanafunzi wote ukimwondoa mmoja tu ambaye alikuwa kiongozi wa nidhamu walikimbilia porini. Kenneth kijana alikuwa mlokole na ni mtoto wa mkuu wa wilaya mstaafu alibaki shule na walipokuja FFU walimzoa na kuondoka naye.

Asubuhi wanafunzi walianza kurejea taratibu na kujiandaa kisha kuingia darasani kama kawaida na shule ilipoa kimya.
Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na bodi ya shule ikakaa kikao cha dharura na kuja na maadhimio kadhaa pamoja na;

1.Kuwafukuza shule wanafunzi wachache.

2.Kuwasimamisha shule wanafunzi kadhaa na kuwaambia warudi na 150,000/= pindi wataporudi shule na wazazi wao.

3.Kila mwanafunzi aje na 75,000/= atakaporudi likizo ya Juni/Julai.

4.Baadhi ya viongozi wa wanafunzi na wanafunzi ambao walionekana kuwa ni wahamasishaji wakubwa wa mgomo ule kuburuzwa mahakamani baada ya kufukuzwa shule.
5.Shule haitafungwa kwa dharura na hatimaye wanafunzi waendelee na masomo mpaka Juni itakapofungwa kwa mujibu wa ratiba ya wizara ya elimu. Msimamo huu ulisimamiwa kikamilifu na headmaster nguli aliyekywa mjeshi Mr. Mwatenga.

Mkuu wa mkoa Albert Chalamila na timu yake wamefanya uamuzi nzuri sana ingawa wapo watakaoumizwa na kuathirika kwa uamuzi huu. Kama atatumbuliwa basi ni kwasababu za kisiasa tu.
 
Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na bodi ya shule ikakaa kikao cha dharura na kuja na maadhimio kadhaa pamoja na;
Mkuu haya yaliotokea Chidya una amini ni sawa na yale yaliyotokea Chunya? Labda tumeelewa vibaya kwani huku Chunya issue yote (sifa au mabaya ni kwa RC). Hivi vile viboko na kuchomwa shule ni kipi kilitangulia?
 
mkuu una matatizo ya kiakili, yaani mkuu wa mkoa aipangie mahakama cha kufanya? azuie mtuhumiwa kupewa dhamana halafu waita sawa? watanzania wengi ni vichaa by nature.
 
Sasa simu yako kushikwa ndio uchome bweni moto. Unachoma mahali pako pa kulala. Stupid
Idiot! Mkuu wa mkoa hana kazi ya kufanya mpaka aka-deal na mambo ua wanafunzi? Huyo ni mjinga anayefanya kazi isiyomhusu kabisa. Na wewe unazidi kumjaza ujinga.
 
Nyie kila kitu mnapinga tu, huo ndio uwendawazimu.
Kitu gani wewe umewahi kuunga mkono ndani ya serikali hii?
Wapo walioburuzwa mahakamani, na wengine kupewa adhabu ndogo ili waendelee na masomo.
mkuu una matatizo ya kiakili, yaani mkuu wa mkoa aipangie mahakama cha kufanya? azuie mtuhumiwa kupewa dhamana halafu waita sawa? watanzania wengi ni vichaa by nature.
 
mkuu una matatizo ya kiakili, yaani mkuu wa mkoa aipangie mahakama cha kufanya? azuie mtuhumiwa kupewa dhamana halafu waita sawa? watanzania wengi ni vichaa by nature.

Hao watoto wamefanya upumbavu mkubwa. Hiki ni kipindi cha vitoto vya 'viroba'. Hata hivyo viongozi wanapaswa kufuata sheria .... Sheria... Nothing but sheria. Hakuna miiko ya uongozi hivi Sasa ndio maana tunapata vimeo kama Chalamila. Look at the president himself!!! Unategemea nini? Ni MSIMU WA viongozi was hovyo.....
 
hao ndo watoto wanabidi walindwe na kutunzwa maana taifa limepoteza sana kizazi cha action.... na tukio hili liwe chachu ya kuibua mdahalo juu ya ulazima wa kuzuia matumizi ya simu shuleni... simu ni zaidi ya mawasiliano, teknolojia inakuja na hakuna wa kuizuia but why tunapambana na vitendo vya watoto kumiliki simu huku tukiwa tumezuia uhuru wa kujieleza kwa jamii...
 
