Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Wadau,
Imekuwa jadi kubwa humu na kwenye mitandao mingine ya kijamii (haswa facebook) kwa watu kumkatisha tamaa sana NAPE na juhudi zake za kukisafisha chama. Kazi hii ni ngumu na mnaelewa fika kwanini.
Binafsi ninachopingana na Nape kimsingi ni kitendo chake cha kuendesha 'Siasa za midako' badala ya siasa za uenezi unaokuwa informed na itikadi sahihi ya Chama. Lakini ukweli pia ni kwamba, Siasa hizi za 'mdako' Nape amezikuta, kwani zipo tangia Mwaka 1992 pale Azimio La Arusha lilipokufa, kulipisha azimio la Zanzibar. Tatizo langu kubwa na Nape ni hilo tu – kwamba hataki kukubali kwamba CCM haina tena DIRA. Nje ya hapo, Kijana huyu anajitahidi sana, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Hakuna kiongozi mwingine ndani ya Chama mwenye uthubutu wa kufanya anayofanya Nape, na haya hakuyaanza alipoteuliwa kuingia Kamati Kuu na kisha Ukatibu Uenezi, Siasa na Itikadi. Nape amekuwa ni kijana mwenye kiu ya mabadiliko tangia akiwa umoja wa vijana, jambo ambalo lilimjengea maadui wengi na wa kudumu. Vijana wengi bado wana imani na CCM kwa sababu ya uwepo wa watu kama Nape kwamba - ‘kumbe wapo viongozi wenye ujasiri wa kukemea chama kinapokosea au kulega lega'.
Vinginevyo nina uhakika kwamba, anachokifanya Nape leo hii ndani ya CCM, ni vijana wachache sana humu Jamii Forums wangekuwa na uthubutu huo, kwani hata katika mijadala humu, wengi hawaweki hata majina yao wala sura zao za kweli. Huku ni kukosa ujasiri kwa kile unachokiamini.
Nape ana mapungufu yake, na kwa upande wangu ni hayo niliyoyataja kwa mfano kuzunguka nchi nzima na kupokewa na vijana wa CCM wakitimua vumbi kwa shangwe wakiimba "Kauli Yetu ni Kulinda Ujamaa na Kujitegemea", na yeye akitabsamu huku akijua fika kwamba vijana wale wamepotoka. Hili ni ‘timing bomb' kwa CCM, kwani vijana hawa, pamoja na wazee na kina mama wengi kwenye uongozi huko kwenye matawi ya Chama wanaotembea na Azimio La Arusha Kama MSaafu au Biblia, wakija kubaini kwamba kwa miaka ishirini walikuwa wanadhania Wanachokiona ni Mwezi, Kumbe ni Nyota, huo ndio utakuwa mwisho wa CCM huko kwenye matawi, kwani nguvu ya chama ni matawi na mashina. Ni huko matawini ndiko kwenye wanachama, na ni huko ndiko vijana, wazee na kina mama kwa miama 20, wanadhania wanaona mwezi kumbe ni nyota. Ni muhimu katika mabadiliko ya katiba kwa CCM kuliangalia suala hili. CCM ilikuwa na nafasi nzuri ya kuweka mambo sawa kwa kufanya mabadiliko kidogo tu juu itikadi yake ili iachane na Ujamaa wa Marx-Lenin, na badala yake kuegemea kwenye Ujamaa wa Kidemokrasia (Social Democracy), bila ya kuleta athari zozote na maneno yoyote kisiasa, huku chama kikiendeleza mengi yake ya sasa kiuchumi, kijamii na kisiasa, bila bugudha. Lakini kwa bahati mbaya, CCK wameshaidaka itikadi hiyo kutokana na maelezo ambayo tumeyaona katika katiba yao ya mpito humu Jamii Forums.
Kwa wale ambao bado wana mapenzi na CCM (kwani imani inaweza kuwa imeisha), nadhani ni muhimu tukamweleza Nape mapungufu yake ni yepi, na changamoto zake ni zipi, huku tukitambua kwamba kibarua chake, na uthubutu wake wa sasa, wengi humu hatuwezi hata kujaribu. Nape alifikia hatua ya kutaka kuvuliwa uanachama wa UVCC, na uanachama wa CCM. Hatua zilishafikia mwisho kabisa. Sasa hata kama ni kweli alitaka kujiunga kwingine, why not iwapo maamuzi ya kukutimua yamekamilika lakini wewe bado unataka kuendelea kutetea maslahi ya taifa lako? Mwenzangu ungefanya nini?
Kibarua chake cha sasa ni cha kubadilisha Chama, na hii ni kazi nzito sana kwani katika organization yoyote, change ni kitu kigumu sana, hata iwe StarBucks, Apple, Microsost, au IBM. Hii ni kwa sababu mabadiliko ndani ya organization yoyote (CCM included), maana yake ni kubadilisha watu – kimtazamo, culture, attitudes, behavior, practice, norms, mambo ambayo yamejengeka ndani ya CCM kwa miaka zaidi ya 35 sasa, pengine hata Nape alikuwa hajazaliwa. Hata kwenye makampuni makubwa duniani, kila wanapohitaji kuleta change, huwa wanapata wakati mgumu sana, na suala hilo huwa linahitaji experts wanaolipwa fedha nyingi sana kusaidia mchakato huo, ambao mafanikio yake mara nyingi huwa ni ya kiwango kisichozidi 70%.
