Wana JF napendekeza kuwepo na maandamano ya vyama vyote vya siasa kutokea Mnazi Mmoja hadi Uwanja wa Taifa. Maandamano hayo yaongozwe na CCM, CHADEMA, CUF, NCCR, UDP, na vyama vingine. Wanachama wakae kwenye kundi la vyama vyao ili kujua chama kipi kina wanachama wengi. Hakuna kutoa posho wala usafiri kwa wanachama. Mwisho wa maandamano kuwepo na Hotuba za Wenyeviti wa Vyama kuzungumzia muskakabali wa siasa wa nchi hii na wito wa kudumisha amani na mshikamano. Pia, viongozi hao wakemee ufisadi kwa aina zake, na uvivu.
Nawasilisha.
Nawasilisha.