Tuliosoma boarding miaka hiyo tunamwona RC kasimama imara na kutenda haki. Tukisema kila kosa tuburuzane mahakamani tutapoteza muda mwingi na fedha nyingi. Mwanafunzi wa secondary hata kama yuko advanced level anatazamwa tofauti na mwanafunzi wa chuo chochote kile.
hao ndo watoto wanabidi walindwe na kutunzwa maana taifa limepoteza sana kizazi cha action.... na tukio hili liwe chachu ya kuibua mdahalo juu ya ulazima wa kuzuia matumizi ya simu shuleni... simu ni zaidi ya mawasiliano, teknolojia inakuja na hakuna wa kuizuia but why tunapambana na vitendo vya watoto kumiliki simu huku tukiwa tumezuia uhuru wa kujieleza kwa jamii...
 
hao watoto ni jasiri sana, kama taifa tuige uthubutu wao...Mange kimambi angeelekeza nguvu zake kwa watoto kama hawa naamini tungekuwa mbali.......
U.F.S Joshua wong..
 
Form five na six wanachoma bweni. Maisha haya unamweka mzazi roho juu kutafuta pesa ya kulipa ujinga wako. Huyo mkuu wa mkoa amefanya vizuri kuwatandika.
Wengi wanao mponda mkuu wa mkoa nadhani labda hawajakulia bongo, kwanza mkuu kawapiga viboko 3 tu, Enzi hizo tumechapwa sana shuhleni but again Enzi hizo mtu mzima yoyote akikuona umekosa adabu anaweza kukuchapa, halafu watu na heshima zao leo wanamponda mkuu wa mkoa halafu watu hao hao wapo kimya kuhusu mabweni yaliochomwa; UPUMBAVU wa kiwango cha lami. Nipo pamoja na mkuu wa mkoa katika hili
 
Hao watoto wamefanya jambo la hovyo sana. Hata hivyo nasema Albert kachemsha!!! Mbeya sasa wamepata RC wa hovyo kabisa tangu Uhuru. Jiji la watu makini kama Mbeya kulipa RC mpuuzi kama Chalamila ni kama kuwadharau Wana_Mbeya. Time will tell. Pause!!!! NI MSIMU WA VIONGOZI WA HOVYO .....
 
mkuu kusoma boarding kielelezo cha wewe kuendelea kung'ang'ania sheria kinzani... hv mtoto kutumia simu wakati ambao si wa kipindi cha masomo ama muda wa kulala bwenini ni kosa? huona kuzuia simu ndo kunapelekea watoto kujitengenezea wiring system zao na kusababisha maafa ya moto? mkuu kama taifa tunatakiwa tukubali kuwa maendeleo yanakuja na kama katiba inaruhusu mtoto wa kike wa miaka 14-15 kuolewa why 18+ mwanafunzi asitumie simu? Tubadirike.
 
Mwaka 2008 Aprili wakati wa kufungua shule baada ya likizo fupi ya pasaka Chidya Secondary iliyopo wilayani Masasi mkoani Mtwara ulitokea mgomo uliosababishwa na wanafunzi kupikiwa uji usio na sukari kwa siku 2 mfululizo.

Wanafunzi wakaamua kufanya uharibifu wa mali za shule ikiwemo na gari kubwa (Lory) ya shule na kwa kulichoma moto na staff ya walimu ilichomwa moto kisha wanafunzi wote ukimwondoa mmoja tu ambaye alikuwa kiongozi wa nidhamu walikimbilia porini. Kenneth kijana alikuwa mlokole na ni mtoto wa mkuu wa wilaya mstaafu alibaki shule na walipokuja FFU walimzoa na kuondoka naye.

Asubuhi wanafunzi walianza kurejea taratibu na kujiandaa kisha kuingia darasani kama kawaida na shule ilipoa kimya.
Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na bodi ya shule ikakaa kikao cha dharura na kuja na maadhimio kadhaa pamoja na;

1.Kuwafukuza shule wanafunzi wachache.

2.Kuwasimamisha shule wanafunzi kadhaa na kuwaambia warudi na 150,000/= pindi wataporudi shule na wazazi wao.

3.Kila mwanafunzi aje na 75,000/= atakaporudi likizo ya Juni/Julai.

4.Baadhi ya viongozi wa wanafunzi na wanafunzi ambao walionekana kuwa ni wahamasishaji wakubwa wa mgomo ule kuburuzwa mahakamani baada ya kufukuzwa shule.
5.Shule haitafungwa kwa dharura na hatimaye wanafunzi waendelee na masomo mpaka Juni itakapofungwa kwa mujibu wa ratiba ya wizara ya elimu. Msimamo huu ulisimamiwa kikamilifu na headmaster nguli aliyekywa mjeshi Mr. Mwatenga.

Mkuu wa mkoa Albert Chalamila na timu yake wamefanya uamuzi nzuri sana ingawa wapo watakaoumizwa na kuathirika kwa uamuzi huu. Kama atatumbuliwa basi ni kwasababu za kisiasa tu.

Hao watoto wachapwe
 
Back
Top Bottom