Mwisho, nia yangu hapa sio kusema CCM Saaaaafiiii, hapana, CCM ya sasa ni Chafu, inanuka. Lakini ni viongozi kama Nape ambao angalau wanatoa matumaini (hata kama ni hafifu) kwa vijana ambao bado wana mapenzi na CCM (sio lazima iwe imani), kwamba kumbe wapo wachache ndani ya CCM wenye mawazo tofauti. Nawaomba sana ndugu zangu, kama hamkubaliani na Nape, basi mfanye hivyo kwa hoja, sio matusi na kejeli kwa mtu ambae ni dhahiri anajitolea sana kujaribu kuleta mabadiliko ndani ya CCM. Vinginevyo hata umweke nani katika nafasi ya Nape, ataonekana ni kilaza tu! Lakini kilicho muhimu zaidi ni lengo la mhusika katika kufanikisha anayo yaamini, ambayo ni kwa maslahi ya CCM in the long run, regardless of the hurdles encountered now. Hata yeye akishindwa na kuondoka, wapo watakaoanzia pale alipoachia.
Wapo wengi wasiokubaliana na Mnyika, Mtatiro, n.k, lakini wanafanya hivyo kwa hoja, sio matusi na kejeli. Binafsi, ingawa kwangu mimi Mnyika stands to be one of the best leaders in our generation, bado ana mapungufu mengi tu ambayo from time huwa watu wanayaelezea kwa hoja, sio matusi na kejeli. Whether ni mapungufu ya Chadema, CCK, CUF, NCCR, CCM, kuyajadili kwa hoja itatujenga na kutufunza mengi sana, huku tukibakia na uanachama wetu wa vyama mbalimbali.
Vyama vya upinzani bado ni vichanga, havijafikia hatua ya kuhitaji kubadilika, lakini vitafikia huko kwani the only thing that is constant in an organization is 'change'. Tusubiri kuona mchakato huo kwenye vyama vya upinzani utapitia misuko suko gani. Vinginevyo ni dhahiri kwamba sakata la kina Hamad, Kafulila, Zitto, ni dalili za mwanzo za wimbi hilo katika vyama husika.
Otherwise, Do Not Speak Unless You Can Improve the Silence.
Imekuwa jadi kubwa humu na kwenye mitandao mingine ya kijamii (haswa facebook) kwa watu kumkatisha tamaa sana NAPE na juhudi zake za kukisafisha chama. Kazi hii ni ngumu na mnaelewa fika kwanini.
Binafsi ninachopingana na Nape kimsingi ni kitendo chake cha kuendesha 'Siasa za midako' badala ya siasa za uenezi unaokuwa informed na itikadi sahihi ya Chama. Lakini ukweli pia ni kwamba, Siasa hizi za 'mdako' Nape amezikuta, kwani zipo tangia Mwaka 1992 pale Azimio La Arusha lilipokufa, kulipisha azimio la Zanzibar. Tatizo langu kubwa na Nape ni hilo tu – kwamba hataki kukubali kwamba CCM haina tena DIRA. Nje ya hapo, Kijana huyu anajitahidi sana, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Hakuna kiongozi mwingine ndani ya Chama mwenye uthubutu wa kufanya anayofanya Nape, na haya hakuyaanza alipoteuliwa kuingia Kamati Kuu na kisha Ukatibu Uenezi, Siasa na Itikadi. Nape amekuwa ni kijana mwenye kiu ya mabadiliko tangia akiwa umoja wa vijana, jambo ambalo lilimjengea maadui wengi na wa kudumu. Vijana wengi bado wana imani na CCM kwa sababu ya uwepo wa watu kama Nape kwamba - ‘kumbe wapo viongozi wenye ujasiri wa kukemea chama kinapokosea au kulega lega'.
Vinginevyo nina uhakika kwamba, anachokifanya Nape leo hii ndani ya CCM, ni vijana wachache sana humu Jamii Forums wangekuwa na uthubutu huo, kwani hata katika mijadala humu, wengi hawaweki hata majina yao wala sura zao za kweli. Huku ni kukosa ujasiri kwa kile unachokiamini.
