kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,666
- 4,365
Mwenzenu nimekuwa na tatizo la kukoroma saana usiku mpaka imekuwa kero kwa mke wangu. Kuna kipindi alikuwa ana lalamika eti namkosesha usingizi kwasababu ya kukoroma kwangu.
Nilibisha nikaona anaanza vituko, nikampiga mkwara usiku huu nilivyokuwa nimelala amerecord video fulani yangu nikiwa usingizini na kuniamsha.
Nilivyoamka akaniambia kuwa amechoka, anakosa usingizi kwasababu ya kulala kwangu. Nikataka kupiga mkwara kama kawaida yangu akanionyesha video, kuangalia hivi ni mimi kweli.
Nakoroma kama vile mtu ambaye ana maji kwenye koo, nikashindwa la kusema.
Naomba msaada kwa yeyote ambaye anaweza jua tatizo hili linachangiwa na nini na dawa yake ni nini.
Naomba anisaidie mwenzenu ndoa yangu mbichi kabisa lakini kwa style hii naona hatuna marefu uko mbeleni. Mimi situmii pombe, au sina kitambi sasa sijui tatizo litakuwa wapi?!
Sent using Jamii Forums mobile app
Nilibisha nikaona anaanza vituko, nikampiga mkwara usiku huu nilivyokuwa nimelala amerecord video fulani yangu nikiwa usingizini na kuniamsha.
Nilivyoamka akaniambia kuwa amechoka, anakosa usingizi kwasababu ya kulala kwangu. Nikataka kupiga mkwara kama kawaida yangu akanionyesha video, kuangalia hivi ni mimi kweli.
Nakoroma kama vile mtu ambaye ana maji kwenye koo, nikashindwa la kusema.
Naomba msaada kwa yeyote ambaye anaweza jua tatizo hili linachangiwa na nini na dawa yake ni nini.
Naomba anisaidie mwenzenu ndoa yangu mbichi kabisa lakini kwa style hii naona hatuna marefu uko mbeleni. Mimi situmii pombe, au sina kitambi sasa sijui tatizo litakuwa wapi?!
Sent using Jamii Forums mobile app