Ndugu zangu naomba msome ibara hii niliyoinukuu kutoka kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Angalieni ibara ya 54(5) na mnisaidie kuielewa,hainiingii akilini.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
_________________________________________________________________
Baraza la Mawaziri na Serikali
Baraza la
Mawaziri
Sheria ya
1984 Na.15
ibara 9
Sheria Na.4
ya 1992 ib
Sheria Na.34
ya 1994 ibara
12
54.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe
wake watakuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais wa
Zanzibar na Mawaziri wote.
(2) Rais atahudhuria mikutano ya Baraza la Mawaziri na ndiye
atkayeongoza mikutano hiyo. Na endapo Rais hayupo basi
mikutano itaongozwa na Makamu wa Rais na kama wote wawili
Rais na Makamu wa Rais hawapo Waziri Mkuu ndiye ataongoza
Mikutano hiyo.
(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara ya 37(1) ya
Katiba hii, Baraza la Mawaziri litakuwa ndicho chombo kikuu cha
kumshauri Rais juu ya mambo yote yanayohusika na utekelezaji
wa madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, na
litamsaidia na kumshauri Rais juu ya jambo lolote
litakalowasilishwa kwenye Baraza hilo kwa mujibu wa maagizo
maalum au maagizo ya jumla yatakayotolewa na Rais.
(4) Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahudhuria mikutano yote
ya Baraza la Mawaziri na atakuwa na haki zote za mjumbe wa
mikutano hiyo isipokuwa hatakuwa na haki ya kupiga kura katika
mikutano hiyo.
(5) Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa
na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katika
mahakama yoyote.
Utata unakuja hapa:-
Je,Mkataba wa Dowans-Richmond ulijadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri?
Kama jibu ni Ndiyo, Je ulikuwa ni ushauri wa Baraza la Mawaziri kwa Rais?
Kama jibu ni Ndiyo, Je Rais alikubali kwa hiari yake kwa mujibu wa masharti yaliyomo katika ibara ya 37(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Kama jibu ni ndiyo, Je Mkataba huu ni halali?
Kama jibu ni hapana, Je tutashitaki kwa nani ili hali imeandikwa katika ibara ya 54(5) kuwa ''Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa
na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katika
mahakama yoyote.
Jamani hiki si kiini macho? Au yawezekana hawa Richmond-Dowans walishazisoma sheria zetu wakaona udhaifu na sasa wanatuadhibu kwa kutunyonya bara-bara kwa kujua hatuna pa kushtaki? na kwamba hata tukishtaki, jambo hilo halitachunguzwa katika mahakama yoyote?
Au yawezekana tunamtafuta mbaya wetu ili hali mbaya wetu ni Sheria zetu wenyewe?
Kweli napata utata, naombeni ufafanuzi!
Maoni yangu: KAMA NA NINYI NDUGU ZANGU MTAPATA UTATA, BASI MABADILIKO YA KUPATA KATIBA MPYA NI YA LAZIMA!
Chanzo:KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA YA MWAKA 1977
(Toleo hili la Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya Mwaka 1977,
limezingatia na kuweka pamoja mabadiliko yote yaliyofanywa katika Katiba
ya Muungano tangu ilipotungwa mwaka 1977 hadi tarehe 30 Aprili, 2000).
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
_________________________________________________________________
Baraza la Mawaziri na Serikali
Baraza la
Mawaziri
Sheria ya
1984 Na.15
ibara 9
Sheria Na.4
ya 1992 ib
Sheria Na.34
ya 1994 ibara
12
54.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe
wake watakuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais wa
Zanzibar na Mawaziri wote.
(2) Rais atahudhuria mikutano ya Baraza la Mawaziri na ndiye
atkayeongoza mikutano hiyo. Na endapo Rais hayupo basi
mikutano itaongozwa na Makamu wa Rais na kama wote wawili
Rais na Makamu wa Rais hawapo Waziri Mkuu ndiye ataongoza
Mikutano hiyo.
(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara ya 37(1) ya
Katiba hii, Baraza la Mawaziri litakuwa ndicho chombo kikuu cha
kumshauri Rais juu ya mambo yote yanayohusika na utekelezaji
wa madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, na
litamsaidia na kumshauri Rais juu ya jambo lolote
litakalowasilishwa kwenye Baraza hilo kwa mujibu wa maagizo
maalum au maagizo ya jumla yatakayotolewa na Rais.
(4) Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahudhuria mikutano yote
ya Baraza la Mawaziri na atakuwa na haki zote za mjumbe wa
mikutano hiyo isipokuwa hatakuwa na haki ya kupiga kura katika
mikutano hiyo.
(5) Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa
na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katika
mahakama yoyote.
Utata unakuja hapa:-
Je,Mkataba wa Dowans-Richmond ulijadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri?
Kama jibu ni Ndiyo, Je ulikuwa ni ushauri wa Baraza la Mawaziri kwa Rais?
Kama jibu ni Ndiyo, Je Rais alikubali kwa hiari yake kwa mujibu wa masharti yaliyomo katika ibara ya 37(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Kama jibu ni ndiyo, Je Mkataba huu ni halali?
Kama jibu ni hapana, Je tutashitaki kwa nani ili hali imeandikwa katika ibara ya 54(5) kuwa ''Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa
na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katika
mahakama yoyote.
Jamani hiki si kiini macho? Au yawezekana hawa Richmond-Dowans walishazisoma sheria zetu wakaona udhaifu na sasa wanatuadhibu kwa kutunyonya bara-bara kwa kujua hatuna pa kushtaki? na kwamba hata tukishtaki, jambo hilo halitachunguzwa katika mahakama yoyote?
Au yawezekana tunamtafuta mbaya wetu ili hali mbaya wetu ni Sheria zetu wenyewe?
Kweli napata utata, naombeni ufafanuzi!
Maoni yangu: KAMA NA NINYI NDUGU ZANGU MTAPATA UTATA, BASI MABADILIKO YA KUPATA KATIBA MPYA NI YA LAZIMA!
Chanzo:KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA YA MWAKA 1977
(Toleo hili la Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya Mwaka 1977,
limezingatia na kuweka pamoja mabadiliko yote yaliyofanywa katika Katiba
ya Muungano tangu ilipotungwa mwaka 1977 hadi tarehe 30 Aprili, 2000).