Nape ana mapungufu yake, na kwa upande wangu ni hayo niliyoyataja kwa mfano kuzunguka nchi nzima na kupokewa na vijana wa CCM wakitimua vumbi kwa shangwe wakiimba "Kauli Yetu ni Kulinda Ujamaa na Kujitegemea", na yeye akitabsamu huku akijua fika kwamba vijana wale wamepotoka. Hili ni ‘timing bomb' kwa CCM, kwani vijana hawa, pamoja na wazee na kina mama wengi kwenye uongozi huko kwenye matawi ya Chama wanaotembea na Azimio La Arusha Kama MSaafu au Biblia, wakija kubaini kwamba kwa miaka ishirini walikuwa wanadhania Wanachokiona ni Mwezi, Kumbe ni Nyota, huo ndio utakuwa mwisho wa CCM huko kwenye matawi, kwani nguvu ya chama ni matawi na mashina. Ni huko matawini ndiko kwenye wanachama, na ni huko ndiko vijana, wazee na kina mama kwa miama 20, wanadhania wanaona mwezi kumbe ni nyota. Ni muhimu katika mabadiliko ya katiba kwa CCM kuliangalia suala hili. CCM ilikuwa na nafasi nzuri ya kuweka mambo sawa kwa kufanya mabadiliko kidogo tu juu itikadi yake ili iachane na Ujamaa wa Marx-Lenin, na badala yake kuegemea kwenye Ujamaa wa Kidemokrasia (Social Democracy), bila ya kuleta athari zozote na maneno yoyote kisiasa, huku chama kikiendeleza mengi yake ya sasa kiuchumi, kijamii na kisiasa, bila bugudha. Lakini kwa bahati mbaya, CCK wameshaidaka itikadi hiyo kutokana na maelezo ambayo tumeyaona katika katiba yao ya mpito humu Jamii Forums.
Kwa wale ambao bado wana mapenzi na CCM (kwani imani inaweza kuwa imeisha), nadhani ni muhimu tukamweleza Nape mapungufu yake ni yepi, na changamoto zake ni zipi, huku tukitambua kwamba kibarua chake, na uthubutu wake wa sasa, wengi humu hatuwezi hata kujaribu. Nape alifikia hatua ya kutaka kuvuliwa uanachama wa UVCC, na uanachama wa CCM. Hatua zilishafikia mwisho kabisa. Sasa hata kama ni kweli alitaka kujiunga kwingine, why not iwapo maamuzi ya kukutimua yamekamilika lakini wewe bado unataka kuendelea kutetea maslahi ya taifa lako? Mwenzangu ungefanya nini?
Kibarua chake cha sasa ni cha kubadilisha Chama, na hii ni kazi nzito sana kwani katika organization yoyote, change ni kitu kigumu sana, hata iwe StarBucks, Apple, Microsost, au IBM. Hii ni kwa sababu mabadiliko ndani ya organization yoyote (CCM included), maana yake ni kubadilisha watu – kimtazamo, culture, attitudes, behavior, practice, norms, mambo ambayo yamejengeka ndani ya CCM kwa miaka zaidi ya 35 sasa, pengine hata Nape alikuwa hajazaliwa. Hata kwenye makampuni makubwa duniani, kila wanapohitaji kuleta change, huwa wanapata wakati mgumu sana, na suala hilo huwa linahitaji experts wanaolipwa fedha nyingi sana kusaidia mchakato huo, ambao mafanikio yake mara nyingi huwa ni ya kiwango kisichozidi 70%.
Mwisho, nia yangu hapa sio kusema CCM Saaaaafiiii, hapana, CCM ya sasa ni Chafu, inanuka. Lakini ni viongozi kama Nape ambao angalau wanatoa matumaini (hata kama ni hafifu) kwa vijana ambao bado wana mapenzi na CCM (sio lazima iwe imani), kwamba kumbe wapo wachache ndani ya CCM wenye mawazo tofauti. Nawaomba sana ndugu zangu, kama hamkubaliani na Nape, basi mfanye hivyo kwa hoja, sio matusi na kejeli kwa mtu ambae ni dhahiri anajitolea sana kujaribu kuleta mabadiliko ndani ya CCM. Vinginevyo hata umweke nani katika nafasi ya Nape, ataonekana ni kilaza tu! Lakini kilicho muhimu zaidi ni lengo la mhusika katika kufanikisha anayo yaamini, ambayo ni kwa maslahi ya CCM in the long run, regardless of the hurdles encountered now. Hata yeye akishindwa na kuondoka, wapo watakaoanzia pale alipoachia.
Wapo wengi wasiokubaliana na Mnyika, Mtatiro, n.k, lakini wanafanya hivyo kwa hoja, sio matusi na kejeli. Binafsi, ingawa kwangu mimi Mnyika stands to be one of the best leaders in our generation, bado ana mapungufu mengi tu ambayo from time huwa watu wanayaelezea kwa hoja, sio matusi na kejeli. Whether ni mapungufu ya Chadema, CCK, CUF, NCCR, CCM, kuyajadili kwa hoja itatujenga na kutufunza mengi sana, huku tukibakia na uanachama wetu wa vyama mbalimbali.
Vyama vya upinzani bado ni vichanga, havijafikia hatua ya kuhitaji kubadilika, lakini vitafikia huko kwani the only thing that is constant in an organization is 'change'. Tusubiri kuona mchakato huo kwenye vyama vya upinzani utapitia misuko suko gani. Vinginevyo ni dhahiri kwamba sakata la kina Hamad, Kafulila, Zitto, ni dalili za mwanzo za wimbi hilo katika vyama husika.
Otherwise, Do Not Speak Unless You Can Improve the Silence.